Kwanini vidole gumba vilikatwa

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa y

KWA NINI VIDOLE GUMBA VILIKATWA?

Baada ya harusi niliendelea kukaa pale kwa muda wa miezi mitatu hata bila ya kurudi kwangu au kuwasiliana na ndugu zangu. Siku moja mkewangu akanieleza kuwa ana ujauzito. Nilifurahi sana, nilimkumbatia kwa furaha. Habari njema zikamfikia mke wa Sltani, basi akaandaa tafrija ndogo ya pale ndani kama kusherekea furaha ya mdogo wake kuata ujauzito. Katika tafrija hiyo muda wa kula ulipofika vyakula mbalimbali vikaletwa.

 

Nikanawa mikono na kuanza kula. Mkewangu hakuwepo alitokakidogo. Nilitamani hata awepo nipate kumlisha. Nilianza kula na kunywa kisha kikala Zerbajeh, nilipogusa tu chakula kile badhi ya wajakazi walikunja sura, Mke wa Sultani akanieleza kuwa mke wako anachukia sana harufu ya chakula hiko, na ndo umeshaanz akula, hivyo itakubidi uvumilie kwa lolote litakalo tokea. Sisi katu hatuta ingilia ugomvi wenu. Basi nilijitahidi kunawa vyema kwa sabuni. Baada ya tafrija kwisha nikarudi kujipumzisha.

 

Ghafla nikaona mkewangu amebadilika sura, na kuniambia “yaani mtu kama wewe unakula zerbajeh bila hata ya kunawa”? nikamueleza mkewangu kipenzi mbona nimenawa” kama umenawa na hii harufu ninayoipata ni ya nini” “ nimejitahidi kunawa ila hii harufu haikati kwa urahisi” haya ni maneno tuliokuwa tukijibizana.

 

Looo!!! Looo!!!! huwezi amini kumbe kubishana ndipo nikawa nauchochea moto wa kifuu. “nilikuona mstaarabu, nikakupenda, na nakupenda sana kipenzi, lakini kwa hili katu siwezi kuvumilia….,” mtu mstaarabu kama wewe unakula bila kunawa jamani, hapana …!! hapana…!!! kwa hili lazima nikupe adhabu, itabidi ukatwe vidole vyako. Ulivyokulia bila ya kunawa.

 

Aliagiza wajakazi wanifunge wanipeleke kwa hakinu ili nikakatwe vidole. Wakanifunga kamba na kunifungia kwenye chumba. Nilikaa kwa siku 10 kwenye kachumba hako huku nikawa ninakula mlo mmoja tu kwa siku. Siku ya kumi akawaambia wajakazi wanitoe, akaninusa mikono yangu na kujiridhisha kuwa harufu imekoka. Hapo akaagiza dawa ziletwe na mkasi, bendeji na vitu vingine. Akawaambia wajakazi wanikamate madhubuti, na hapo akanikata vidole gumba vyangu vyote

 

“nakukata hivi vidole vilivyokuacha ukala zerbajeh bila ya kunawa. Nataka ukumbuke kuwa chakula hiki, utakapokula unawe mara 40 kwa alita, mara 40 kwa sabuni na mara 50 kwa maji. Vinginevyo nitamaliza na vingine. Nilijiwazia mambo mengi hata nikasema huwenda ni huu ujauzit ndio unamsumbuwa. Lakini ujauzto ndi anikate vidole. Baada ya hapo alilia sana na akachukuwa dawa akanipaka na kuendelea kuniuguza.

 

Niligunduwa kuwa ananipenda sana, japo sikupatapo kujuwa hasa kilichomtokea hata akachukia sana chakula hiki. Milipanga siki moja nije nimuulize. Baada ya wiki kama 3 vidonda vyangu vilipona na hapo akaja mke wa sultani na aliponikuta akapiga tema makofi na kuniambia kuwa “umefaulu mtihani wa nne” sasampohuru kuondoka. Sikuwa naelewa maneno ya mke waSultani kuhusu mitihani ile lakini pia nilifurahi.

