Hadithi ya chongo wa tatu mtoto wa mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

HADITHI YA CHONGO WA TATU MTOTO WA MFALME

Mimi ni mtoto wa mfalme kama nilivyotangulia kusema na ni mtoto wa kipekee kwa baba na mama. Nilipewa taaluma nyingi na wazazi wangu na nilifahamu vizuri. Nilifundishwa sayansi, maarifa ya mazingira, simulizi na biashara. Kwa upande wangu nilipenda sana uandishi na nilikuwa na muandiko mzuri sana hata niliwashinda waandishi wote nilowahi kukutana nao. Uzuri wa muandiko wangu ulifika mbali sana hata nikawa ninaa ndika barua zote za mfalme kwenye nchi za majirani.

 

Ilitokea sikumoja nikaandika barua iliyotakiwa kuenda nchi za hindi kwa mfalme wa wahindi. Niliandika barua ile kwa ufndi wa hali ya juu na ikatumwa kwa mfalme wa hindi. Taarifa zikatujia baada ya miezi kadhaa kuwa mfalme wa wahidi amestaajabishwa sana na uzuri wa mwandiko wa barua ile hivyo akataka amuone mwandishi huyo na alitowa zawadi nyingi kwa mfalme wa nchi yetu yaani baba yangu ili aniruhusu niende uhindini akanione.

 

Baba alifurahihwa sana n barua ile na mimi pia nilifurahi japo nilisita kuenda hindi. Kwa zawadi alizopokea baba aliniomba niende na kuniambia huenda nikajifunza mambo mengi ambayo pale nchini kwetu hakuna. Baba alichagua walinzi wazur kwa ajili ya kuulinda msafara wetu kwani safari ilikuwa ni ndefu na yenye ugumu pia.

 

Basi ilibidi nikubaliane na mawazo ya baba ya kwenda nchi ya wahindi chini ya ombila mfalme wa watu nwa hindi. Baada ya siku 10 safari ilianza kuelekea uhindini. Safari ilikuwa nchema na yenye amani. Tuliweza kupita kwenye majangwa na misitu. Tulivuka mito na mabwawa ya kuvutia na kupendeza. Nilifurahishwa na safari na kujiahidi mwenyewe kuwa kwa hakika nitajifunza mengi huku niendko.

 

Tulitembea bila ya dharuba kwa siku 15 na tulilala siku hiyo katika eneo la jangwa lenye mlima wa michana na vichuguu vya hap na pale. Bila ya kujua lolte kumbe kulikuwa na wavamizi wanatuchunguza. Asubuhi ya siku ilofata tuliondoka pale na tukapita kwenye ponde lililochimbika. Wale wavamizi walikaa juu ya bonde na kutuacha sisis tunapita chini yake. Ghafla wakaanza kutushambulia na wengi katika sisi wakapoteza maisha. Kila mtu akaanza kukimbia upande wake kuokoa maisha yake.

 

Kwa upande wangu sikuona hata askari aliyekuwa akinikinga. Basi nikavua yale mavazi ya watoto wa wafalme na kuwatupia wavamizi na nikaanza kukimbia. Hii ilikuwa ni salama yangu kwani mavazi yale yana thamani kubwa hivyo wasingethubutu kuniachia. Nilikimbia bila ya kujua ninakoelekea mpaka niliposilkia sauti ya jogoo akiwika. Kwa mbali nikasikia sauti ya pungu hapo nikajuwa kumbe ilikuwa ni saa saba sasa.

 

Nilielekea kule niliposikia sauti zile na kukutana na mzee mmoja na kumuelezea tukio lote. Mzee huyu akakybali kunipa msaada wa kuishi pale kkwake. Nikaishi pale kwa muda wa siku tatu kwa yule mzee nikila na kuoga bila ya tatizo lolote. Siku ya nne yule mzee akaniuliza. “mwanangu, unaishi hapa ila inabidi ujifundishe kuishi mwenyewe bila ya kunitegemea. Vip kwani mwanangu una ujuzi gani wewe?”. nikamjibu “mimi nimeishi maisha ya kifalme kama nilivyokwambia baba yangu ni mfalme hivyo maisha niloishi ni ya kisomi. Taaluma nilonayo ni masimulizi na uandishi”.

 

Yule mzee aliposikia maneno yangu akaguna kidogo kisha akasema “mwanangu, kwa ujuzi ulonao hapa ni vigumu kuweza kujitgemea. Hivyo nakushauri uanze biashara ya kukata kuni. Nitakuandalia zana na nitakufundisha pia. Kwa hakika ni kazi njema na ni ya rahisi katika eneo hili”. Basi siku ilofata yule mzee akanikabidhi shoka na panga pamoja na kata ya kubebea mizigo ya kuni.

 

Basi mzee alinichukuwa kuelekea msituni ambapo akanifundisha kazi ile na unielekeza mambo yahusuyo. Tulikata kuni siku ile na tukarudi na mizigo kila mtu na wa kwake. Mzee akanipeleka sokoni na kunelekeza matajiri wa kununua kuni zile. Siku ilofata nikaenda peke yangu, kwa kweli mwanzo kazi niliiona ngumu sana ila baada ya siku kadhaa nikaanza kuzoea.

