image

ADABU ZA KUSOMA QURAN

Adabu wakati wa kusoma quran 1.

ADABU ZA KUSOMA QURAN

imageimage Adabu wakati wa kusoma quran
1.kuwa na ikhlas. Hapa jinachokusudiwa ni kuwa na nia iliyo takata kuwa unasoma kwa ajili ya Allah na si vinginevyo. Kama ilivyokuwa ibada zote anatakiwa afanyiwe Allah kama Mtume alivyosea katika hadithi sahihi aliyoipokea Bukhari, Muslim kwa mtume amesema “hakika si vinginevyo amali (hulipwa) kwa (kuzingatia) nia...” . Hivyo msomaji asifanye ili watu wamsikie eti yeye ndo bigwa ila asome kwa kutaraji radhi za Allah.

2.Kuwa na khushui, na kuleta mazingatio. Mwenye kusoma qurani ajitahidi ahudhurishe moyo wake wote kwenye lile analolifanya nalo ni kusoma qurani. Pia alete mazingatio kama anaelewa nini qurani inazungumza. Amesema Ibraahim Khawas kuwa: dawa ya nyoyo ni mambo matano ambayo nui: kusoma Qurani kwa mazingatio, kufunga, kusimama usiku na kukaa na watu wema.

3.Kulia wakati wa kusma Qurani. Mwenye kusoma qurani huenda ikamfanya alie, hivi ni vizuri sana na ni sifa ya watu wema. Hata mtume alikuwa naposomewa qurani alikuwa akilia.

4.Kusoma kwa sauti. Mzomaji wa qurani anatakiwa atoe sauti yake yaani asome kwa sauti kwa namna ambayo hatawaudhi watu walio karibu nae kama mtu aliolala, anayeswali ama waliokuwepo kwenye mazungumzo yake.

5.Kusoma kwa sauti nzuri. Msomaji wa qurani anatakiwa ajitahidi kuwa na sauti nzuri. Zipo riwaya nyingi ambazo zinaonesha msisitizo juu ya kuremba sauti. Mapaka mtume akasema “mtu amabye hasomi qurani vizuri sio katika sisi.” katika mapokezi mengina ya Bukhari, muslim na Abuu Dawd ni kuwa Allah amemuamrisha mtume kusoma qurani kwa sauti nzuri.

6.Tajweed. Maana ya tajweed ni kuisoma qurani kwa hukumu zake. Qurani ina hukumu zake katika kusoma. Kila herufi inatakiwa itamkwe kwa namna ileile inayotakiwa. Kila herufi ipewe haki yake katika idh-hari, ikh-fai, id-ghami, mada, ghunnah na ntingineso nyingi.

7.Kudhihirisha maana. Mwenye kusoma qurani ajitahidi kudhihirisha maana wakati anaposoma. Mtu anatakiwa ajuwe kitu ambacho kinazungumziwa katika aya anayoisoma.

8.Kusoma kwa kupumzika. Kwenye kusoma qurani natakiwa asisome mfululizo ila awe ana viu vya kupumzika. Amesimulia Ummu salama kuwa alikuwa mtume anapumzika kwenye usomaji wake alikuwa akisoma AL-HAMDU LILLAHI RABIL-ALAMIIN kisha hupumzika kisha anasoma AR-RAHMAANIR-RAHIIM kisha hupumzika, kisha husoma MALIKI YAUMIDIIN (amepokea Tirmidh).

9.Kuchunga hukumu za waqfu. Waqfu unaweza kusema ni vituo vya kupumzikia au kutokupumzika au kuunga maneno wakati wa kusoma qurani. Kuna ambavyo inajuzu kuunganisha (صلي), au kujuzu kusimama (قلي), au kujuzu kusimama ila kwa ufupi (ج), au vya lazima kusimama (ه) au ambavyo haitakiwi kusimama (لا).

10.Kutokusoma harakaharaka (mbiombio). Basi mwenye kusoma Qurani ajitahidi kusoma katika mpangilio unaopendeza. Sio mbiombio kiasi kwamba inaweza kuwa rahisi kufanya makosa ya kiusomaji.

11.Inapendeza pia kutwaharisha kinywa kwa kupiga mswaki kabla ya kusoma qurani.

12.Kusoma kwenye msahafu. Hili ni jambo ambalo linapendeza kwa wale wanaotaka kuhifadhi qurani. Tofauti na kusikiliza ikisomwa wawe wanaangalia maandishi ya qurani hasa kwenye msahafu.

13.Kumuomba Allah unaposoma qurani. Amesema Mtume “mwenye kusoma qurani basi na amuombe Allah kwayo, kwani hakika watakuja watu watasoma qurani na wataomba kwayo watu” (amepokea tirmidh)

14.Msomji awe ni twahara. Hili ni jambo linalipendeza sana kwa anayesoma qurani awe na tahara. halikadhalika mtu mwenye janaba haruhusiwi kusoma qurani ila kama ataisoma kama dua. Kwa mfano akisoka adhkari za kulala ambazo zina qurani ndani yake.

15.Kuanza kusoma qurani kwa kujikinga na shetani yaani kusema “A’UDHU BILLAHI MINAS-SHAYTWANIR-RAJIIM”

16.Kuomba dua unapofika sehemu za heri. Amepokea hadithi Muslimu kuwa Abuu ‘Abdallah Hudhaifiya amesimulia kuwa alikuwa Mtume “… Anaposoma aya yenye tasbih huleta tasbih, na anaposoma aya yenye maombi(dua) huomba (dua), anaposoma aya yenye t’awdh (kutakahifadha) hutaka hifadha”

17.Kujikinga na shari anaposoma aya za shari. Yaani anaposoma aya ambazo zinataja adhabu za makafiri na watu waovu humuomba Allah amuepushe kuwa katika kundi hilo.

18.Kleta sijdat tilawa unapofika sehemu za kusujudi.


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 706


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

Aina za Madd far-iy
Mada zipo katika makundi mawili ambayo ni madda far-iy na mdada twab-iy. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MADD
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

DARSA ZA QURAN
Soma Zaidi...

Dai kuwa Muhammad Alitunga Qur-an ili Ajinufaishe Kiuchumi
Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MADD YAANI KUVUTA HERUFI KWENYE USOMAJI WA QURAN
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Maswali yanayohusu quran
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

Muhammad hakufundishwa quran na padri Bahira
Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al qadir
Asbab nuzul surat al qadi. Hii ni sura ya 97 katika mpangilio wa mashaf. Surat al qadir imeteremshwa Madina na ina aya 5. Soma Zaidi...

Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum
SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s. Soma Zaidi...

Sababu za kshuka surat al Asr
Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo… Soma Zaidi...