picha

Safari ya saba ya Sinbad

Posti hii inakwenda kukuletea muendelezo wa safari saba za Sinbad

SAFARI YA SABA YA SINBAD

Walipokusanyika siku ilofata Sinbad akawaambia kuwa kilichofanya nikavunja ahadi yangu ya kutosafiri tena ni kauli ya Sultani Nilipopunzika kwa muda wa miezi miwili nilipata habari kuwa Sultani ananiita. Nilipokwenda alinieleza kuwa anataka nipeleke barua yake kwa mfalme wa Serendib ya kumjibu kuwa ameridhika na urafiki. Nikamueleza kuwa nimeweka ahadi ya kutousafiri tena kutokana na yalonikuta. Sultani alisisitiza sana mimikwenda na akaniambia kuwa mimi ndie mtu nafaa zaidi kwani mfalme wa Serendib ananijua.

 

Basi nilikubaliana na amri ya Sultani na ikaandaliwa safari ya kifalme na jahazi lililo madhubuti zaidi na la kisasa liliandaliwa na Sultani mwenyewe. Baada ya maandalizi kukamilika mali nyingi kama zawadi ziliandaliwa kwa ajili ya mfalme. Safari ilianza salama na tuliwasili Serendib kwa amani muda wa jioni. Mfalme wa Serendib alinipokea mwenyewe na kunikumbatia na kunivika joho lenye ukosi ulochovywa kwenye dhahabu nyekundu.

 

Mfalme alilidhika na zawadi zile na alifurahi sana kwa kuniona. Mfalme alifurahi zaidi kuona barua ile imejibiwa kama atakavyo. Mafalme wa Serendib akaniozesha mtoto wake kama takrima ya udugu wetu. Ndoa ilifanyika salama na baada ya kukaa pale kwa muda wa mwezi mmoja nilipewa ruhusa ya kuondoka mimi na mkewangu na zawadi nyingi kwa ajili yangu na kwa ajili ya Sultani wa Baghadad.

 

Mfalme mwenyewe aliandaa jahazi na kulimadhiubutisha na safari iliandaliwa kifalme kwani ndani mlikuwa na mkwe na mtoto wa mfalme. Tuliwasili Baghadadi baada ya mwe ndo wa siku kumi na tano. Na Sultani alitupokea kwa heshima zote na kukutana na binti wa Mfalme wa Serendib. Sultani alitufanyia sherehekubwa kama ile ilofanyika wakati wa harusi kule Sererndib. Kwa hakika ilikuwa ni furaha kubwa zaidi. Na huu ndio mwisho wa safari zangu saba za majini.

 

Mpaka sasa nina wake watatu mmoja nilishamuoa nilipokuwa kijana na mwingine ni yule nilookoka nae kwenye makaburi na wa tati ni huyu. Na nimebahatika kuoa mabinti wawili wa wafalme. Kisha Sinbad akawaomba wakezake wote waje ili Sinbad wa nchikavu awaone, kisha akamkutaninisha na yule mzee wa bostani alokuja nae Sinbad. Kisha Sinbad wa baharini akamuuliza Sinbad wa nchikavu “je! Unafikiri sistahiki kupata maisha haya kwa sasa?, je! Kuna yeyote unayemfahamu amepata taabu kama mimi?” majibu ya maswali haya alibakia nayo Sinbad moyoni kwa mshangao.

 

Baada ya pale Sinbad wa majini akamwambia Sinbad mbeba mizigo kuwa sasa tumeshakkuwa marafiki. Kwa siku saba hizi umekuwa kama ni ndugu yangu sasa. Naomba uje na familia yako tukae hapa kama ndugu. Sindab mbeba mizigo akakubaliana na ombi lile na waliishi na Sinbad kwa muda mrefu sana. Waliishi kama kaka na ndogoake. Hata alipofariki Ndugu wa Sinbad wakamchagua kijana Sinbad mbeba mizigo awe ndiye msimamizi mkuu wa mali za mzee Sinbad. Kwa hakika maisha yao yalikuwa mazuri sana na mahusiano yao na ya Sultani wa Baghadad na mfalme wa Serendib hayakukoma.

 

Mpaka kufikia hapa Schehrazade akamaliza hadithi hii ya Sinbad, na tayari miezi mingi ilishapita bila ya kuuliwa na Sultani Shahariyar. Baada ya hapa Sultani Shahariyar akauliza “hatujajua kilichomkuta mtoto wa Sinbad aliyemzaa kutoka kwa ‘Aisha mtoto wa mfalme” Dinarzade akamwambia “ni hadithi ya kusisimua sana” na kama utaniongeza muda zaidi wa kuishi nitakusimulia hadithi nzuri zaidi ya yalomkuta mtoto wa Sinbad.

 

 

NA HUU NDIO MWISHO WA HADITHI ZA ALIF LELA U LELA KITABU CHA KWANZA. KUPATA MUENDELEZO WA HADITHI DOWNLOAD APP YETU YA ALIF LELA U LELA KITABU CHA PILI.

 

KUPATA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NAMI KWA

EMAIL: HYPERLINK "mailto:rajabumahe@gmail.com" rajabumahe@gmail.com

PHONE:+255712939055

YOOTUBE:www.youtube.com/c/Rajabu Athuman. 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021-11-09 Topic: Aliflela1 Main: Burudani File: Download PDF Views 1957

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 web hosting    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

NDOTO YA MGONJWA MTOTO WA MFALME

Download kitabu Hiki Bofya hapa NDOTO YA MGONJWA BINTI WA MFALME.

Soma Zaidi...
HADITHI YA BINT WA PILI MWIMBA MASHAIRI MWENYE MAKOVU

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA BINTI WA PILI MWIMBA MASHAIRI MWENYE MAKOVU.

Soma Zaidi...
HADITHI YA MWEN YEKUTABIRIWA MTOTO WA TAJIRI

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITI YA MWENYE KUTABIRIWA MTOTO WA TAJIRI Kwanza tambua ewe ndugu yangu kuwa mimi ni mtoto wa tajiri mkubwa sana katika nchi yetu hii.

Soma Zaidi...
HADITHI YA TABIBU NA MFALME

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA TABIBU WA MFALME Katika nchi ya Zouman iliyopo maeneo ya uajemi alikuwepo mfalme mkubwa sana.

Soma Zaidi...
Malipo ya wema ni wema

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya chongo wa kwanza mtoto wa mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya mji uliogeuzwa mawe

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya chongo wa tatu mtoto wa mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
SAFARI YA SABA YA SINBAD

Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA SABA YA SINBAD Walipokusanyika siku ilofata Sinbad akawaambia kuwa kilichofanya nikavunja ahadi yangu ya kutosafiri tena ni kauli ya Sultani Nilipopunzika kwa muda wa miezi miwili nilipata habari kuwa Sultani

Soma Zaidi...
HADITHI YA SAMAKI WA RANGI NNE

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA SAMAKI WA RANGI NNE.

Soma Zaidi...