TONGE LA MWISHO

TONGE LA MWISHO

Download kitabu Hiki Bofya hapa KWISHA KWA CHAKULA Watu waliaanza kumaliza vyakula vyao na wakaanza kufa baada ya siku kadhaa.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

TONGE LA MWISHO

pic
Download kitabu Hiki Bofya hapa

KWISHA KWA CHAKULA

Watu waliaanza kumaliza vyakula vyao na wakaanza kufa baada ya siku kadhaa. Tulianza kuwazika mpaka wenzangu wote wakaisha hata nikamzika mwenzeu wa mwisho pekeangu na kubakia mimi tu. Nikiwa na mkate mmoja tu wa ngano ulobakia nikaaza kulia na kijuta kuwa bora nisingesafiri. Nilikata tamaa na nguvu ziliniishia nikajua sasa ndo nakufa mimi. Wakati nilipokuwa nimekaa pale niliona ndege akinywa maji ya kale kajimto. Nilitamani nimuuwe ndege yule nipate chakula.

Nilianza kumvizia ndege yule na hata nikamrushia jiwe, na kwa kiwewe ndege yule akaingia kwenye lile pango ambalo kale kajimto kamepotelea. Nilimsubiri nje ya pango ili atoke lakini hakuweza kutoka hata ikafika jioni. Nikala kipande cha mkate na kubakiwa na kipande kimoja. Ilipofika asubuhi nikapata akili luwa kama yule ndege hakuweza kutoka kwenye [pango lile kutakuwa na mabo makuu mawili yanaweza kutokea, moja huenda ameliwa au ametokea nje ya pango sehemu nyingine. Hapo nikajipa matumaini kuwa mto huu utakuwa umetokea eneo jingine.

Basi nikaanza kuunganisha mabao kisha nikajilaza kifudifudi na kukusanya mali za dhahabu, almasi na mali nyinginezo za madini katika eneo lile na kulweka mabao yangu kwenye mto ule ambao ulinichukuwa na kupotea nami kwneye pango. Niliweza kupitishwa sehemu nyembembe sana ambapo niliumia sana. Nilimaliza kipande cha mkate wangu hata nikawa sina chochote. Nikawa nawaz anaweza kufa humu kabla hata sijaliona jua. Kwa njaa na mawazo na maumivu ya kugongwa nilipoteza fahamu na nisijue kinachoendelea kwenye mto ule.

Nilipokija kuzinduka nikakuta nimezungukwa na watu wengi sana na ni wakubwa zaidi. Wakawa wananiuliza mimi ni nani na nimefika vipi pale kwenye eneo lile. Kabla sijaeleza chochote kwani sikuwa na uwezo wa kusema hivyo nikaomba wanipatie chakula na maji. Nikapewa na kuanza kuridhisha tumbo langu hata nikashiba na kumshukuru Mwenyezi Mungu. Nikawaeleza habari yangu na walishangaa sana. Wakaamuwa kunipeleka kwa mfalme wao ili apate kujuwa yalonikuta.

Walinichukuwa mimi na mabao yangu yale na mali zangu na ku nipeleka kwa mfalme wao wa kisiwa hiki kiitwache Serendib. Kwa heshima na taadhima nikamsalimia mfalme na kumueleza kila kilchotokea bila hata ya kuficha. Mfalme alishangaa sana na kuniona nimezaliwa na nyota ya ajali inayoambatana na uokovu. Mfalme akamumu habari yangu iandikwe kwa maandishi ya dhahabu na iwekwe kwenye hifadhi ya kifalme kwa vizazi vijavyo.

Nilikaa pale Serendib kwa muda wa mwezi mmoja na nikamuomba ruhusa mfalme niweze kurudi nyumbani. Alikubali na kunipatia malinyingi kisha akanipatia barua ili nikampe Sultan Harun Rashid wa Baghadad. Barua ilikuwa imeeandikwa kwenye karatasi cha bluu zilizotengenezwa na ngozi ya nyok. Maadhishi yalikuwa ni ya dhahabu yaliyochovywa na mafuta ya misk. Mfalme pia alinipatia zawadi nyingi sana kwa ajili ya familia yangu na kwa ajili ya Sultani Harun Rashi. Barua ilikuwa na lengo la kuomba urafiki kati ya vuiongozi wawili hawa.

Nilisafiri kwa amani hata nikafika kwenye bandari ya Balsora na kufika nyumbani na mali mengi sana. Niliwaeleza ndugu zangu yalonikuta na safari hii nikaadidi kuwa sasa sitosafiri tena kibiashara. Siku ilofuata nikaongozana na familia yangu na kuelekea kwa Sultan kwenda mpatia barua yake. Sultani alifurahi sana na alipenda zawadi alopewa. [ia aliniuliza habari nyingi kuhusu mfalme wa Balsora na kumridhisha maswali yake. Nikaondoka na kurudi kwangu. Baada ya hapa nikaanza kutengeneza maisha yangu na sikutaka tena kusafiri majini.

Baada ya kumaliza kusimulia hadithi hii ya safari hyake ya sita Sinbad alimpatia Sinbad wa nchikavu pesa kiasi kadhaa kama fidia ya kupoteza muda wake na kumsikiliza. Watu wakatawanyika pale na akamuahidi Sinbada awahi kesho ili asikilize kilichotokea kwenye safari yake yta saba na kwa nini alivunja ahadi yake mara hii.


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aliflela1 Main: Burudani File: Download PDF Views 1137

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Kitabu Cha  hadithi ya wanawake watatu
Kitabu Cha hadithi ya wanawake watatu

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Kutokana nyani mpaka kuwa chongo
Kutokana nyani mpaka kuwa chongo

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake
Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya mke na kasuku
Hadithi ya mke na kasuku

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya mfalme na waziri wake
Hadithi ya mfalme na waziri wake

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya mzee wa tatu na mbwa wake mwekundu
Hadithi ya mzee wa tatu na mbwa wake mwekundu

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
SAFARI YA PILI YA SINBAD
SAFARI YA PILI YA SINBAD

Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA PILI YA SINBAD Basi siku ile Sinbad mbeba mizigo aliwahi haraka sana na mapema zaidi, na akamkuta Sinbad wa baharini ameshakaa na watu wake wanamsubiri kuanza hadithi.

Soma Zaidi...
HADITHI YA KISIWA CHA MAWE YANAYOLIA
HADITHI YA KISIWA CHA MAWE YANAYOLIA

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YAKISIWA CHA MAWE YANAYOLIA.

Soma Zaidi...
SAFARI YA SABA YA SINBAD
SAFARI YA SABA YA SINBAD

Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA SABA YA SINBAD Walipokusanyika siku ilofata Sinbad akawaambia kuwa kilichofanya nikavunja ahadi yangu ya kutosafiri tena ni kauli ya Sultani Nilipopunzika kwa muda wa miezi miwili nilipata habari kuwa Sultani

Soma Zaidi...
HADITHI YA MJI ULOGEUZWA MAWE
HADITHI YA MJI ULOGEUZWA MAWE

Download kitabu Hiki Bofya hapa HDITHI YA MJI ULOGEUZWA MAWE.

Soma Zaidi...