Zijuwe Suna zinazofungamana na swaumu na funga ya ramadhani

Zijuwe Suna zinazofungamana na swaumu na funga ya ramadhani

Sunnah zinazoambatana na funga ya Ramadhani



Katika Mwezi wa Ramadhani kuna mambo kadhaa aliyoyafanya Mtume (s.a.w) na kutusisitiza nasi tuyafanye. Matendo haya ya Sunnah ambayo hurutubisha funga zetu na kutupelekea kufikia lengo la funga kwa ufanisi zaidi ni pamoja na:



(i) Kula na kuchelewesha Daku
Daku ni chakula kinacholiwa usiku wa manane kwa ajili ya kujiandaa kufunga siku inayofuatia. Kula daku ni sunnah iliyokokotezwa kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:


Anas (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: ... Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa alfajir katika weusi wa usiku .. (2:187)



(ii) Kufuturu Mapema
Wakati wa kufuturu ni mara tu linapokuchwa jua kama tunavyofahamishwa katika Hadith:
Umar (r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah amesema: Usiku unapoingia na mchana ukitoweka, na jua likitua, mtu aliyefunga atafungua.(Bukhari na Muslim).



Ni sunnah iliyokokotezwa kufanya haraka kufuturu mara tu linapokuchwa jua na kabla ya kuswali swala ya Magharibi kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:



Sahl (r.a) amesimulia kwamba Mtume wa Allah amesema: Watu w ataendelea kunawiri (kufanikiwa) pindi w atakuw a wanaharakisha kufuturu. (Bukhari na Muslim).



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Allah (s.w) amesema: Mpendwa zaidi kwangu kati ya waja wangu ni yule ambaye mw epesi kuliko w ote katika kufuturu. (Tirmidh).



Pia ni Sunnah kufuturu kwa Tende au kwa maji kwani tunajifunza katika Hadith kuwa Mtume (s.a.w) alifanya hivyo na akatuagizia tufanye h ivyo:
Anas (r.a) ameeleza kuwa mtume (s.a.w) alikuwa akifungua kwa Tende mbivu kabla ya kuswali (Magharibi), kama hizi hazikuwepo alifungua kw a Tende kavu, na kam a hizi hazikuw epo alikunyw a m afunda macha che y a m aji. (Tirm idh n a A bu Da ud).



Salman bin Amir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Mmoja wenu atakapokuwa anafuturu, na afuturu kwa Tende kwa sababu ni baraka, kama hakupata Tende, na afuturu kwa maji, kwa sababu yametakasika (ni twahara). (Ibn Majah).



Vile vile ni sunnah wakati wa kufuturu kusoma dua ifuatayo: (Allahumma laka swumtu wa’alaariz-qika aftwar-tu)
“Ewe Mola! Nimefunga kwa ajili yako, na kwa riziki yako ninafuturu”. (Abu Daud).



Ni sunnah vile vile mtu kuzidisha dua anapokuwa katika swaumu kwani Mtume (s.a.w) amesema:
“Watu watatu dua yao hairejeshwi - aliyefunga mpaka afungue. Imamu muadilifu na mtu aliyedhulumiwa. ” (Tirmidh).



(iii)Kuzidisha Ukarimu



Pamoja na kuwa siku zote tumekokotezwa kuwakirimu na kuwasaidia wenzetu wenye shida mbalimbali, katika mwezi wa Ramadhani tunatakiwa tuzidishe. Mtume (s.a.w) alikuwa karimu zaidi katika mwezi wa Ramadhani, kuliko alivyokuwa katika miezi mingine kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:



Amesimulia Ibn Abbas (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa ni mkarimu sana kuliko watu wote na alikuwa akizid is ha ukarimu wake katika mwezi wa Ramadhani wakati ambao Jibril (a.s) alikuwa akimjia. Jibril (a.s) alikuwa akikutana naye kila usiku wa Ramadhani mpaka mwisho wa mwezi. Mtume (s.a.w) alikuwa akisoma Qur-an mbele ya Jibril, na Jibril alipokutana naye alikuwa mwema (mkarimu) zaidi kuliko upepo wa kusi (wa mvua) (Bukhari).



