Yusufu(a.s) Atupwa afungwa Gerezani
Mkewe Al-Aziz hakumkatia tamaa Yusufu(a.
Yusufu(a.s) Atupwa Gerezani
Mkewe Al-Aziz hakumkatia tamaa Yusufu(a.s). Uovu wake ulimchochea kuzidi kumuandama Yusufu(a.s). Alimpa Yusufu chaguzi mbili: Ama akubali kuzini naye au amfanyie hila atiwe gerezani.
................Na kama hatafanya ninalomuarisha, hakika atafungwa gerezani na atakuwa miongoni mwa madhalili(12:32)
Kwa kumukhofu Allah(s.w) na kuchukia tendo chafu la zinaa, Yusufu akasema Ee Mola wangu! Nastahabu zaidi gereza kuliko haya wanayoniitia........(12:33)
Maisha ya Yusufu(a.s.) Gerezani
Yusufu(a.s) alijikuta yupo gerezani, si kama mhalifu bali aliyeonewa kwa uadilifu na uaminifu wake. Lakini pia hakusononeneka kwa dhulma ile aliyofanyiwa kwani kuwepo gerezani kulimtenga na watu waovu waliotaka kumtia kwenye uchafu.
Uadilifu na sifa zake njema zilikuwa zimezagaa kila mahali. Hata alipoingia gerezani wafungwa wenzake walimpa heshima ya pekee. Walikiri kwamba Yusufu(a.s) ni miongoni mwa watu wazuri.
Yusufu Afikisha Ujumbe wa Uislamu kwa Wafungwa
Ilitokea kule gerezani wafungwa wenzake wakaota ndoto na kumtaka Yusufu(a.s) awape tafsiri yake.
Na wakaingia pamoja naye gerezani vijana wawili. Mmoja wao akasema: Hakika nimeona (katika ndoto) nakamua ulevi”; na mwingine akasema: Hakika nimeona(katika) ndoto nabeba mikate juu ya kichwa changu ambayo ndege wanaila. Tuambie tafsiri yake; kwa yakini sisi tunakuona wewe ni miongoni mwa watu wazuri(12:36)
Yusufu(a.s) aliwakubalia ombi lao lakini kabla ya kuwatafsiria ndoto zao aliwalingania kwa Allah(s.w) kwakuwauliza:
“Enyi wafungwa wenzangu wawili! Je, waungu wengi wanaofarikiana ndio bora (kuabudiwa) au Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu (juu ya kila kitu?)” (12:39).
Hamuabudu badala yake (Mwenyezi Mungu) ila majina (matupu) mliyopanga nyinyi wenyewe na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuteremsha dalili kwa hayo. Haikuwa hukumu ila hii ya Mwenyezi Mungu tu; ameamrisha msimuabudu yoyote isipokuwa Yeye tu. Hiyo ndiyo Dini iliyonyooka lakini watu wengi hawajui.” (12:40).
Baada ya kuwafikishia ujumbe huu muhimu, Nabii Yusufu (a.s) akaanza kuwaeleza taawili ya ndoto zao kuwa:
Enyi wafungwa wenzangu wawili! Mmoja katika ninyi atarejeshwa kazini kwake akamnyweshe bwana wake ulevi. na yule mwingine atauawa kwa kusulubiwa, na ndege watamla kichwa chake. Limekwishakatwa (huko kwa Firaun) hili jambo mlilokuwa mkiuliza (12:41)
Kisha Yusufu(a.s) akamuomba yule atakayetolewa gerezani:
“...........Unikumbuke mbele ya bwana wako;(umwambie kuwa nimeonewa nimefungwa bure); Lakini shetani alimsahaulisha kumkumbusha bwana wake. kwa hivyo akakaa gerezani (Nabii Yusufu) baadhi ya miaka (baada ya hapa)(12:42)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 ai web app 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
CHANZO CHA VITA VYA VITA VYA AL-FIJAR NA ATHARI ZAKE
MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU).
Soma Zaidi...Kusilimu kwa Wachawi wa Firaun
Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as).
Soma Zaidi...Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)
Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s.
Soma Zaidi...Ukasha bin Mihsan ni Sahaba aliyechangamkia Fursa
Katika somo hili utakwnda kujifunz anamna nambavyo Sahaba Ukasha alivyochangamkia fursa katika mambo ya heri
Soma Zaidi...