Twahara

Twahara

FIQH 1.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Twahara

FIQH
1.TWAHARA
Twahara ni neno la kiarabu lenye maana ya usafi au unadhifu. Na neno hili kisheria ni kuondoa yale yanayomzuilia mtu kuswali ambayo ni katika hdathi na najisi, kwa kutumia maji au vinavyosimama badala ya kukosekana kwa maji kama udongo.

Kuondoa najisi ni jambo la wajibu pindi mtu anapokumbuka na akiwa na uwezo wa kufanya hivyo. Kama aliposema Allah kumwambia Mtume (s.a.s): “na nguozako uzitwaharishe” (surat muzammil: 4). Na Mtume صليالله عليه وسلم amesema “haikubaliwi swala (iliyoswaliwa ) bila ya udhu”.

Kuwa twahara tofauti na kuwa ni jambo lililohimizwa sana kwenye uislamu hata Mtume صليالله عليه وسلم akasema: “uislamu ni usafi” ila pia kuna faida nyingi sana tunazipata kwa kutekeleza jambo hili:

1.Twahara ni sharti katika kuswihi kwa sala. Hadithi iliyopokelewa kutoka kwa Mtume صليالله عليه وسلم amesema:”haikubaliwi swala ya mtu aliyehuduthi (aliyejamba) mpaka atawadhe” (Bukhari na Muslim)

2.Allah amewasifia sana watu ambao wanakuwa twahara. Amesema Allah “hakika Allah anawapenda wenye kutubia na anawapenda wenye kuwa twahara” (Surat baqara aya 222).

3.Kuwa twahara ni sababu ya kutokuadhibiwa kaburini. Ni kuwa watu ambao hawajikingi na najisi kama mkojo na hawajitwaharishi wataadhibiwa makaburini. Imesimuliwa hadithi na Ibn Abas kuwa Mtume صليالله عليه وسلم alipita kwenye makaburi mawili kisha akasema : “hakika watu hawa (waliozikwa hapa ) wanadhibiwa, na si kwa makosa makubwa bali kwa hakika huyu mmoja alikuwa hajisafishi anapokojoa.….” (Ibn Majah N Abu daud na isnad ya hadithi ni sahihi)

Aina za twahara.
Basi tambua kuwa twahara ip katika makundi makuu mawili ambayo ni:

1.twahara haqiqiya: nayo ni ni kujitwaharisha na khabathi yaani najisi na inaweza kuwa kwenye mavazi au mwili.

2.Twahara hukmiyah: nayo ni kujitwaharisha na hadathi na hii inahusiana na mwili tu na aina hii imegawanyika katika makundi matatu ambayo ni:-
A)Twahara kubwa; ambayo ni kuonga (josho la kisheria)
B)Twahara ndogo; nayo ni kutawadha yaani udhu
C)Twahara iliyo badala ya aina mbili zilizotangulia nayo ni kutayamam, yaani kujitwaharisha kwa kutumia udongo.


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2388

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kuswali swala vitani
Jinsi ya kuswali swala vitani

Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani.

Soma Zaidi...
Kujitwaharisha kutokana na najisi
Kujitwaharisha kutokana na najisi

Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi.

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mwenye hadathi kubwa.
Yaliyo haramu kwa mwenye hadathi kubwa.

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ya haramu kwa mwenye hadathi kubwa

Soma Zaidi...
Mifano na namna ya kurithisha
Mifano na namna ya kurithisha

Ugawaji wa mirathi-Mume ana nusu (1/2) = 1/2 -Mama ana sudusi.

Soma Zaidi...
Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu

Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi
Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi

Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali.

Soma Zaidi...