Hizi ndizo aina tatu za Hija

Hizi ndizo aina tatu za Hija

Aina za Hija



Kuna aina tatu za Hija ambazo kila mwenye kuhiji ana uhuru wa kuchagua mojawapo kulingana na uwezo wake wa kukidhi masharti ya kila aina. Aina hizi ni
(i) Ifraad,
(ii) Qiran na
(iii) Tamattu kama zinavyoelezewa katika hadith ifuatayo:



Amesimulia Aysha (r.a): 'Tulitoka na Mtume wa Allah (s.a.w) (kwenda Makka) katika Hija ya Mtume ya kuaga. Miongoni mwetu tulivaa Ihram kw a n ia y a kufany a `Umra tu (al-Tama ttu) w engine kw a Hija n a `Umra pamoja (al-Qiran) na kw a w engine kw a Hija tu (al-Ifraad). Mtume w a Allah (s.a.w) alivaa Ihram kwa nia ya Hija tu. Kwa hiyo kwa yule aliye vaa Ihram kwa Hija tu au kwa Hija na `Umra pamoja, hakutoka katika Ihram mpaka siku ya kuchinja (kutoa muhanga yaani siku ya mwezi 10 Dhul-Hija). (Bukhari).



(i)Ifraad: Ni aina ya Hija ambapo, 'Hajj' anavaa Ihram kwa nia ya kufanya Hija tu bila ya 'Umra' na ataanza kuitikia mwito wa Allah (s.a.w ) kwa:(Labbaika lhajji ) yaani 'Nimeitika kwa Hija.' Hajj hatavua Ihram yake mpaka amalize matendo yote ya Hija yanayomlazimu kuwa katika Ihram. Haji huruhusiwa kuvua Ihram na kutoka kwenye masharti yake baada ya kutupa mawe kwenye mnara na kunyoa au kupunguza nywele siku ya mwezi 10 Dhul-Hija. Kwa yule aliyechagua aina hii ya Hija halazimiki kuchinja siku ya mwezi 10 Dhul-Hija.



(ii)Qiran: Ni aina ya Hija ambapo Haji huvaa Ihram kwa nia ya kufanya Hija na 'Umra pamoja na katika talbiya ataanza kutikia mwito wa Allah kwa: (labbaika lhaji wa Umra) - yaani 'Nimeitika kwa Hija na 'Umra'.Hajj katika aina hii ya Hija hatavua Ihram mpaka baada ya kuchinja na kufanya Tawaful-Ifadha (tawafu ya nguzo) siku ya mwezi 10 Dhul-Hija.



Aina hii ya Hija inafanywa na wale wanaokuja Makka na wanyama. Katika Hija yake ya kuaga, baada ya kumaliza ibada ya 'Umra, Mtume (s.a.w) aliwaamrisha watu wote wavue Ihra m ila kw a w ale w a liokuja n a w any ama.


(iii) Tamattu: Katika aina hii ya Hija, Haji anapofika katika Miiqaat yake huvaa Ihram kwa nia ya kufanya 'Umra tu na ataitikia mwito wa (Labbaika liumra) - yaani 'Naitikia kwa 'Umra'. Baada ya kumaliza 'Umra atanyoa au kupunguza nywele na kuvua Ihram na kuwa huru na miiko yote ya Ihram. Atavaa tena Ihram kwa nia ya Hija mnamo mwezi 8 Dhul-Hija, na atabakia na Ihram mpaka amalize Hija ya mwezi 10 Dhul-Hija kama ilivyo katika aina nyingine za Hija. Haji analazimika kuchinja siku ya mwezi 10 Dhul-hija.



Katika aina hizi tatu za Hija, At-Tamattu ndio aina bora zaidi na yenye nafuu kubwa kwa wale wanaotoka mbali wasioweza kuja na wanyama, ama kwa wakazi wa Makka au majirani wa Makka ambao wana uwezo wa kwenda na wanyama, Hija iliyo bora kwao ni hii ya Al-Qiran. Lakini wenye kuhiji Hija ya Tamattu wanalazimika kununua mnyama na kumchinja siku ya mwezi 10 Dhul-Hija kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:


'... Na mtakapokuwa kwenye salama, basi mwenye kujistarehesha kwa kufanya `Umra kisha ndio akahiji, basi achinje mnyama aliyesahilika (mbuzi au kondoo).Na asiyepata, afunge siku tatu katika Hija na siku saba atakaporudi (kw ake); hizi ni kumi kamili. Hayo ni kwa ajili ya yule ambaye watu wake hawako karibu na msikiti Mtakatifu wa Makka. Na mcheni Mwenyezi Mungu na jueni ya kuwa Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu. ' (2:196).




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 279


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

sura ya 11
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Kafara ya mwenye kuvunja masharti ya ihram
Soma Zaidi...

surat al mauun
SURATUL-MAM'UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat.. Soma Zaidi...

Maadili na malezi ya jamii
Soma Zaidi...

Misingi na Maadili Katika Uislamu
5. Soma Zaidi...

KWA NINI DIRISHA MOJA?
KWA NINI DIRISHA MOJA? Soma Zaidi...

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa
Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

mafunzo ya TAWHID, maarifa na imani ya dini ya kiislamu
YALIYOMO1. Soma Zaidi...

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama
Soma Zaidi...

Nini maana ya asaba katika mirathi ya kiislamu
Soma Zaidi...

Taratibu na namna ya kutafuta mchumba na sifa za mchumba
Soma Zaidi...

TANZU ZA HADITHI
Tanzu za Hadith(1) Tanzu ya UsahihiKulingana na kiwango cha usahihi wa Hadith, Hadith zimegawanywa katika makundi makuu manne:(a) Sahihi'(b) Hasan/Nzuri. Soma Zaidi...