Yusufu(a.s) Atupwa afungwa Gerezani

Mkewe Al-Aziz hakumkatia tamaa Yusufu(a.

Yusufu(a.s) Atupwa afungwa Gerezani

Yusufu(a.s) Atupwa Gerezani


Mkewe Al-Aziz hakumkatia tamaa Yusufu(a.s). Uovu wake ulimchochea kuzidi kumuandama Yusufu(a.s). Alimpa Yusufu chaguzi mbili: Ama akubali kuzini naye au amfanyie hila atiwe gerezani.

................Na kama hatafanya ninalomuarisha, hakika atafungwa gerezani na atakuwa miongoni mwa madhalili(12:32)

Kwa kumukhofu Allah(s.w) na kuchukia tendo chafu la zinaa, Yusufu akasema Ee Mola wangu! Nastahabu zaidi gereza kuliko haya wanayoniitia........(12:33)


Maisha ya Yusufu(a.s.) Gerezani


Yusufu(a.s) alijikuta yupo gerezani, si kama mhalifu bali aliyeonewa kwa uadilifu na uaminifu wake. Lakini pia hakusononeneka kwa dhulma ile aliyofanyiwa kwani kuwepo gerezani kulimtenga na watu waovu waliotaka kumtia kwenye uchafu.



Uadilifu na sifa zake njema zilikuwa zimezagaa kila mahali. Hata alipoingia gerezani wafungwa wenzake walimpa heshima ya pekee. Walikiri kwamba Yusufu(a.s) ni miongoni mwa watu wazuri.



Yusufu Afikisha Ujumbe wa Uislamu kwa Wafungwa


Ilitokea kule gerezani wafungwa wenzake wakaota ndoto na kumtaka Yusufu(a.s) awape tafsiri yake.

Na wakaingia pamoja naye gerezani vijana wawili. Mmoja wao akasema: Hakika nimeona (katika ndoto) nakamua ulevi'; na mwingine akasema: Hakika nimeona(katika) ndoto nabeba mikate juu ya kichwa changu ambayo ndege wanaila. Tuambie tafsiri yake; kwa yakini sisi tunakuona wewe ni miongoni mwa watu wazuri(12:36)



Yusufu(a.s) aliwakubalia ombi lao lakini kabla ya kuwatafsiria ndoto zao aliwalingania kwa Allah(s.w) kwakuwauliza:

'Enyi wafungwa wenzangu wawili! Je, waungu wengi wanaofarikiana ndio bora (kuabudiwa) au Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu (juu ya kila kitu?)' (12:39).




Hamuabudu badala yake (Mwenyezi Mungu) ila majina (matupu) mliyopanga nyinyi wenyewe na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuteremsha dalili kwa hayo. Haikuwa hukumu ila hii ya Mwenyezi Mungu tu; ameamrisha msimuabudu yoyote isipokuwa Yeye tu. Hiyo ndiyo Dini iliyonyooka lakini watu wengi hawajui.' (12:40).

Baada ya kuwafikishia ujumbe huu muhimu, Nabii Yusufu (a.s) akaanza kuwaeleza taawili ya ndoto zao kuwa:




Enyi wafungwa wenzangu wawili! Mmoja katika ninyi atarejeshwa kazini kwake akamnyweshe bwana wake ulevi. na yule mwingine atauawa kwa kusulubiwa, na ndege watamla kichwa chake. Limekwishakatwa (huko kwa Firaun) hili jambo mlilokuwa mkiuliza (12:41)



Kisha Yusufu(a.s) akamuomba yule atakayetolewa gerezani:

'...........Unikumbuke mbele ya bwana wako;(umwambie kuwa nimeonewa nimefungwa bure); Lakini shetani alimsahaulisha kumkumbusha bwana wake. kwa hivyo akakaa gerezani (Nabii Yusufu) baadhi ya miaka (baada ya hapa)(12:42)



                   

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 167

Post zifazofanana:-

Rangi za majimaji yanayotoka kwenye uke na maana yake kiafya
Je unajuwa kuwa majimaji yanayotoka ukeni yanatueleza mengi kuhusu afya yako, rangi za majimaji ya ukeni na damu ya hedhi Soma Zaidi...

Swala ya kupatwa kwa jua na mwezi na namna ya kuiswali
11. Soma Zaidi...

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya
Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

Fahamu vitamini C na kazi zake, vyakula vya vitamini C na athari za upungufu wake.
kuhusu vitamini C, kuanzia chanzo chake, maana yake, upungufu wake na kazi zake kwenye miili yetu. Soma Zaidi...

quran na sayansi
Soma Zaidi...

DUA 21 - 31
21. Soma Zaidi...

NAMNA YA KUSWALI
13. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ibrahiim(a.s)
Soma Zaidi...

Watu wanaowajibikiwa kuhiji
Soma Zaidi...

Ni nini maana ya ndoa?
Soma Zaidi...

Hukumu na taratibu za mirathi na kurithi katika uislamu
Soma Zaidi...

Sharti za kutoa zaka
Masharti ya Utoaji wa Zakat na Swadaqat Utoaji katika njia ya Allah (s. Soma Zaidi...