Athari na faida za kumuamini Allah katika maisha ya mwanadamu duniani na akhera

Athari za Kumuamini Mwenyezi Mungu (s.

Athari na faida za kumuamini Allah katika maisha ya mwanadamu duniani na akhera

Athari na faida za kumuamini Allah katika maisha ya mwanadamu duniani na akhera

Athari za Kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku.
Muumini wa kweli huishi katika kila kipengele cha maisha yake kwa mujibu wa taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w), na hii kama ifuatavyo;



(i)Kupata ukombozi kutokana na utumwa wa aina zote;
Huu hupatikana baada ya mtu kuwa huru na kuishi kwa kufuata taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w) pekee.
Rejea Qurโ€™an (12:39).



(ii) Mwanaadamu huwa mwadilifu katika utendaji wa maisha yake ya kila siku;
Muumini wa kweli hufanya mema na kuepuka maovu bila hata ya kusimamiwa au kuonekana na watu, kwa kujua kuwa mjuzi pekee ni Mwenyezi Mungu (s.w).
Rejea Qurโ€™an (50:16).



(iii) Humfanya mwanaadamu kuwa mpole, mvumilivu na mwenye huruma;
Mwanaadamu huwa mpole hasa kwa wenye shida na matatizo na pia kuwa na subra anapofikwa na mitihani na kujiepusha na kibri, majivuno na kujiona.
Rejea Qurโ€™an (6:165).



(iv) Humfanya mja kuwa jasiri katika kusimamia haki, uadilifu na usawa katika jamii;
Muumini wa kweli huwa shujaa katika kupambana na dhulma na ukandamizaji wa aina yeyote na kupigania haki bila kumchelea mtu yeyote.
Rejea Qurโ€™an (4:74), (5:45) na (9:111).



(v) Humfanya mja kuwa na mtazamo mpana na sahihi juu ya maisha;
Muumini wa kweli kamwe hawi na fikra na mtazamo finyu katika kuyaendea maisha yake ya kila siku kwa kujua lengo, thamani na nafasi yake juu ya maisha ya Akhera.
Rejea Qurโ€™an (15:9).



(vi) Humuwezesha mja kuwa mwenye kukinai na kutosheka;
Muumini wa kweli hutosheka na kuridhika na kile alichokadiriwa na Mwenyezi Mungu (s.w) iwe kwa kupungukiwa au kuzidishiwa, yote kwake anashukuru.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Main: Dini File: Download PDF Views 1995

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰2 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

MAANA YA Quran

Maana na majina ya Quran Maana ya Wahyi.

Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...
fadhila za sura kwenye quran

FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.

Soma Zaidi...
NGUZO ZA IMAN

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...