8.
8.1. Ukuaji na Uendeshaji wa Dola ya Kiislamu Wakati wa Makhalifa Wanne Waongofu
Makhalifa wanne wa Mtume (s.a.w) waongofu walioendeleza Dola ya Kiislmu ni;
1. Abu Bakar Sswiddiq (r.a) kutoka mwaka 11 A.H – 13 A.H.
2. Umar Ibn Khattab (r.a) kutoka mwaka 13 A.H – 24 A.H.
3. Uthman bin Affan (r.a) kutoka mwaka 24 A.H – 36 A.H
4. Ali bin Abu Twalib (r.a) kutoka mwaka 36 A.H – 41 A.H
Uchaguzi wa Makhalifa wanne waongofu
1. Kuchaguliwa Abu Bakar Sswiddiq (r.a) kuwa Khalifa
- Mtume (s.a.w) mpaka anatawafu, hakuusia nani awe khalifa baada yake.
- Abu Bakar (r.a) alipendekezwa na Umar Ibn Khattab (r.a), na Answar wengi walikubali pendekezo hilo kutokana na sifa zifuatazo:
i. Sifa zilizopelekea Abu Bakar (r.a) kuchaguliwa kuwa kiongozi wa Dola ya Kiislamu ni pamoja na;
1. Ucha – Mungu
2. Ujuzi wa kutosha wa Qur’an na Sunnah
3. Tabia njema
4. Siha (afya) nzuri
ii. Alisilimu akiwa mtu mzima na alikuwa karibu sana na Mtume (s.a.w)
kuliko sahaba yeyote yule.
Rejea Qur’an (9:40)
iii. Mtume (s.a.w) alimteua kuongoza swala kwa niaba yake alipokuwa mgonjwa.
iv. Alikuwa mwenye msimamo, maamuzi, ikhlas na uoni mpana kwa kufuata ipasavyo nyayo na mwenendo wa Mtume (s.a.w)
2. Kuchaguliwa Umar Ibn Khattab (r.a) kuwa Khalifa baada ya Abu Bakar (r.a)
- Abu Bakar (r.a) alipokaribia kutawafu aliitisha shura na kumpendekeza
Umar Ibn Khattab (r.a) kuwa Khalifa baada yake kutokana na sifa zake.
- Walikuwepo wajumbe wengi miongoni mwao ni pamoja na;
1. Umar Ibn Khattab (r.a) o Uthman bin Affan (r.a) o Ali bin Abi Twalib (r.a) o Zaid bin Thabit (r.a)
2. Abdul – Rahman bin Auf (r.a)
3. Muadh bin Jabal
4. Ubay bin Ka’ab (r.a) na wengineo katika Muhajirina na Answaar.
- Baada ya shura, wajumbe wote walikubali pendekezo la Abu Bakar (r.a)
kuwa Umar bin Khattab (r.a) achukue nafasi ya kuongoza Dola ya Kiislamu.
3. Kuchaguliwa Uthman bin Affan (r.a) kuwa Khalifa
- Umar (r.a) alipendekekeza watu sita wenye sifa za kuongoza Dola ya
Kiislamu ambao ni;
1. Uthman bin Affan (r.a)
2. Ali bin Abu Twalib (r.a)
3. Saad bin Waqqas (r.a)
4. Talha (r.a)
5. Zubair bin Awwam (r.a) na
6. Abdul – Rahman bin Auf (r.a)
- Siku ya tatu baada ya kutawafu Umar Ibn Khattab (r.a), Uthman bin Affan (r.a) alichaguliwa na jopo la masahaba baada ya Abdul – Rahman bin Auf (r.a) na wengineo kujitoa.
- Siku ya nne, Uthman bin Affan (r.a) alitangazwa rasmi na kupewa bai’at
kuwa ndiye kiongozi wa Dola ya Kiislamu.
4. Kuchaguliwa Ali bin Abi Talib (r.a) kuwa Khalifa
- Baada ya miaka sita tu ya uongozi wa Ali bin Abi Talib (r.a), fitna ilizushwa na Myahudi aliyesilimu kwa uongo, Abdallah bin Sabaa.
- Waislamu waligawanyika makundi mawili, moja linakubaliana na uongozi wa Ali bin Abi Talib (r.a) na jingine kupingana nao.
- Sababu za kugawanyika ni kudai kuwa Khalifa Ali (r.a) halipizi kisasi kwa wauaji wa Uthman bin Affan (r.a), makundi hayo yalikuwa ni;
i. Wafuasi wa Uthman – (Uthmanis);
- Wao walitaka Dola iwaadhibu wauaji wa Uthman bin Affan (r.a).
ii. Marafiki wa Ali – (Shian – Ali)
- Ndilo kundi la watu wa mji wa Kufa na Misr lililomuua Khalifa
Uthman (r.a)
iii. Mashibah
- Ni kundi la waislamu waliokwenda Jihad wakati Khalifa Uthman
(r.a) anauawa, hawakuwaunga mkono ‘Uthmanis wala Shian – Ali’
iv. Ahli – Sunnah Wal- Jama’ah
- Lilikuwa ndilo kundi lenye masahaba wengi katika Dola yote ya
Kiislamu.
- Takriban uongozi wote wa Khalifa Ali (r.a) ulikumbwa na migogoro iliyopelekea kuuawa kwake.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Kutokana na histoira ya Nabii Sulaiman (a.
Soma Zaidi...Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Kuanzishwa kwa Dola ya Kiislamu Madinah.
Soma Zaidi...Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w, sehemu ya 5. Hapa utajifunza kuhusu kuzaliwa kwa Mtume.
Soma Zaidi...