Usuluhishaji wa walio dhurumiwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela
USULUHISHAJI WA WALODHULUMIWA.
Basi baada ya kusikiliza hadithi hizi mfalme akaanza usuluhishi na kumwambia Zubeidah achome huo unywele ili amuite jini binti mfalme. Basi Zubeidah akauchoma huo unywele na baada ya punde akaja jini yule na mfalme akataka msamaha kwa mabinti walogeuzwa mbwa, basi akawambwagia maji na wakageuka kuwa watu. Pia bint mfalme akazungumza kuwa alomfanyia unyama Amina ni mwanao mwenyewe ewe mfalme ni kuwa mtoto wako alimpenda Amina na kumposa na ndoa aliifanya kwa siri na hatimaye mambo yakawa hivyo. Basi jini akaondoka.
Mfalme akamuita mwanae na kumuuliza yalotokea na akamjibu kama mambo yalivyo elezwa. Basi akatoa amri mrejee mkewe na kisha Zubeidah ana dada zake akawaozesha kwa wale machongo watatu na yeye mwenyewe mfalme akamuoa Sadie. Inasemekana ndoa zao zilikuwa ni za upendo wa hali ya juu na hakukutokea ugomvi mpaka Allah akapitisha amri yake.
Baada ya Schehra-zade kumaliza kusimulia hadithi hii Dinar-zade alifurahi sana. Lakini furaha hii haikumzidi sultani. Hapo Schehra-zade akamwambia basi hadithi hii haifiki hadithi ya Sinbad mwenda baharini. Sultani akuliza ni kipi kilompata sinbad mwenda baharini hata hadithi yake ikawa nzuri hivyo? Hapo Schehra-zade akaanza kusimulia hadithi hii;-
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 ai web app 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
HADITHI YA CHONGO WA KWANZA MTOTO WA MFALME
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA CHONGO WA KWANZA MTOTO WA MFALME kwanza utambue mimi ni mtoto wa mfalme na ni wa kipekee katika uzawa.
Soma Zaidi...Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela
Soma Zaidi...Safari ya majibu juu ya maswali mawili
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela
Soma Zaidi...Hadithi ya binti wa kwanza na mbwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela
Soma Zaidi...Kitabu Cha hadithi ya Chongo
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.
Soma Zaidi...