Deni la mapenzi


image


Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani


DENI LA MAPENZI

Badisiku ambayo niliamua niuze vitu vya ndani kwangu ili nilipe madeni ya watu, ndipo yule binti akatokea tena. Ilikuwa kama bahati vile akanikabidhi pesa ndefu nikalipa madeni na haikubakia hata kidogo. Siku hiyo alikaa karibu nami na kuanza kuzungumza hapa na pale. Nilimuomba niione sura yake kwa ukaribu zaidi, alimuita mjakazi wake mmoja na kumwambia akae karibu naye, kisha akafunua kitambaa kilichoziba uso wake.

 

Nilipata kujiridhisha baada ya kukutana na nyusi ndefu zilizolala vyema, zilizo nyeusi sana, silizonyooka kama mwezi mwandamo. Macho ya duara yaliyo meupe. Nywele nyembamba, zilizoshuka kukaribia masikio. Hakuwa mweupe sana kama mwarabu wa Sham. Sikupata kujuwa nini amepaka kwenye midomo yake, maana alikuwa anameremeta. Sikutaka zaidi kumuangalia, niliamini itakuwa ni makosa. Kwakuwa nilikuwa naangalia uso, iliniridhisha kukubali uwepo wake.

 

Hatimaye nikatamk maneno kumweleza, kama kuna dawa umenipa. Mwenzio zilali kutwa kucha kukuwaza. Siwachi kufukiri sura yako machoni mwangu. Nakiri kwa ulimi wangu, penzi lako nahitaji. Nilijikuta nabwabwanya maneno yasiyo mpangilio, yasiyo na vina vya mashairi, wala weledi wa mazungumzo. Niliamini kubwabwanya kwangu kutakuwa kumeelewaka japo kidogo. Hakuweza kunijibu kitu chochote, ila alinieleza kuwa atanijibu kwa barua. Lakini aliniomba kuwa nimkopee tena bidhaa kama za siku ile.

 

Hata sikuwahi kufikiri, nikaingia kwenye maduka ya wenzangu na kumchukulia bidhaa zake. Kwa haraka akawaagiza vijakazi wake, wakafunga mzigo na kupotelea mtaani. Baada tu ya kuondoka nikaanza kujiuliza, hivi inamaana utajiri wote alionao yule binti ndo anashindwa kuwa na pesa ya kununulia bidhaa hizi?, ama hii ni mbinu ya matajiri kunyonya wanyonge. Sikuweza kuwaza sana maana kila nikikumbuka sura yake, na kimna ambavyo moyo wangu kwake, hata deni pia nalisahau.

 

Sasa nikawa na mambo mawili ya kusubiria, kwanza barua na pili ni pesa ya watu. Sikumoja mapema asubuhi nikapokea barua kutoka kwa mtu asiyejulikana. Barua iliandikwa kwa maandishi meusi, kutokana na wino wa ngisi uliochanganywa na manukato. Imeandikwa kwenye karatasi nzuri. Kwa shauku nilikata kamba na kufungua barua ile. Maneno machache yaliandikwa:

 

Salam, kipenzi, natumai upo salama. Nashukuru kwa nguo ulionichagulia siku ile imenitosha sawa. Ujumbe wa barua hii utaletewa ifikapo jioni, na pesa yako pia. Basi ilipofika jioni akaja moja kati ya wale wajakazi wake. Akanipatia pesa yangu kisha akaanza kusimulia:-

 

“.….. toka alipoondoka hapa siku ile hakuweza kulala kwa kukuwaza wewe. Anakupenda na amenituma nije nikwambie hivyo. Kama upo tayari anakutaka wende ukaonekane kwao.” kwani anaitwa nani na kwao ni wapi? Huu ni mzigo wa maswali nilio mjibu. Anaitwa Shaniat bint ‘Aziz mkwe wa sultani Harun Rashid. Mmh sasa nitafikaje kwao?” nilimuulliza. “…. kuna mtihani umepewa na mke wa mfalme, uende kwa siri, ukifanikiwa atafanya taratibu zote za harusi yetu badala ya kuridhishwa nawe atakapo kuona, na kama ukifeli ukakamatwa, basi utapoteza maisha” haya ndiyo maneno aliyonijibu.

 

Sikujuwa ni kwa nini ameamuwa kunipa mtihani huu. Lakini nilijuwa kuwa kama nisipoweza kumuona ka masiku mengi zaidi huwenda nikawa kichaa ama punguani. Niliamini ni bora nijaribu kwenda kwa siri nikifa nife kiume, kuliko kubakia hapa na kujiwazia naishia kukumbatia ukuta. Nikamjibu kuwa nimekubali. Basi akanielekeza kuwa kesho mida ya jioni niende kwenye bostani lililopo karibu na ikulu na hapo nitakutana nae.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Ndani ya pango la makaburi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Aladini katika pango la utajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Mshenga wa aladini mbele ya mfalme kwa mara ya pili
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)
Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini. Soma Zaidi...

image Kwisha kwa chakula
Posti hii inakwenda kukuletea muendelezo wa safari za Sinbad Soma Zaidi...

image Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi. Soma Zaidi...

image Hadithi ya Mama mchoyo na mwehu
Posti hii inahusu zaidi habari za Mama mmoja aliyekuwa mchoyo akampa mkate mwehu na kuutia Sumu ila kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu sana aliutunza mkate na kuwapatia watoto wa yule mama waliokuwa wakitoka shule na njaa kali Soma Zaidi...

image Hadithi ya chongo watatu wa mfalme na wanawake wa Baghdad
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Utajiri wa baba na kifo chake
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu. Soma Zaidi...