 

Nilianza kuishi bila a kumtegemea mzee wangu yule, kwa hakika alinizoea sana na alinifanya kama mwanae. Alikuwa nabinti yake aliye mdogo alikuwa kila siku akiniambia pindi akikuwa ataniozesha. Ingawa sikua na matumaini hayo lakini nilikubwa kwa kuataka kumridhisha mzee yule. Hivyo nikawa ninatoka asubuhi kuelekea kazina na mida ya mchana ninarudi kwa ajili ya kutegea soko la mchana na wale anaotaka kupika usiku.

 

Sasa nimesha zoea kazi hata mzee aliweza kuniachia familia yake niweze kihudumia pindi alipopata safari za dharura. Ni mieze miwili na siku nane sasa toka nikutane na mzee huyu. Nilimuheshimu sana na alinipenda pia. Kwakweli heshima inapelekea kupendwa na watu. Mambo yalikuwa kama hivyo, ila siku moja kila kitu kiliharibika. Kwa hakika sikuweza kuisahau siku hii hata mara moja.

 

Ilitokea siku moja nilikwenda kukatakuni asubuhi sana na mapema. Siku hii nilikwenda mbali sana tofauti na sikuzote. Nilipokuwa ninachanja kuni ghafla nikasikia sauti kama vile shoka imepiga chini ambapo kuna shimo. Nikaacha kuchanja kuni na kuanza kufukua pale chini na nilishangaa kuona kuna mfunikowa zege. Pale nikaanza kuchimba ule mfunika hata nikaufungua na kukuta kuna ngazi ya kushuka chini. Kwa umakini nikaikamata ngazi ile na kuanzakushuka nayo kule chini na kukuta kuna jumba moja kubwa sana.

 

Nilistaajabu kuona jumba kule chini. Kwa udadisi zaidi nikataka kujua kuna nini hasa. Ikaelekea mlango mkuu wa jumba lile na kugonga mlango na kufunguliwa na wafanyakazi wa kike. Wakanipeleka mpaka kwa mkubwa wao. Kumbe jumba lile lina wananwake watupu na mkubwa wao ni mwananoke ambaye ni mtoto wa mfalme. Nilipomuona tu nilistaajabu kwa ururi ambao ameumbiwa. Kwa hakika ni mzuri na anaonekana katika mavazi ya heshima zaidi.

 

Nikamsalimia kwa upole na kurudisha salamu. Baada ya salamu nikajitambulisha kwa jna la Hamid mchanja kuni wa kijiji, binti alitabasamu na kuniacha mdomo wazi kwa mshangao.nilimuuliza kipi kimemsibu na yeye ni nani hasa. Akaanza kunielezea habari yake kama ifuatavyo;-



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-08     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 937


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Dalili za uchungu
Uchungu wa uzazi hutokana na kubana nakuachia kwa misuli hii husababishwa kufunhuka kwa mlango wa tumbo la uzazi pamoja na shingo ya kizazi na kumuongezea mama uchungu wakati wa kujifungua(during labour) Pia kubana na kuachia huanza polepole wakati wa Soma Zaidi...

TAMBUA FAIDA NA ATHARI ZA MICHEZO
POSti hii inahusu kwenye michezo na burudani.michezo ni kile kitu ambacho unakifanya kwa ajili ya kujifuraisha wewe mwenyewe.pia na watu waliokuzunguka.tukiangalia michezo anaweza kucheza mtu yeyeto yule kwa sababu michezo haina ubaguzi. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, tunajua kuwa mama yake na binti alimtorisha yule binti mbali kabisa ila kijana naye aliamua kutoroka na kumfuata binti mfalme na hatimaye akampata alipo. Soma Zaidi...

Mtihani penzini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Kifo cha mtoa burudani wa sultani
Posti hii inakwenda kukusimulia kuhusu hadithi ya kifo cha mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...

Safari ya majibu juu ya maswali mawili
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Dalili za vidonda vya tumbo
Vidonda vya tumbo no tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda,hutokea baada ya ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaitwa mucus kuharibika. Vidonda vya tumbo (peptic ulcers) imegawanyika katika ma Soma Zaidi...

WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 2
Post hii ni mwendelezo wa hadithi ambayo Kwa jina inaitwa wakati wa Kufumbuka, ni mwendelezo wa pale maria anawekwa mbele ya wazee Ili akili kwamba John sio mtoto wa Mzee maganga ila maria akikumbuka wazi kwamba John ni mtoto wa Mzee maganga anakataa kuki Soma Zaidi...

Aladini katika pango la utajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

Hadithi ya chongo wa tatu mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya aliyekatwa vidole gumba
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tatu)
Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya kijana Frank na Amisa pia na wapenzi wawili ambao ni James na Amina. Soma Zaidi...