Kipi kingine utafanya ukiwa Facebook

Somo hili linakwenda kukueleza Mambo mengne unayoweza kuyafanya ukiwa Facebook

KIPI KINGINE UTAFANYA UKIWA FACEBOOK

Facebook ni mtandao wa kwanza wa kijamii (social media) unaotembelewa na watu wengi. Mitandao mingine ni kama twitter, linkedin, youtube, whatsApp, instagram na mingine mingi. Facebook imeanzishwa huko marekani, na imekuwa ikiongeza nguvu kila kukicha na kuboresha huduma zake zaidi kila siku. Leo facebook imekuwa ni kituo cha kufanya mengi zaidi ya mtumiaji wa kawaida anavyotambua. Katika makala hii nitakueleza matumizi mengine ya facebook ambayo watu wengi hawayajui.

 

Mtumiaji wa kawaida wa facebook amezoea kulogin na kuchat kwa sms, kushare picha, maoni, video na masimuliz, kupiga simu ya sauti yu ama video. Pia hutumika facebook kwa kuhifadhi taarifa binafsi pamoja na kuupdate wasifu wako. Hebu tuone baadhi ya matumizi mengine unayoweza kuyafanya ukiwa facebook

 

1. Kutangaza biashara na wasifu wako. Facebook ni njia ya haraka kwa anayetaka kutangaza wasifu wake, biashara yake ama kampuni. Ukiwa marafiki, na watu wengi wanaokufuata unaweza kuitumia nafasi hii kwa ajili ya kutangaza kile unachokitaka watu wakijue.

2. Unaweza kutumia facebook kama kituo cha kukupatia kipato. Wapo watu wengi leo wanajiingizia kipato kwa kutumia facebook, kwa mfano watu wanaomiliki kurasa za video wanaweka matangazo ya watu na kujiingizia kipato. Pia unaweza kutumia fursa hii ya facebook kutangaza biashara yako na kupata wateja. Sambamba na haya unaweza kujiingizia kipato kwa kutumia makala unazoandika kwenye ukurasa wako unaoumiliki.

3. Unaweza kufanya mikutano ya siri, watu maalumu ama ya hadhara, inaweza kuwa kwa kutumia video ama kwa sauti tu. Halikadhalika pia mikutano hii inaweza kuwa ya njia ya maandishi kama mkipenda pia.

4. Pia unaweza kucheza gemu ukiwa facebook. Huna haja ya kudownload gemu, ukiwa na simu ya smartphone

5. Kukusanya taarifa kuhusu mtu, watu, kikundi ama kampuni. Taarifa hizi zinaweza kuwa: namba ya simu, barua pepe (email), familia, sehemu, marafiki, vitu anavyopenda, mawazo yake kuhusu siasa, dini ama jamii, tabia yake na vitu anavyochukia. Pia unaweza kupata taarifa za mtu kuhusu vitabu anavyosoma, watu anaowafuata, video ama miziki anayotazama na kusikiliza, tarehe ya kuzaliwa na anapofanya kazi ama shule alizosoma, sambamba na kiwango cha elimu yake. Miongoni mwa taarifa hizi watu wengi wanadangaya ukweli wa mambo hususani majina na tarehe ya kuzaliwa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Teknolojia Main: Jifunze File: Download PDF Views 1138

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Muda wa kuchaji simu yako

Posti hii itakwenda kukujuza juu ya kuda mzuri wa kuchaji simu yako

Soma Zaidi...
Utafanyaje ili blog yako ionekane Google, Big, Yandex ama yahoo?

Post hii inakwenda kukufundisha kwa ufupi jinsi ya kuifanya blog yako, ama post za kwenye blog yako ziweze kupatikana kwenye search Engine kama Google, Bong, yandex na yahoo.

Soma Zaidi...
yanayoathiri betri ya kifaa chako

makala hii itakuelezea mambo makuu ambayo ni hatari kwa usalama wa betri ya kifaa chako

Soma Zaidi...
Maana ya legacy contact katika Facebook

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya legacy contact katika facebook

Soma Zaidi...
Chanzo

Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta..

Soma Zaidi...
EPUKA MALWARE (VIRUSI, WORM NA TROJAN UKIWA MTANDAONI)

Malware ni neno pana na watu wengi si wenye kulitumia.

Soma Zaidi...
Epuka malware (virus,work)ukiwa mtandaoni

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuepuka malware ukiwa mtandaoni

Soma Zaidi...
Nini Chanzo

Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta..

Soma Zaidi...