Udhu ni ufunguo wa Swala na ni miongoni mwa ibada zinazomtakasa Muislamu kimwili na kiroho. Mbali na kuwa sharti la baadhi ya ibada, wanazuoni wamebainisha kuwa kuna mambo mengi yanayopendeza kufanywa na mtu akiwa na udhu. Mambo hayo huongeza thawabu, humkaribisha mja kwa Allah, na humfanya awe katika hali ya twahara wakati wote.