LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).
LAKINI UMRI WANGU MKUBWA
Baada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).
“Kwa nini nisimtake Muhammad aniowe? Inagawaje fikra hii ni mfano wa ndoto, lakini ni jambo linalowezekana. Lakini vipi? Nani atakayekubali kunifikishia ombi langu?”
Alipokuwa katika hali ile, mlango ukagongwa.
“Nani anayegonga mlango?”
“Mimi dada yako Halah.”
Bibi Khadija akamkaribisha dada yake.
“Ahlan wa sahlan, karibu ewe Halah”
Halah:
“Ahsante Khadija vipi hali zenu?”
Khadija:
“Hatujambo, ziara hii ya ghafla naona.”
Khadija:
“Bila shaka ewe dada yangu, kwani nimekuja kukujulia hali yako tu”.
Khadija:
“Kuijua hali yangu tu! Mbona unasema maneno ya kiajabu, au kuna jambo unataka kunificha?”
Halah akamtizama dada yake mtizamo wa kuchunguza, kisha akamwambia:
“Abadan, hakuna la kukuficha isipokuwa mchana wa leo ulinichukuwa usingizi nikakuota unatembea mfano wa mtu aliyepotea katika njia ya kiza na nyuma yako sauti inakwambia: “Nenda mbele, nenda mbele”. Nikaona bora nije kukujulia hali yako, ingawaje sijuwi ndoto hiyo tafsiri yake nini”.
Bibi Khadija (Radhiya Llahuu anha) akatabasamu kidogo kisha akasema:
“Kusema kweli mimi siku hizi ninaishi ndani ya mawazo mengi sana.”
Halah:
“Unawaza juu ya nini na wewe upo katika neema kubwa kama hii?”
Khadija:
“Muhammad, ewe dada yangu. Nafikiri juu ya sifa zake na utukufu wake ambao hajapata kuufikia hata mmoja katika watu wa kabila la Kikureshi.”
Halah:
“Na nini mwisho wa fikra hizo?”
Khadija:
“Nataka aniowe”.
Halah:
“Basi muombe akuowe”.
Bibi Khadija akamjibu kwa uoga:
“Naogopa asije akanikataa, kwani yeye ni kijana anayeheshimika kupita vijana wote”
Halah:
“Na wewe pia dada yangu ni mtu mtukufu unayeheshimika na watu wote”.
Khadija:
“Lakini umri wangu mkubwa unaokaribia miaka arubaini, na nishaolewa mara mbili, wakati yeye bado ni kijana mwenye umri wa miaka ishirini na mitano na bado hajapata kuowa. Vipi Muhammad atakubali kumuowa mwanamke aliye na umri sawa na mama yake aliyekwisha olewa mara mbili na ana watoto?”
Halah akasema:
“Nani aliyekujulisha na Muhammad mara ya mwanzo hata ukaweza kumpa mali yako aifanyie biashara?”
Khadija:
“Rafiki yangu mmoja anayeitwa Nafisa”.
Halah:
“Basi Nafisa huyo huyo ndiye atakayeweza kukufikishia ombi lako hilo”.
Kisha Halah akamuaga dada yake na kuondoka
ANAOLEWA NA MUHAMMAD
Ziara ya Hala ilikuwa mfano wa ufunguo wa kheri katika nafsi ya bibi Khadija (Radhiya Llahu anha), kwani siku ya pili yake Nafisa alipokuja kumtembelea bibi Khadija, akamhadithia juu ya mazungumzo yaliyopita baina yake na baina ya dada yake Halah, na Nafisa akakubali kuchukuwa jukumu la kulifikisha ombi hilo kwa Muhammad (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Alipoondoka, Nafisa alielekea moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Abu Talib alipokuwa akiishi Muhammad (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na alipomuona akamwambia:
“Ewe Muhammad, wewe una umri wa miaka ishirini na tano na mpaka sasa bado hujaowa.”
Muhammad (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akashangazwa sana na maneno hayo, akamuuliza:
“Kipi kilichokufanya ujishughulishe na jambo hili ewe Nafisa?
Nafisa:
“Bibi anayeheshimika anataka umuowe, nini rai yako?”
Muhammad (Swallah Llahu alayhi wa sallam):
“Bibi gani huyo?”
Nafisa:
“Bibi huyo ni Khadija binti Khuwaylid, na wewe unamuelewa vizuri juu ya heshima yake na utukufu wake na sifa zake zote njema”.
Muhammad (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akasema:
“Naam, hakika yeye ni mtu anayeheshimika, lakini mimi sina mali hata niweze kumuowa.”
Nafisa;
“Yeye hana haja ya mahari, kwani unajuwa vizuri kuwa yeye hana shida ya mali na anao utajiri mkubwa”.
Muhammad:
“Mimi utajiri haunishughulishi, kwani mali inakuja na kuondoka, na Khadija pia ni mwanamke mzuri wa umbo na tabia na mwenendo, lakini niache nimshauri ami yangu kwanza juu ya jambo hili”.
Ami yake akamwambia:
“Ewe Muhammad, hii ni bahati iliyokujia kutoka mbinguni. Naapa kuwa Khadija ni mwanamke aliyetakasika kupita wote katika Makka na mwenye akili na uwezo wa kupima mambo kupita wote, na mwenye hekima kupita wote na anayetokana na ukoo bora kupita wote. Wangapi wenye mali na jaha walitaka kumuoa akawakataa, na leo anakutaka wewe wakati huna mali yoyote, hii ni bahati kubwa.
Kubali ewe mwana wa ndugu yangu, kwani asingekutaka isipokuwa amekuwekea heshima kubwa sana”.
Muhammad (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akakubali, na bibi Khadija akafanya arusi kubwa sana iliyohudhuriwa na watu wengi, na wanyama wengi sana wakachinjwa siku hiyo na kila muhitaji alifaidika.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w sehemu ya 4. Hapa utajifunza kuhusu historia ya kuangamiza kwa jeshi la tembo.
Soma Zaidi...Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua.
Soma Zaidi...KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s.
Soma Zaidi...Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Sahaba wa kwanz akufariki akiwa shahidi, alifariki kwa sababu ya mateso aliyoyapata kutoka kwa Makafiri wa ki Quraysh
Soma Zaidi...