picha

Bara la Arabu Zama za Jahiliyyah

Wakati Mtume(s.

Bara la Arabu Zama za Jahiliyyah

Bara la Arabu Zama za Jahiliyyah
Zama za Jahiliyyah ni zile zama ambazo watu walikuwa wakiendesha maisha yao ya kibinafsi na kijamii kwa kufuata matashi yao kinyume na mwongozo wa Allah(s.w) na mitume wake.



Wakati Mtume(s.a.w) anazaliwa katika karne ya Sita (570 A.D) dunia ilikuwa katika giza totoro la ujahili. Wakazi wa Bara Arab, katika kipindi hicho walikuwa chini sana katika maadili. Ubabe, unyang’anyi na uporaji mali ya misafara ya biashara yalionekana matendo ya kishujaa na ya kujivunia. Wanyonge hawakuwa na haki, wanawake walinyanyaswa na kudhalilishwa hadi kufikia watoto wa kike kuzikwa wangali hai na wanawake kurithiwa kwa nguvu kama ilivyorithiwa mali.



Kwa muhtasari hali ya Bara Arab wakati huo ilikuwa kama alivyoeleza Jaffari bin Abu Twalib mbele ya Mfalme Najash wa Uhabesh:

“Ewe Mfalme, sisi tulikuwa waovu na majahili, tukiabudia masanamu na kula nyamafu hata mizoga ya wanyama waliokufa wenyewe.Tulifanya kila aina ya matendo machafu na ya aibu. Hatukuwa wenye kuwajibika kwa jirani na jamaa zetu. Wenye nguvu miongoni mwetu waliwakandamiza wanyonge. Kisha Allah akamleta Mtume miongoni mwetu ambaye tulimfahamu vema kwa nasaba yake, utukufu wake na uzuri wa tabia yake adhimu. Alituita tumuabudu Mungu mmoja tu na akatukataza kuabudia masanamu na mawe. Alitufundisha kusema ukweli kutunza amana, kuwaangalia ndugu na jamaa na kuwafanyia wema na kuacha maovu. Alituamrisha kusimamisha swala na kutoa Zakat. Alituamrisha kujiepusha na maovu na kujiepusha na umwagaji damu. Alitukataza zinaa, kusema uwongo, kula mali ya yatima na kuwasingizia uovu wanawake watwaharifu.
Alitufundisha Qur-an...” 4 (A Guillaume – The life of Muhammad).



Hali hii ya ujahili haikutawala Bara Arab peke yake, bali katika karne hii ya 6 A.D ulimwengu wote, Mashariki na Magharibi, ulizama katika giza totoro la uovu na ujahili. Ulimwengu katika zama hizo, wanyonge na watu wa chini walikandamizwa na kudhulumiwa pasina chembe ya huruma na wenye uwezo na watukufu miongoni mwao.



Katika kipindi hicho, hata wale waliodai kufuata mafundisho ya Mitume wa Mwenyezi Mungu, Mayahudi na Wakristo, walikuwa katika giza hilo hilo la uovu na ujahili. Mayahudi waliacha mafundisho ya Mtume wao na wakaamua kuishi kulingana na matamanio ya nafsi zao. Walipotokea Mitume waliwafanyia maovu mengi kama ilivyobainishwa katika Qur-an. Wakristo nao waliacha mafundisho sahihi ya Nabii Isa(a.s) badala yake wakafuata ushirikina wa Warumi. Walileta uzushi mwingi juu ya Dini ya Allah(s.w) kama tunavyojifunza katika Qur-an:




“Na Mayahudi wanasema: ‘Uzeiri ni Mwana wa Mwenyezi Mungu’ na Wakristo wanasema; ‘Masihi ni Mwana wa Mwenyezi Mungu’; haya ndiyo wayasemayo kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya wale waliokufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa! (9:30)



Wamewafanya Wanavyuoni wao na Watawa wao kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu, na wamemfanya Masihii Mwana wa Maryamu (pia Mungu) hali hawakuamrishwa isipokuwa kumuabudu Mungu mmoja, hakuna anayestahiki kuabudiwa ila Yeye. Ametakasika na yale wanayomshirikisha nayo.” (9:31).





“Enyi Mlioamini! Wengi katika Makasisi (Wanavyuoni wa Mayahudi na wakristo) na Watawa (wao) wanakula mali za watu kwa batili na kuwazuilia njia ya Mwenyezi Mungu..........” (9:34)



Katika kipindi hicho cha historia utawala wa Kikristo Ulaya Magharibi uliwakandamiza na kuwanyonya wanyonge kama utawala wa kishirikina ulivyokuwa ukifanya huko Mashariki ya Kati na Mashariki ya mbali. Katika kipindi hiki wanasayansi walioibuka na ugunduzi ulio kinyume na maelezo ya Wakuu wa Kanisa walisulubiwa na kuuliwa kinyama miongoni mwao ni mwanasayansi maarufu, Galileo.




                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2537

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 web hosting    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)

LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).

Soma Zaidi...
Ukasha bin Mihsan ni Sahaba aliyechangamkia Fursa

Katika somo hili utakwnda kujifunz anamna nambavyo Sahaba Ukasha alivyochangamkia fursa katika mambo ya heri

Soma Zaidi...
Maandalizi ya Kimafunzo aliyoandaliwa Mtume Muhammad

(i) Suratul- ‘Alaq (96:1-5)“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba Aliyemuumba mwanaadamu kwa ‘alaq.

Soma Zaidi...
tarekh 4

KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji.

Soma Zaidi...
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu

KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.

Soma Zaidi...