Simulizi za Hadithi EP 6 Part 21: Kinyozi mwenyewe

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 21: Kinyozi mwenyewe

Muendelezo....

HADITHI YA KINYOZI YEYE MWENYEWE

 

 

 

Mimi si mtu wa maneno mengi kama kijana anavyonidhania. Hata hivyo nipo tofauti sana na kaka zangu kwani mimi ndiye mtoto wa mwisho.. nitakusimulieni kisa kimoja hapa ndipo mtagundua kuwa mimi si mtu wa maneno mengi. Siku moja nilipokuwa sina kitu cha kukila na kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi sikuweza kwenda kukopa. Niliweza kusikia wepesi wa tumbo langu kwa njaa, hata nikathubutu kufunga kipande cha kanga tumboni. Sikujuwa ni kwa nini siku ile nilikuwa na njaa sana. Niliamini huenda ikawa ni majaribu yamenifikia. Mingurumo ya tumbo ilizidi kusumbua.

 

 

Basi katika pirika zangu nikakutana na vijana 10 wapo kwenye dau. Kwa mawazo yangu nikadhani wanakwenda kusherehekea. Na hii ilikuwa ni kawaida kwa vijana wakikusanyika eneo hili wanakwenda upande wa pili wa mto kufurahia na kula na kunywa. Mawazo ya njaa yalikuja karibu zaidi hata ikawa chakula kama kipo mbele yangu. Nikaanza kupata harufu ya paja la kuku lililokaangwa na kukaushwa vyema. Chapati za mayai zilizofunika samaki vyema. Harufu ya juisi nikaanza kuipata kwa mbaali wakati nakodolea macho paja la kuku.

 

 

Kwa njaa zangu na pupa ndipo nikakimbilia bilauri ya juisi na kuanguka. Loo! Nimevunja bilauri ya watu. Ghafla nikashituka kutoka kwenye dimbwi la mawazo. Nikawahi kwenye dau na mimi kuingia. Bila hata ya kuuliza zaidi kilichowakuta na wapi wanakwenda. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi sikuweza kuuliza sana. Nahodha akang’oa dau na kuanza kutokomea mtoni. Nilianza kushangaa kumbe vijana wote 10 waliomo mule wamefungwa minyororo, na walikuwa chini ya uangalizi wa askari. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi niliendelea kuwa kimya.

 

 

Tulipofika ng’ambu ya pili ya mto tulipokelewa na kundi kubwa la askari na kupelekwa kwa kadhi. Sikuzungumza kitu na wala sikujitetea kwa lolote. Ni kwa sababu mimi si mtu wa maneno mengi. Tulipofika kwa kadhi wale mabwana kumbe walikuwa na kosa na mauwaji na hivyo kadhi akaamuriu vijana wote 10 wakatwe vichwa vyao mara moja. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi niliendelea kukaa kimya none hatma ya uwepo wangu pale. Basi askari akawachukuwa wote vijana 10 na kwenda kukata vichwa vyao.

 

 

Baada ya muda kidogo askari akaja mbele ya kadhi na kutamka kuwa kazi imekwisha, yaani ameshakata vichwa vyao. Kadhi akamuuliza mbona umechukuwa 9 na huyu wa 10 umemuacha hapa. Askari akajibu hapana mkuu nimechukuwa wote 10. kadhi hakuamini hata akaenda kuhesabu vichwa. Loo! Ni kweli vichwa vilikamilika 10. hapa kadhi akawa na furushi la maswali kichwani mwake. Furushi lote akataka kunitundika mimi. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi niliendelea kunyamaza. Kadhi akaja akiwa amefura kw ahasira na mawazo.

 

 

Alipokaa vyema akaagiza aletewe maji kwenye chombo. Kadha alipoletewa maji alikuywa na kutawadha. Alifanya hivi ili kupunguza hasira, ili asijefanya maamuzi yasiyo ya haki. Kisha kadhi akaniuliza haya wewe ni nanai na imekuwaje akuajumlishwa kwenye kundi hili la watu wabaya? Basi sasa sina budi nikaanza kumueleza Kadhi namna nilivyofika pale. Kadhi alishangaa sana kuona vile hivyo akanieleza kuwa ni kwa nini hukuzungumza toka mwanzo. Nikamueleza kuwa mimi si mtu wa maneno mengi. Nikaendelea “usidhani kuwa mimi ni mtu wa maneno mengi, mimi ni tofauti sana na kaka zangu.

 

 

Kwani kaka yangu wa kwanza ni kichaa na ameupata ukichaa kutokana na yaliyomkuta na maneno mengi yake. Ili uamini kuwa mimi si mtu wa maneno mengi, nitakuhadithia yaliyowapata kaka zangu wote kutokana na maneno yao mengi. Baada ya kuzungumza hivi kinyozi akaanza kuhadithia yaliyotokea kwa kaka wake wa kwanza:

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 279

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 4: Simulizi ya chongo wa kwanza mtoto wa Mfalme
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 4: Simulizi ya chongo wa kwanza mtoto wa Mfalme

Tusikilizie simulizii inahusu chongo wa kwanza wa mtoto wa mfalme iliyopo ndani ya kitabu cha kwanza cha Hadithi za HALIF LELA U LELA.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 12: Hadithi ya mfalme alikuwa kwenye kisima
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 12: Hadithi ya mfalme alikuwa kwenye kisima

Wapendwa tuendelee kuoata stori nzuri na za kusisimua kutoka katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 10: Hadithi ya Ndoto ya binti mgonjwa wa mfalme
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 10: Hadithi ya Ndoto ya binti mgonjwa wa mfalme

Skmulizi hii ipo ndani ya kitabu cha kwanza kwenye hadithi za HALIF LELA U LELA......

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 6: Sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 6: Sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad

Muendelezo wa sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 9: Hadithi ya binti wa ndotoni.
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 9: Hadithi ya binti wa ndotoni.

Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...