Habari nasumbuliwa na tumbo upande wakilia adi nikikojoa mkojo wa mwisho uwa wa kahawia tiba take nini?
Maumivu ya tumbo yanaweza kusababishwa na mambo mengi ikiwemo typhod, vidonda vya tumbo na shida nyingine kwenye mfumo wa chakula.
Swali:
Habari nasumbuliwa na tumbo upande wakilia adi nikikojoa mkojo wa mwisho uwa wa kahawia tiba take nini?
Maumivu kwenye tumbo upande wa kulia yanaweza kuwa ni dalili ya shida kwa afya. Mfano maumivu haya yanaweza kusababishwa na: -
1. Tumbo kujaa gesi
2. Shida kwenye figo
3. Mimba iliyotungia nje
4. Shida kwenye mfumo wa uzazi kama ovari
5. Ugonjwa wa PID
6. Kukosa choo
7. Hekima
8. Apendix
Zipo sababu nyingi zinazosababisha maumivu haya. Majibu hutegemea nanamna ambavyo yanauma. Pia baada ya vipimo utapata majibu hasa.
Maumivu haya yanaweza kuondoka hata bila ya kumeza dawa. Lakini kufika Kituo cha afya ni vyema zaidi.
Muone haraka daktari endapo maumivu haya yatachanganyika na: -
1.Maumivu na mkandamizo kwenye kifua
2.Homa
3.Damu kwenye kinyesi
4.Kuendelea kwa kichefuchefu na kutapika kwa masiku kadhaa.
5.Ngozi kuwa na rangi ya njano
6.Kukaza kwa tumbo sana unapoligusa
Ama kuhusu mabadiliko ya rangi ya mkojo, kunywa maji kwa wingi ama fika kituo cha afya kupima UTI.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 ai web app 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dalili na ishara za kuvimba kope.
Posti hii inaonyesha Dalili na ishara za kuvimba kope ambayo kitaalamu hujulikana Kama blepharitis.
Soma Zaidi...Vidonda vya tumbo husababishwa na nini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu visababishi vya vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Dalili za kisukari na njia za kuzuia kisukari
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisakari, dalili zake,na namna ya kujikinga usipate kisukari au Kama tayari unakisukari ukijikinga madhara yanapungua au kupona kabisa.Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwa
Soma Zaidi...Mambo yanayosababisha kuharisha
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuharisha, kuharisha ni kitendo Cha kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisichokuwa na damu
Soma Zaidi...Je unaijuwa ugonjwa wa bawasiri
Katika post hii nitakwenda kukujuza kuhusu ugonjwa wa bawasiri
Soma Zaidi...