EPUKA MALWARE (VIRUSI, WORM NA TROJAN UKIWA MTANDAONI)
Malware ni neno pana na watu wengi si wenye kulitumia.
EPUKA MALWARE (VIRUSI, WORM NA UKIWA MTANDAONI
Malware ni neno pana na watu wengi si wenye kulitumia. Malware hukusanya maana za virusi, trojan, spyware na worm. Watu wengi wamezoea kutumia neno virusi. Utasikia mtu anasema kuwa simu yake ina virusi. Kwahiyo virusi ni sehemu ndogo sana ya malware.
Mara nyingi virusi hawawezi kuharibu mafaili kwenye kifaa chako ila huathiri utendaji wa kazi wa kifaa chako. Virusi huweza kujizalisha wenyewe kwa wenyewe ndani ya kifaa chako. Worm wanaweza kutembea kutoka faili moja mpaka jingine. Kuna tofauti kubwa kati ya virusi, worm na trojan.
Malware ni program ama software ama code zinazoingizwa kwenye kifaa chako kama simu ama kompyuta, na kuunganisha kifaashako na mitandao ya watu au kuharibu taarifa (data) za kwenye kifaa chako. Malwarei huweza kuingia kwenye kifaa chako kwa kupitia:
- Waya wa USB
- Flash
- Ukiwa mtandaoni kwa kudownload mafaili, kufungua email (barua pepe)
- Bluetooth
- Kushea mafaili kwa njia nyinginezo.
Malware huondolewa kwenye kifaa chako kwa kutumia program za kuondoa malware zijulikanazo kama antivirus. Kuna program (software) nyingi ambazo zinaweza kufanya kazi hui ya kuondoa malware ikiwemo virusi. Program hizo ni pamoja na avast, kerspersky, avag, window defender na nyinginezo nyingi. Pia kwa watumiaji wa simu google playstore inafanya kazi hiyo bure kwa kuscan App zote ulizoziinstall.
Njia za kujilinda na malware
- Weka antivirus kwenye kifaa chako.
- Hakikisha unascan kifaa chako mara kwa mara
- Scan waya wa USB
- Kuwa makini unapotuckuwa mafaili kwa kutumia bluetooth ama njia nyingine. Vi vyema ukascan mafaili hayo
- Kuwa makini na kudownload kitu usichokijua, ama kufungua mafaili ama email usisozijua.
- Kuwa makini na matangazo yanayotaka uclick eitha upate zawadi ama bonasi
- Scan mafaili yote ulioyadownload.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 web hosting 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Kipi kingine utafanya ukiwa Facebook
Somo hili linakwenda kukueleza Mambo mengne unayoweza kuyafanya ukiwa Facebook
Soma Zaidi...Utajuaje Kama simu au kompyuta yako Ina virus
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kujua Kama simu yako ina virus
Soma Zaidi...Nini Chanzo
Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta..
Soma Zaidi...MUDA WA KUCHAJI SIMU YAKO AMA MUDA WA KUCHAJI BETRI YAKO
Wwatu wengi wamekuwa wakijiuliza ni muda gani hasa inapasa kuchaji simu, je nisubiri mpaka chaji iishe kabisa, ama nichaji ikiwa na asilimia ngap?
Soma Zaidi...Kutuma sms ndefu
Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta..
Soma Zaidi...