 

Jioni mke wangua akanipatia pesa nyingi na vipande vya dhahabu na kunieleza kuwa nikanunue nyumba nzuri ya ssi kuishi. Nilifanya hivyo, nilitafuta nyumba nzuri sana nje kidogo ya mji na sasa nina watoto wawili. Nimeamua leo kuja kufurahi na watu wa mjini ndipo nikakutana na shuhuli hii.

 

Baada ya huyu bwana kusimulia habari yake, basi mjakazi wa Sultani akamwambia Sultani, Je! Hadithi hii si yenye kushangaza kuliko hadithi ya mtoa burudani? Hapo sultani akasema “ni nzuri ila bado haijashinda hadithi ya mtoa burudani” kufikia hapo tabibu akapiga magoti na kusema “mtukufu Sultani, nitasimulia hadithi ya kushangaza zaidi kuliko mazungumzo yaliyo tangulia, kama utaikubali zaidi iwe kafara la tukio la leo. Hapo tatibu akaanza kusimulia hadithi yake

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-07     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 601

Post zifazofanana:-

Jinsi uislamu ulivyokomesha biashara ya utumwa wakati na baada ya mtume Muhammad (s.a.w)
Soma Zaidi...

Dalili za vidonda vya tumbo
Vidonda vya tumbo no tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda,hutokea baada ya ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaitwa mucus kuharibika. Vidonda vya tumbo (peptic ulcers) imegawanyika katika ma Soma Zaidi...

Uwepo wa asidi nyingi mwilini
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kuwepo kwa asidi nyingi mwilini hali uwasumbua watu wengi na kufikia kiasi cha kusababisha madhara mengine mawilini ikiwamo pamoja na kansa ya koo, ili kujua kama una wingi wa asildi mwilini unapaswa kujua dalili kama ifu Soma Zaidi...

vidonda vya tumbo, dalili zake, chanzo chake na tiba yake
Makala hii itakwenda kukupa elimu juu ya vidonda vya tumbo, nini hasa chanzo chake, vipi vinatokea ni zipi dalili zake, ni zipi njia za kujilinda dhidi ya vidonda vya tumbo. Pia tutaangalia matibabu ya kutibi vidonda vya tumbo. Soma Zaidi...

Namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni
Post hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni, ni njia zinazotumika kuzuia maambukizi kwenye nephroni Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI (sehemu ya sita)
Post inahusu zaidi hadithi ya NIMLAUMU NANI ambayo ni sehemu ya sita, katika kipengele hiki tunaenda kumwona msichana Amina anapambana na hatimaye anafunga ndoa ya kiserikali na Frank Soma Zaidi...

Madhara ya kutotibu uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu ugonjwa wa uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo,ni madhara yanayotokea kwenye mfumo mzima wa kupitisha mkojo na via vya uzazi kama ifuayavyo. Soma Zaidi...

Magonjwa ya kuambukiza
Magonjwa ya kuambukiza: Ni yale yanayoweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine au kutoka kwa wanyama kwenda kwa mtu Mlipuko tukio lililoenea la ugonjwa katika jamii kwa wakati fulani ambao huonekana kama kesi mpya kwa kiwango ambacho kinazi Soma Zaidi...

Mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo chini ya umri wa miaka mitano ili kuweza kuweka afya yake kwenye njia safi. Soma Zaidi...

Ifahamu dawa ya kutibu kifua kikuu
Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu. Soma Zaidi...

Mimi naumwa na tumbo chini ya kitovu upande wa kulia, ninapotok kushiriki tendo la ndoa ndonapata maumivu zaid pia nawashwa sehemu za siri itakuwa shida ni nin?
Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa yanaweza kuwa ni dalili ya maradhi fulani, ama shida kwenye mfumo w uzazi. PID na UTI hutuhumiwa kuwa ni katika sababu hizo. Ila zipo nyingine nyingi tu. Kama ina hali hii vyema ukafika kituo cha afya Soma Zaidi...

Fahamu mapacha wanavyounganishwa.
Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa vijusi viwili vitakua kutoka kwa kiinitete hiki, wataendelea kushikamana mar Soma Zaidi...