Siku za kupata mimba

Nitakujulisha siku ya kupata mimba na sifa zake, na namna ya kuweza kuitafuta

Siku za kupata mimba

SIKU ZA KUPATA MIMBA
Kwa wale wanaohangaika kutafuta ujauzito makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakwenda kukujuza siku yako mujarabu ambayo utatapa ujauzito. Pia nitakujuza sifa za siku za kupata mimba. Unajuwa wanawake wanatofautiana sana katika mifumo yao ya uzazi, simaanishi maumbile, namaanisha hali zao. Watu wengi wanaelewa kuwa mwanamke anaweza kupata mimba siku zote. Hapa hii sio sahihi kabisa. Ukweli ni kuwa kuna siku maalumu na ni chache. Kitaalamu siku hizi hufahamika kama faertile window.



Siku ya kupata ujauzito utaweza kuijuwa kwanza kuangalia mambo kadhaa nitakayoyatajahapo chini. Kabla ya kuyajuwa mabo hayo haklikisha kuwa unakula lishe bora na inayoshawishi kutafuta mtoto kweli kama unatafuta mtoto. Kwa wanaume wale vyakula vya kuongeza mbegu za kiume kama karangga, korosho, kunywa maji mengi na vyakula vingine, wasiliana nasi hapo chini nikueleze. Pia hakikisha wewe na mwenza mnakula vyakula vya kuongeza hamu ya tendo lando kwaingi. Hakikisha mwili ni msafi na kila mmoja amejiandaa vyema kumpokea mwenza. Sasa nakwenda kukufundisha siku za kupata mimba.



1.Kutambuwa siku za kupata mimba kwa mahesabu.
Kwanza hakikisha unaujuwa tarehe yako ukiwa ni mwanmke, na kama ni mwanaume itambuwe vyema tarehe ya mwenzio. Tambua byema mzunguruko wake wa hedhi unakwenda siku ngapi. Ukitambua vitu hivyo sasa twende pamoja. Wataalamu wanaeleza kuwa mwaname anaweza kubeba mimba siku 12 mpaka 14 kabla ya kuingia hedhi yake. Pia wataalamu wanatueleza kuwa yai la mbegu ya mwanaume inaweza kuwa hai ndani ya siku tatu mbaka 5 na yai la mwanamke linaweza kukaa masaa 12 mpaka 24 . ila sanasana ni siku 3, yaani mbegu iliyoingia leo inaweza kurutubisha yai siku tatu zijazo. Hivyo tyujaalie mwaname ana mrunguruko wa hedhi wa siku 28. tutafanya hivi:-



Mfano wa kwanza mwenye siku 28
A.28 - 12 = 16 (ongeza moja iwe 17, kufidia yai la mama)
B.16 - 02 = 14
C.14 - 3 = 11 (tunapunguza 3 nyuma kufidia mbegu ya maba)
Hivyo mwanamke huyu siku zake za kupata mimba ni kati ya siku ya 11 mpaka 17 toka siku ya kwanza aingie hedhi.



Mfano wa pili mwenye siku 35
A.35 - 12 = 23 (ongeza 1 iwe 24)
B.23 - 02 = 21
C.21 - 03 = 18
Hivyo mwenye mzunguruko wa siki 35 siku zake hatari kupata mimba ni kati ya siku ya 18 mpaka 24 toka siku ya kwanza kuona hedhi.



Mfano wa tatu mwenye siku 21
A.21 - 12 = 9 (ongeza 1 iwe 10)
B.9 - 2 = 7
C.7 - 3 = 4
Mwanamke huyu anaweza kubeba ujauzito punde tu baada ya kumaliza hedhi mpaka siku ya 10



Unaweza kutumia mifano hii kitafuta skuku yako ya kupata mimba. Wanawake wanatofautiana sana siku zao. Kuna ambao ni 21, kuna ambao ni 35. ila kwa hali ya kawaida siku za hedhi ni kati ya 21 mpaka 35. ikizidi hapo ama kuwa chini ya hapo kutakuwa na shida kwenye mfumo wa homoni. Kama upo katika kutafuta ujauzito hakikisha unashiriki ngono katika siku zote hizo ama unaweza kuruka ruka ila hakikisha unaanza na siku ya kwanza, kisha unaweza kuacha moja na kushiriki inayofata.



