picha

Nabii Ibrahiim(a.s) Kumlingania Uislamu Baba Yake

Baada ya NabiiIbrahiim(a.

Nabii Ibrahiim(a.s) Kumlingania Uislamu Baba Yake

Nabii Ibrahiim(a.s) Kumlingania Uislamu Baba Yake


Baada ya NabiiIbrahiim(a.s) kutoa shahada ya kweli alipomuahidi Mola wake: “Nimejisalimisha kwa Bwana Mlezi wa Walimwengu Wote” alianza kulingania Tawhiid kwa watu wa jamii yake. Kwa hekima aliona aanze kumlingania baba yake, aliyekuwa mchonga masanamu na kiongozi wa Ibada ya masanamu. Alianza kumlingania kwa kutumia hoja zenye mashiko katika akili ya mwanaadamu kama ifuatavyo:



(Wakumbushe) alipomwambia baba yake: “Ewe baba yangu! Kwa nini unaabudu visivyosikia na visivyoona na visivyofaa chochote?” (19:42)



“Ewe baba yangu! Kwa yakini imenijia ilimu isiyokujia. Basi nifuate nitakuongoza njia iliyo sawa.(19:43)



Ewe baba yangu! Usimuabudu Shetani, hakika Shetani ni mwenye kumuasi (Mwenyezi Mungu) Mwingi wa rehema.(19:44)



“Ewe baba yangu! Hakika naogopa kukupata adhabu inayotoka kwa Mwingi wa rehema (Mwenyezi Mungu), (ukifanya hivyo) utakuwa mwenziwe shetani.” (19:45)



Babu yake, badala ya kuyatia akilini aliyofikishiwa na mwanawe, alimkemea, kumtisha na badaye kumfukuzilia mbali nyumbani kwake.



“Akasema (yule baba yake) “Je! Unaichukia miungu yangu, ewe Ibrahim? Kama huachi (haya unayosema) lazima nitakupiga mawe. Na niondokelee mbali kwa muda mchache (huu).” (19:46)



Nabii Ibrahim(a.s)hakutetereka na kurudi nyuma alipofukuzwa nyumbani mwa baba yake. Alibakia na msimamo wake wa kulingania Dini ya Allah(s.w) kwa moyo mkunjufu huku akitarajia msaada kutoka kwake Allah(s.w) pekee.



“Na mimi nakuondokeeni (na kujiepusha) na mnayoyaabudu kinyume cha Mwenyezi Mungu. Hakika sitakuwa mwenye kukhibu (kukosa ninalotaka) kwa kumuomba Mola wangu.” (19:48).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1656

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake

Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a.

Soma Zaidi...
Historia ya Firaun, Qarun na Hamana

Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a.

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”.

Soma Zaidi...
Watu waliovunja amri ya kuheshimu siku ya Jumamosi.

Katika zama za kale Mayahudi walikatazwa kufanya kazi siku ya Jumamosi.

Soma Zaidi...