Adabu za kusikiliza quran

ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1.

Adabu za kusikiliza quran

imageimage ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI
1.kutafuta msomaji mwenye sauti mzuri. Inapendeza mtu mwenye kusikiliza qurani asikilize kwa yule mwenye sauti ambayo ataipenda. Jambo hili litampa hamu ya kusikiliza qurani. Hata mtume alikuwa na wasomaji wake maalumu wa kumsomea qurani. Amesimulia Jabir kuwa mtume amesema “hakika mtu mwenye sauti nzuri anaposima qurani ni yule ambaye pindi mnapomsikia anasoma qurani mnamdhania kuwa anamuogopa Allah. (amepokea ibn majah).

2.Kuleta mazingatio pamoja na kufikiri kwa kina maana. Inatakiwa nayesikiliza qurani sio tu atosheke na sauti lakini anatakiwa awe na mazingatio juu ya kile ambacho kinasomwa.

3.Mwenye kusikiliza qurani awe ni mzuri wa kusikiliza na mwenye kunyamaza. Amesema Allah kuwa “na pindi inaposomwa qurani isikilizeni na nyamazeni ili mrehemewe. (surat al-a’araaf 204)

4.Kulia na kuwaidhika na kinachozungumzwa. Kama ilivyo kwa msomaji hata msikilizaji pia ni vema akalia kwa kuwaidhika na qurani. Amesema Allah “na pindi wanaposikia yale yaliyoteremswa kwa Mtume utayaona macho yao yanabubujika machozikutokana na yale walioyajua katika haki” (surat maaidah 83)

5.Kuleta khushui, unyenyekevu na kutukuza kitabu cha Allah. Mwenye kusikiliza qurani ahakikishe kuwa analeta khushui na unyenyekevu, awe na utulivu huku akijuwa ukubwa wa kitabu cha Allah.

6.Kusujudi pindi unaposikia aya ya kusujudi. Sijida hii ni sunnah na mbele za maimamu wa fikh wapo wanaiita ni swala kama ilivyo swala ya jeneza. Hivyo haipasi mtu kusujudi akiwa hana udhu. Atasema mwenye kusujudi sijida hii “SAJADA WAJHI LILLADHII KHALAQANIY WASHAQA SAM’AHU, WABASWARAHU, BIHAWLIHI, WAQUWATIHI” amsesimulia ‘Aisha. Aya hizi za sijida zipo 15 katika qurani ambazo ni aya ya mwisho ya surat al-araf, aya ya 15 ya surat rad, aya ya 50 ya surat nahli, aya ya 109 ya surat israa, aya ya 58 ya surat maryam, aya ya 18 ya surat haj, aya ya 77 ya ryrat haj, aya ya 60 ya surat furqan, aya ya 26 ya surat naml, aya ya 15 ya surat sajda, aya ya 38 ya surat fusilat, aya ya 62 ya surat najmi, aya ya 21 ya surat inshiqaq, aya ya 19 ya surat ‘alaq.


                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1676

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

quran na sayansi

QURANI KATIKA ZAMA ZA SAYANSI NA TEKNOLOJIAAsalaalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii

Soma Zaidi...
Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa

Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat An-Nasr (idhaa jaa)

SURATUN-NASR Sura hii imeteremka wakati Mtume (s.

Soma Zaidi...
ASBAB-NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN

ASBAB NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN Quran imeteremka kwa muda wa miaka 23 kidogokido.

Soma Zaidi...
Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA

SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( مْ).

Soma Zaidi...