image

HADITHI YA KINYOZI MSIRI WA MFALME

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA KINYOZI MSIRI WA MFALME.

HADITHI YA KINYOZI MSIRI WA MFALME


Download kitabu Hiki Bofya hapa

HADITHI YA KINYOZI MSIRI WA MFALME.

Hapo zamani za kale katika nchi moja kulikuwepo na mfalme aliyependa kufuga nywele. Mfalme huyu alikuwa akinyowa nywele zake mara nne kwa mwaka. Mfalme huyu alipenda kuvaa kilemba kichwani kama ilivyo kawaida katika tamaduni za kiislamu. Watu wengi walipenda uvaaji wa mfalme wao na yeye alilijuwa hili kwa muda mrefu. Kumbe mfalme alikuwa anasiri kubwa katika uvaaji ule. Mfalme alikuwa akinyolewa na kinyozi maalumu. Ilipita masiku na miaka mingi hata yule kinyozi wa mfalme akafariki. Ilibidi mfalme atangaze kumtafuta kinyozi mwingine. Uchunguzi ulifanyika kumtafuta kinyozi muadilifu na mwenye maadili. Zaidi ya sifa hizi mfalme alitaka kinyozi mwenye sifa ya kutunza siri. Sifa hii aliitaka mfalme kwa kuwa kuna siri kubwa kwenye kichwa chake. Basi alipatikana kinyozi mmoja kijana mwenye familia ya watoto wanne. Alikuwa ana maadili mazuri na ni muadilifu pia.

Ilitokea siku moja mfalme akataka kunyolewa. Akamuita kinyozi wake na kumwambia “kwa mara ya kwanza ndo unakiona kichwa changu, utakachokiona kwenye kichwa changu iwe siri yako mpaka utakapoingia kaburini”. Kinyozi akaapa mbele ya mfalme kuwa katu hataizungumza siri ile kwa yeyote. Kinyozi kufunguwa kilemba cha mfalme alishikwa na mshangao kkubwa baada kuona siri kubwa katika kichwa cha mfalme. Kinyozi akajuwa kumbe hii ndio sababu ya mfalme kuvaa kilemba na kufuga nywele.

Basi kinyozi yule alikaa na siri ile kwa siku nyingi sana. Alithubutu hata kukimbia nchi kwa kuogopa kutoa siri ya mfalme. Hali iliendelea kama hivyo anamnyoa kinyozi na anaenelea kutunza siri ya mfalme. Kama ujuavyo siri ikikaa sana kwenye moyo utadhani moyo unataka kutumbuka. Kinyozi akawaza hii siri ya mfalme siwezi kuotoa nitafanya nini sana. “ningejua kama mfalme ana pembe katu nisingekubali kukifunua kichwa cha mfalme”. Ni maneno ya kinyozi.

Basi siku moja akatoka na chepe lake na jembe kwenda porini. Kufika kule akachimba shimo kubwa mpaka kiunoni. Baada ya hapo akainama na kuanza kuimba “mfalme anapembe, mfalme anapembe”. Aliimba hivi kwa muda mpaka alipoona moyo wake umetulia na umepoa kwa kuiweka siri ya mfalme kwa muda. Basi baada ya hapo akafukia shimo lake na akaondoka kurudi nyumbani. Haukupita muda mrefu shimo like likaota majani na pakaota mti mkubwa sana.

Ni miaka 15 sasa imepita toka mti ule uote sasa mti ule ukabakia na siri ile aloiacha kinyozi miaka 15 iliyopita. Mti ule ulipofikia kutoa maua ukawa upepo ukaja unarudia ule mwimbo wa alouacha kinyozi miaka 15 ilopita. Hivyo ukaja upepo mti unaimba “mfalme ana peembe mfalme anapembe, waaa waaa waaa”. Ikatokea siku moja wawindaji wakapita karibu na mti ule wakastaajabu kusikia wimbo wa ajabu unaozungumza kuwa mfalme ana pembe.

Basi habari zikaanza kusambaa kwa kasi sana mpaka ikamfikia kinyozi. Watu wakawa wanafunga safari kwenda kuuangalia mti uanoimba kuwa mfalme ana pembe. Habari zilisambaa mpaka zikamfikia mfalme. Mafalme akatoka na msafara wake nae akashuhudie mti unaotoa siri yake ya pembe kichwani. Alishangaa sana, ilibidi siku ilofata aitishe mkutano mkubwa kwa kila atakaetaka kuhudhuria kwenye eneo lile lenye mti ule.

Basi watu walikusanyika sana eneo lile, watoto, wazee na vijana walimwaika eneo lile la tukio. Baada ya muda watu walipokusanyika akasimama na kuanza kuhutubia, kisha akavua kilembe chake watu wote wakashuhudia pembe kichwani mwake. Kisha akasema “nimeamini hakuna siri”. Na huu ndio mwisho wa hadithi ya kinyozi msiri wa mfalme. Basi Amina na Sadie walifurahi sana na wakamruhusu kijana aenelee kubakia pale.

Basi pale ndani chakula kikapikwa na watu wakawa wanakula na kunya na kufurahi. Mashairi yaliimbwa na furaha zaidi. Wakatowa pombe wakanywa na wakaendelea kufurahi pale ndani. Nyakati za swala pia ziliwapita palelpale walipokaa. Mapaka wanakuja kutambua ni jioni na kigiza kinakaribia kuingia. Zubeida akamwambia kijana “amka uende zako, muda wa kutengana na wewe umekaribia”. Kijana akaanza kujitetea tena kuwa amelewa sana hivyo hataweza kufika kwake. Kama watamruhusu alale pale mpaka kesho ataondoka na kurudi kwake.


                   



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 324


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

HADITHI YA MZEE WA TATU NA MBWA
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MZEE WA TATU NA MBWA WAKE MWEKUNDU Kama nilivyotangulia kusema , huyu ni mkewangu wa ndoa tulioishi pamoja kwa muda wa miaka zaidi ya kuni na tano sasa. Soma Zaidi...

HADITHI YA BINTI WA KWANZA NA MBWA
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA BINTI WA KWANZA NA MBWA. Soma Zaidi...

HADITHI YA MVUVI NA JINI
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MVUVI NA JINI Hapao zamani kulikuwepo na mvuvi aliyekuwa masikini wenye watoto watatu na mke mmoja. Soma Zaidi...

MALIPO YA WEMA NI WEMA
Download kitabu Hiki Bofya hapa MALIPO YA WEMA NI WEMA Basi baada ya kupita kwa muda Zubeidaha akapewa chai na chakula safi na akawekwa kwenye kiti kilicho kizuri na akaambiwa msubiri atakuja sasa hivi. Soma Zaidi...

Safari ya sita ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukuletea muendelezo wa safari za Sinbad Soma Zaidi...

Hadithi ya chongo wa kwanza mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

SAFARI YA MAJIBU JUU YA MASWALI MAWILI
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA MAJIBU JUU YA MASWALI MAWILI. Soma Zaidi...

Ndani ya pango la makaburi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Safari ya tatu ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Kuingia kwa wageni
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

HADITHI ILIYOSIMULIWA NA MLEVI MBELE YA SULTANI
Soma Zaidi...

SAFARI YA TANO YA SINBAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA TANO YA SINBAD Baada ya watu kukusanyika siku ilofata sinbad akaanza kusimulia stori ya safari yake ya tano. Soma Zaidi...