2.Sifa za siku za kupata mimba.
Baada ya kujuwa kuitafuta siku ya kupata mimba sasa napenda ujuwe ssifa za siku hiyo. Sasa hata kama unaijuwa kwa mahesabu ukweli ni kuwa unaweza pia kuikosa kwani sio maalumu. Sasa hapa nitakurahisishia kazi kwa kukutajia sifa za siku hizo za kupata mimba.



1.Siku ya kupata mimba ina sifa hii, kwanza joto la mwili linakuwa kubwa tofauti na siku zilizotangulia na siku zijazo. Tambuwa kuwa hapa mwili utakuwa na joto ila haliusiani na ugionjwa wowote ama mambo mengine. Kwa mfano kuchelewa kulala, misongo ya mawazo maradhi na homa kwa pamoja hupelekea joto la mwili kupata. Joto tunalolizungumzia hapa halisababishwi na sababu yeyeote katika hizi.



2.Uteute wa ukeni utakuwa mwingi kulinganisha na siku zilizopita. Uteute huu husaidia kati akuzisafirisha mbegu za kiume kwenda kutungisha mimba. Uteute kuu ni mlaini na unateleza sana. Mwanamke anaweza kuuiona baada ya kuingiza kidole ndani sana kwenye shingo ya uzazi.



3.Siku hii mwanamke atakuwa na hamu sana ya kushiriki tendo la ndoa kuliko siku zilizopita. Hii ni kutokana na miamsho iliyosababishwa na homoni ambazo zinaandaa mwili kwa ajili ya ujauzito.



Sifa hizi huweza kupotea baada ya kupata ujauzito ama muda wa kubeba mimba ukiisha. Mabadiliko hayo pia huweza kuathiriwa na mabo mengine kama matumizi ya uzazi wa mpango hasa wa kutumia sindano. Je utakuwa na maoni, maswali ama mapendekezo?. wasiliana nasi kwa hapo chini





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 3081

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 web hosting    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Changamoto za ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu changamoto za ujauzito na dalili zake endelevu

Soma Zaidi...
Sababu za kupata hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja, mara nyingi kuna Watu ambao huwa wanalalamika kwa sababu ya kupata hedhi za mara kwa mara kwa mwezi mmoja.

Soma Zaidi...
Sababu za mwanamke kukosa hamu ya tendo la ndoa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mwanamke kukosa tendo la ndoa, ni sababu ambazo uwakuta wanawake wengi unakuta mama yuko kwenye ndoa ila hana hata hamu ya lile tendo la ndoa hali ambayo umfanya mwanamke kuona kitendo cha tendo la ndoa ni unyanyasaji au

Soma Zaidi...
Kutokwa maji yan seminal swhemu za siri kwa mwanamke nidalili ya ugojwa gan?

Kutokwa Majimaji sehemu za siri kwa mwanamke sio jambo la kushangaza na kuhisivunaumwa. Majimajivhaya ndio huboresha afya ya uzazi kwa kusafisha na kulinda via vya uzazi. Lakini majimajivhaya yakiwa mengi, ama yanawasha ama yanaharufu haa ndipo kwenye tat

Soma Zaidi...
Madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu,ni madhara ambayo utokea kwa mtu anayetumia madawa ya kupunguza maumivu.

Soma Zaidi...
ZIJUWE DALILI KUU 5 ZA MIMBA CHANGA

Dalili za mimba, na m,imba changa

Soma Zaidi...
Sababu za kuongezeka uzito wa wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuongezeka uzito kwa wajawazito, Mara nyingi Mama akibeba mimba uongezeka uzito kutoka wiki ya Kwanza mpaka wiki ya mwisho ya kujifungua.

Soma Zaidi...
TATIZO LA KUVIMBA KWA USO NA MIGUU KWA WAJAWAZITO

KUVIMBA VYA MIGUU KWA WAJAWAZITO Kuvimba kwa miguu ni hali inayowapara wengi katika wajawazito.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisukari wakati wa ujauzito.

Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito.

Soma Zaidi...
mkewang alikuwa anasumbuliwa na tumbo kama siku tatu lika tuliya saivi analalamika kiuno na mgongo vina muuma nini tatizo tockt

Maumivu ya tumbo nakiuno kwa mwanamke yanahitaji uangalizi wakina. Kwani kuna sababu nyingi ambazo zinawezakuwa ni chanzo.

Soma Zaidi...