Habari nasumbuliwa na tumbo upande wakilia adi nikikojoa mkojo wa mwisho uwa wa kahawia tiba take nini?
Maumivu ya tumbo yanaweza kusababishwa na mambo mengi ikiwemo typhod, vidonda vya tumbo na shida nyingine kwenye mfumo wa chakula.
Swali:
Habari nasumbuliwa na tumbo upande wakilia adi nikikojoa mkojo wa mwisho uwa wa kahawia tiba take nini?
Maumivu kwenye tumbo upande wa kulia yanaweza kuwa ni dalili ya shida kwa afya. Mfano maumivu haya yanaweza kusababishwa na: -
1. Tumbo kujaa gesi
2. Shida kwenye figo
3. Mimba iliyotungia nje
4. Shida kwenye mfumo wa uzazi kama ovari
5. Ugonjwa wa PID
6. Kukosa choo
7. Hekima
8. Apendix
Zipo sababu nyingi zinazosababisha maumivu haya. Majibu hutegemea nanamna ambavyo yanauma. Pia baada ya vipimo utapata majibu hasa.
Maumivu haya yanaweza kuondoka hata bila ya kumeza dawa. Lakini kufika Kituo cha afya ni vyema zaidi.
Muone haraka daktari endapo maumivu haya yatachanganyika na: -
1.Maumivu na mkandamizo kwenye kifua
2.Homa
3.Damu kwenye kinyesi
4.Kuendelea kwa kichefuchefu na kutapika kwa masiku kadhaa.
5.Ngozi kuwa na rangi ya njano
6.Kukaza kwa tumbo sana unapoligusa
Ama kuhusu mabadiliko ya rangi ya mkojo, kunywa maji kwa wingi ama fika kituo cha afya kupima UTI.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Madrasa kiganjani π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Kitau cha Fiqh π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Kitabu cha Afya π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Fangasi aina ya Candida
Huu ni ugonjwa wa fangasi wanaosababishwa na mashambulizi ya fangani aia ya yeast waitwao candida.
Soma Zaidi...Vitamini B12: Kazi zake na vyakula vyenye wingi wake.
Vitamini B12 (cobalamin) ni kirutubisho muhimu sana ambacho mwili wa binadamu hauwezi kujitengenezea wenyewe. Ni vitamini inayoyeyuka kwenye maji na ina jukumu la msingi katika kudumisha mfumo wa neva, utengenezaji wa damu, na ufanisi wa DNA. Ukosefu wake unaweza kusababisha madhara makubwa kiafya, ikiwemo upungufu wa damu na matatizo ya neva. Makala haya yanalenga kutoa elimu kuhusu kazi za vitamini hii na jinsi unavyoweza kuipata kupitia lishe bora.
Soma Zaidi...Maumivu ya mgongo.
Post yetu Leo inaenda kuzungumzia Maumivu ya nyuma ni malalamiko ya kawaida. Kwa upande mkali, unaweza kuchukua hatua za kuzuia au kupunguza matukio mengi ya maumivu ya mgongo. Ikiwa kinga itashindikana, matibabu rahisi ya nyumbani na mbinu sahihi za m
Soma Zaidi...Sababu za mwanamke kuumwa tumbo y chini ya kitovu.
Posti hii inahusu sababu za mwanamke kuumwa tumbo chini ya kitovu, ni tatizo ambalo limewapata wanawake wengi na pengine sababu ni vigumu kupata au pengine zinapatikana lakini kwa kuchelewa hali ambayo usababisha madhara mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Faida za kufanya mazoezi kila siku
βKatika somo hili, tunaangazia jinsi mazoezi ya kila siku yanavyochangia katika kuimarisha mfumo wa moyo, kudhibiti uzito, kuboresha afya ya akili, na kuongeza nguvu ya mwili. Tunaeleza faida hizi kulingana na ushahidi wa kisayansi na kutoa mwongozo mfupi wa jinsi ya kuanza mazoezi ili kupata matokeo bora
Soma Zaidi...