Home Afya Shule ICT Burudani Dini Maktaba Maswali Madrasa Apps Blog Legacy Login

MTIHANI PENZINI


image


Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani


MTIHANI PENZINI

Sikuwa na wasiwasi maana niliamini kuwa nitafanikiwa tu. Siku ile nilioga na kuvaa ngua safi na kuvaa viatu vikubwa vya kuchomeka. Nikatoka kuelekea tulipoahidiana. Nilipofika pale nikakutana na kundi la vijakazi wa kike. Mmoja wao akaniuliza ndiye wewe mgeni, wasiri? Nikamjibu ndio. Hapo wakaniambia niingie kwenye moja ya boksi la mbao kisha likafungwa vyema. Niliweza kujihisi kama nipo kwenye jeneza vile. Wakafunganya na mizigo yao mingine na tukaondoak zetu.

 

Walipofika getini kwnyw jumba la mfalme mabawabu (walinzi wa geti) wakataka kuchunguza kilichomo. Wale wajakazi wakasema kuwa wamebeba nguo za mke wa mfalme. Walinzi wakawaruhusu kupita. Walipofika geti la pili, wakaulizwa tena wakazungumza vilevile. Waliporuhusiwa kupita ghafla mfalme akatokea. Akasema nataka nichunguze mwenyewe vitu vinavyokwenda kwa mkewangu. Hapo nikajua sasa ndio mwisho wangu. Hapo nikaanza kuhisi mkojo unauma. Tumbo likanza kunguruma na woga ukanijaa. Nikaanza kushahadia naa kutubu madhambi yangu.

 

Mfalme akawaambia watue mizigo, na wafungue boksi mojamoja. Kwa mkono wake mfalme akaanza kufungua kila boksi na anapojiridhisha hufunga. Ndipo akafika kwenye boksi ambalo nimo. Alipotaka kufungua mjakazi mmoja akamwambia, “mtukufu, humu kuna nguo za ndani za Malkia, si vyema zikaonekana hadharani, tunakuomba radhi ufunue boksi hili ukiwa peke yako. Basi mfalme alionekana kukubali na hapo nafsi ikatulia kiasi. Mfalme akaagiza maboksi yote yaingizwe ndani.

 

Boksi ambalo nipo nikachukuliwa na kupelekwa kwengine. Baada ya mwendo wa hatua kadha upatao dakika kama 10 boksi likatuliwa na kufungulia. Hapo nikatoka nje na kupata hewa safi. Mke wa Sultani alipiga makofi kwa kunipongeza nna kuniambia nimefaulu mtihani wa kwanza. Hapo nikapiga magoti kumsalimu na kumshukuru kwa tumaini alilonipa. Aliniangalia kwa muda kama wa dakika 2 hivi na kisha kapiga tena makofi na kusema “umefaulu mtihani wa pili” sikujuwa ni mtihani gani.

 

Akanielekeza pa kukaa huku nikisubiria chakula. Kikaletwa chakula, na vinywaji. Niliishia kunywa maji na chakula. Nilikula kiasi kidogo. Sikutaka kula saana nikiwa ugenni. Niligundua vinywaji vile vinatofautiana rang na harufu. Kwakuwa sukjuwa kwa undani vinywaji vile nikaamuwa ninywe maji tu. Baada ya chakula akaja tena mke wa sultani. Alikaa mbele yangu na kupiga tena makofi na kusema “umefaulu mtihani wa tatu” na sasa nitakuozesha mdogo wangu, il a harusi hii itakuwa ya siri, usijefanyiwa fitina na waliokataliwa posa zao.

 

Nikaelekezwa chumba cha kukaa, mke wa Mfalme akaend kuzungumza na mfalme pamoja na watu wa familia yao.wakakubaliana mahari iwe vipande 500 vya dhahabu. Mke wa mfalme alitowa mahari ili kunitolea na harusi ikafanyika. Sitaki kueleza zaidi kuhusu hiyo harusi. Mambo yakawa kama hivyo, muuza mikanda nimekuwa ndugu na Sultani wa Baghadad.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 ICT       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    4 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    5 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    6 Madrasa kiganjani    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS

Imeandikwa na Drsky Tags Burudani , simulizi , ALL , Tarehe 2021-11-07     Share On facebook or WhatsApp Topic school Zaidi Dini AFYA ICT Burudani Tags Uzazi maswali Afya mengineyo dini HIV Sira vyakula Matunda HTML php Alif Lela 1 Alif Lela 2 FANGASI Dawa SQL Tips Quran Sunnah fiqh DARSA Magonjwa Tajwid tawhid simulizi Dua Academy Wahenga chemshabongo WAJUWA Michezo ICT Imesomwa mara 1187



Post Nyingine


image Utajiri wa baba na kifo chake
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tatu)
Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya kijana Frank na Amisa pia na wapenzi wawili ambao ni James na Amina. Soma Zaidi...

image Jaribio la kwanza la aladini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Safari saba za sinbad
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Hadithi ya mwenye kutabiriwa mtoto wa tajiri
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya tatu)
Post hii inahusu zaidi mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini wakipanda gari kuelekea shule kuanza maisha mapya. Soma Zaidi...

image Hadithi ya waziri aliyeadhibiwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi. Soma Zaidi...

image Siri ya wageni wale inafichuka
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image WAKATI WA KUFUMBUKA
Post hii ni mwendelezo wa hadithi inayohusu Kufumbuka ambapo , John anaonekana kama sio mtoto wa Mzee maganga kwa sababu na miungu imekili kwa sababu chakula chote kimeliwa na kuisha. Soma Zaidi...