Adabu za kusikiliza quran

ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1.

Adabu za kusikiliza quran

imageimage ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI
1.kutafuta msomaji mwenye sauti mzuri. Inapendeza mtu mwenye kusikiliza qurani asikilize kwa yule mwenye sauti ambayo ataipenda. Jambo hili litampa hamu ya kusikiliza qurani. Hata mtume alikuwa na wasomaji wake maalumu wa kumsomea qurani. Amesimulia Jabir kuwa mtume amesema “hakika mtu mwenye sauti nzuri anaposima qurani ni yule ambaye pindi mnapomsikia anasoma qurani mnamdhania kuwa anamuogopa Allah. (amepokea ibn majah).

2.Kuleta mazingatio pamoja na kufikiri kwa kina maana. Inatakiwa nayesikiliza qurani sio tu atosheke na sauti lakini anatakiwa awe na mazingatio juu ya kile ambacho kinasomwa.

3.Mwenye kusikiliza qurani awe ni mzuri wa kusikiliza na mwenye kunyamaza. Amesema Allah kuwa “na pindi inaposomwa qurani isikilizeni na nyamazeni ili mrehemewe. (surat al-a’araaf 204)

4.Kulia na kuwaidhika na kinachozungumzwa. Kama ilivyo kwa msomaji hata msikilizaji pia ni vema akalia kwa kuwaidhika na qurani. Amesema Allah “na pindi wanaposikia yale yaliyoteremswa kwa Mtume utayaona macho yao yanabubujika machozikutokana na yale walioyajua katika haki” (surat maaidah 83)

5.Kuleta khushui, unyenyekevu na kutukuza kitabu cha Allah. Mwenye kusikiliza qurani ahakikishe kuwa analeta khushui na unyenyekevu, awe na utulivu huku akijuwa ukubwa wa kitabu cha Allah.

6.Kusujudi pindi unaposikia aya ya kusujudi. Sijida hii ni sunnah na mbele za maimamu wa fikh wapo wanaiita ni swala kama ilivyo swala ya jeneza. Hivyo haipasi mtu kusujudi akiwa hana udhu. Atasema mwenye kusujudi sijida hii “SAJADA WAJHI LILLADHII KHALAQANIY WASHAQA SAM’AHU, WABASWARAHU, BIHAWLIHI, WAQUWATIHI” amsesimulia ‘Aisha. Aya hizi za sijida zipo 15 katika qurani ambazo ni aya ya mwisho ya surat al-araf, aya ya 15 ya surat rad, aya ya 50 ya surat nahli, aya ya 109 ya surat israa, aya ya 58 ya surat maryam, aya ya 18 ya surat haj, aya ya 77 ya ryrat haj, aya ya 60 ya surat furqan, aya ya 26 ya surat naml, aya ya 15 ya surat sajda, aya ya 38 ya surat fusilat, aya ya 62 ya surat najmi, aya ya 21 ya surat inshiqaq, aya ya 19 ya surat ‘alaq.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2671

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

As-Sab nuzul

Sababu za kuteremshwa baadhi ya sura Katika darsa hii tutaangalia sababu za kushuka kwa aya na sura ndani ya quran.

Soma Zaidi...
fadhila za sura kwenye quran

FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.

Soma Zaidi...
HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za Quran kuwa mwongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kukusanywa na kuhifadhiwa kwa quran

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq

Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq.

Soma Zaidi...
Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.

Soma Zaidi...