ADABU ZA KUSOMA QURAN

Adabu wakati wa kusoma quran 1.

ADABU ZA KUSOMA QURAN

imageimage Adabu wakati wa kusoma quran
1.kuwa na ikhlas. Hapa jinachokusudiwa ni kuwa na nia iliyo takata kuwa unasoma kwa ajili ya Allah na si vinginevyo. Kama ilivyokuwa ibada zote anatakiwa afanyiwe Allah kama Mtume alivyosea katika hadithi sahihi aliyoipokea Bukhari, Muslim kwa mtume amesema “hakika si vinginevyo amali (hulipwa) kwa (kuzingatia) nia...” . Hivyo msomaji asifanye ili watu wamsikie eti yeye ndo bigwa ila asome kwa kutaraji radhi za Allah.

2.Kuwa na khushui, na kuleta mazingatio. Mwenye kusoma qurani ajitahidi ahudhurishe moyo wake wote kwenye lile analolifanya nalo ni kusoma qurani. Pia alete mazingatio kama anaelewa nini qurani inazungumza. Amesema Ibraahim Khawas kuwa: dawa ya nyoyo ni mambo matano ambayo nui: kusoma Qurani kwa mazingatio, kufunga, kusimama usiku na kukaa na watu wema.

3.Kulia wakati wa kusma Qurani. Mwenye kusoma qurani huenda ikamfanya alie, hivi ni vizuri sana na ni sifa ya watu wema. Hata mtume alikuwa naposomewa qurani alikuwa akilia.

4.Kusoma kwa sauti. Mzomaji wa qurani anatakiwa atoe sauti yake yaani asome kwa sauti kwa namna ambayo hatawaudhi watu walio karibu nae kama mtu aliolala, anayeswali ama waliokuwepo kwenye mazungumzo yake.

5.Kusoma kwa sauti nzuri. Msomaji wa qurani anatakiwa ajitahidi kuwa na sauti nzuri. Zipo riwaya nyingi ambazo zinaonesha msisitizo juu ya kuremba sauti. Mapaka mtume akasema “mtu amabye hasomi qurani vizuri sio katika sisi.” katika mapokezi mengina ya Bukhari, muslim na Abuu Dawd ni kuwa Allah amemuamrisha mtume kusoma qurani kwa sauti nzuri.

6.Tajweed. Maana ya tajweed ni kuisoma qurani kwa hukumu zake. Qurani ina hukumu zake katika kusoma. Kila herufi inatakiwa itamkwe kwa namna ileile inayotakiwa. Kila herufi ipewe haki yake katika idh-hari, ikh-fai, id-ghami, mada, ghunnah na ntingineso nyingi.

7.Kudhihirisha maana. Mwenye kusoma qurani ajitahidi kudhihirisha maana wakati anaposoma. Mtu anatakiwa ajuwe kitu ambacho kinazungumziwa katika aya anayoisoma.

8.Kusoma kwa kupumzika. Kwenye kusoma qurani natakiwa asisome mfululizo ila awe ana viu vya kupumzika. Amesimulia Ummu salama kuwa alikuwa mtume anapumzika kwenye usomaji wake alikuwa akisoma AL-HAMDU LILLAHI RABIL-ALAMIIN kisha hupumzika kisha anasoma AR-RAHMAANIR-RAHIIM kisha hupumzika, kisha husoma MALIKI YAUMIDIIN (amepokea Tirmidh).

9.Kuchunga hukumu za waqfu. Waqfu unaweza kusema ni vituo vya kupumzikia au kutokupumzika au kuunga maneno wakati wa kusoma qurani. Kuna ambavyo inajuzu kuunganisha (صلي), au kujuzu kusimama (قلي), au kujuzu kusimama ila kwa ufupi (ج), au vya lazima kusimama (ه) au ambavyo haitakiwi kusimama (لا).

10.Kutokusoma harakaharaka (mbiombio). Basi mwenye kusoma Qurani ajitahidi kusoma katika mpangilio unaopendeza. Sio mbiombio kiasi kwamba inaweza kuwa rahisi kufanya makosa ya kiusomaji.

11.Inapendeza pia kutwaharisha kinywa kwa kupiga mswaki kabla ya kusoma qurani.

12.Kusoma kwenye msahafu. Hili ni jambo ambalo linapendeza kwa wale wanaotaka kuhifadhi qurani. Tofauti na kusikiliza ikisomwa wawe wanaangalia maandishi ya qurani hasa kwenye msahafu.

13.Kumuomba Allah unaposoma qurani. Amesema Mtume “mwenye kusoma qurani basi na amuombe Allah kwayo, kwani hakika watakuja watu watasoma qurani na wataomba kwayo watu” (amepokea tirmidh)

14.Msomji awe ni twahara. Hili ni jambo linalipendeza sana kwa anayesoma qurani awe na tahara. halikadhalika mtu mwenye janaba haruhusiwi kusoma qurani ila kama ataisoma kama dua. Kwa mfano akisoka adhkari za kulala ambazo zina qurani ndani yake.

15.Kuanza kusoma qurani kwa kujikinga na shetani yaani kusema “A’UDHU BILLAHI MINAS-SHAYTWANIR-RAJIIM”

16.Kuomba dua unapofika sehemu za heri. Amepokea hadithi Muslimu kuwa Abuu ‘Abdallah Hudhaifiya amesimulia kuwa alikuwa Mtume “… Anaposoma aya yenye tasbih huleta tasbih, na anaposoma aya yenye maombi(dua) huomba (dua), anaposoma aya yenye t’awdh (kutakahifadha) hutaka hifadha”

17.Kujikinga na shari anaposoma aya za shari. Yaani anaposoma aya ambazo zinataja adhabu za makafiri na watu waovu humuomba Allah amuepushe kuwa katika kundi hilo.

18.Kleta sijdat tilawa unapofika sehemu za kusujudi.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2621

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Sababu za kushuka kwa Surat al-Kawthar na fadhila zake

SURATUL-KAUTHAR Imeteremshwa maka, na sura hii imeshuka kwa sababu al-aAs ibn Waail.

Soma Zaidi...
Aasbab Nuzul surat Ash sharh: sababu za kushuka alam nashrah (surat Ash sharh)

Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh.

Soma Zaidi...
quran na sayansi

2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio.

Soma Zaidi...
Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum

SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s.

Soma Zaidi...
namna quran inavyogawanya mirathi na wanaorithi pamoja na mafungu yao

Qur-an inavyogawa MirathiMgawanyo wa mirathi umebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo:Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Mwanamume apate sawa na sehemu ya wanawake wawili.

Soma Zaidi...
As-Sab nuzul

Sababu za kuteremshwa baadhi ya sura Katika darsa hii tutaangalia sababu za kushuka kwa aya na sura ndani ya quran.

Soma Zaidi...
Quran Tafsiri kwa Kiswahili

Tafsiri ya quran kw akiswahili, imeandikw ana Shekh Ali Muhsin al-Barwani

Soma Zaidi...