Kufuturisha aliyefunga kumeahidiwa malipo makubwa kama tunavyojifunza katika hadith ifuatayo:
Zaidi bin Khalid(r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Atakayemfuturisha mtu aliyefunga, au atakayempa askari wa Allah zana za vita, kwake kuna malipo sawa na malipo ya mwenye kufunga au ya mpiganaji (bila wao kupunguziwa). (Baihaqi).



(iv)Kuzidisha kusoma Qur’an
Kusoma Qur’an kumesisitizwa nyakati zote kwani Qur’an ndio mwongozo pekee wa maisha wanaotakiwa Waumini wa kweli waufuate hatua kwa hatua katika kila kipengele cha maisha yao ya kila siku. Lakini, katika mwezi wa Ramadhani, ambamo Qur-an imeanza kushuka, tumesisitizwa kuzidisha kusoma Qur’an katika swala na nje ya swala angalau tuumalize msahafu mzima katika mwezi huu. katika Hadith tumejifunza kuwa, Mtume (s.a.w) alikuwa akisoma Qur-an mbele ya Jibril kwa mwezi mzima.Kuhusu kushuka Qur-an katika mwezi wa Ramadhani tunafahamishwa katika aya ifuatayo:



“Ni mw ezi wa Ram adhani ambamo imeteremshwa Qur-an ili iw e uongozi kwa watu na hoja zilizo wazi za uongozi na upambanuzi .. (2:185).



Ili Qur’an iwe mwongozo na kipambanuzi cha haki na batili, hatuna budi kuisoma kwa mazingatio na kwa hiyo ni muhimu kujua tafsiri ya yale tuyasomayo. Tukumbuke kuwa kusoma Qur’an bila ya mazingatio ni kama kuiangukia kwa uziwi na upofu, sifa ambayo waumini wa kweli wanatakiwa wajiepushe nayo. Kwani Allah (s.w) anatufahamisha kuwa miongoni mwa waja wake watakaofuzu ni pamoja:


“Na wale ambao wanapokumbushwa aya za Mola wao hawaziangukii kwa uziwi na upofu” (25:73).



(v)Kusimamisha Swala ya Usiku ya Tarawehe
Swala ya Tarawehe ambayo tumeshajifunza habari zake, ni miongoni mwa Sunnah zilizokokotezwa katika mwezi wa Ramadhani.



(vi)Kuutafuta usiku wa Lailatul-Qadr
Lailatul-Qadr au Usiku Wenye Cheo na Baraka ni usiku mmoja katika mwezi wa Ramadhani. Ni katika usiku huu Qur’an tukufu ilianza kushushwa kwa Mtume (s.a.w) kwa mara ya kwanza alipokuwa katika pango la mlima Hiraa (Jabal Hiraa). Aya za kwanza kumshukia Mtume (s.a.w) ni aya tano za mwanzo wa suratul-Alaq, sura ya 96 katika msahafu. Kuhusu kushuka Qur’an katika usiku huu tunafahamishwa katika Qur’an yenyewe:


“Kw a yakini Tumeteremsha (Qur-an) katika usiku uliobarikiw a. Bila shaka Sisi ni Waonyaji. ” (44:3).


“Hakika tumeiteremsha (Qur-an) katika Lailatul-Qadr (Usiku Wenye heshima kubwa)” (97:1).






                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3047

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya

Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali.

Soma Zaidi...
Ufafanuzi kuhudu mgogoro wa mwezi ni muda gani mtu aanze kufunga.

Je inapoonekana sehemu moja tufunge duania nzima ama tufunge kwa kuangalia mwandamo katika maenro tunayoishi.

Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala?

Je kusimamisha swala kuna maana gani kwenye uislamu?

Soma Zaidi...
Utaratibu wa kuzika maiti ya kiislamu, hatua kwa hatua

Kuzika Kuzika ni kitendo cha nne cha faradh tunacho lazimika kumfanyia ndugu yetu aliyetutangulia kufa.

Soma Zaidi...
Funga za Sunnah na namna ya kuzitekeleza

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu

Maana: ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa baina ya mume na mke mbele ya mashahidi wawili kwa kuzingatia sheria ya Kiislamu.

Soma Zaidi...
Hadhi na Haki za Mwanamke katika jamii mbalimbali hapo zamani

Utangulizi:Uislamu unamuelekeza mwanaadamu namna nzuri ya kuendesha maisha yake katika kila kipengele cha maisha akiwa binafsi, katika familia na katika jamii.

Soma Zaidi...