Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao
Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.
2. Fangasi wa mapunye;
Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni. Kitaalamu fangasi hawa hujulikana kama tinea” au “dermatophytosis. Na kwa maarufu sana wanafahamika kama ringworm kwa kuwa wanatoa mabako ya mduara kwenye ngozi.
Fangasi hawa wanaweza kukaa kwenye ngozi, kuta, nguo, taulo na maeneo mengine. Miongoni mwa dalili zao ni kuona maduara kwenye ngozi, mara nyingi dalili za fangasi hawa huweza kuonekana kuanzia siku 4 mpaka 14 baada ya ngozi kupata maambukizi ya fangasi hawa. zifuatazo ni katika dalili za fangasi hawa:-
- Kuwasha kwa ngozi na maumivu wakati mwingine
- Kuwepo kwa mapele ama ukurutu uliotengeneza umbo la duara
- Ngoz kuwa nyekundu, kupasuka ama kuwa kavu
- Kukatika ama kunyonyoka kwa nywele kwenye sehemu iliyo athirika
Fangasi hawa wanaweza kukaa katika maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha dalili tofautitofauti kulingana na eneo lililo athirika. Kwa mfano;-
Fangasi hawa wakiwa kwenye nyayo (sthlete’s foot) huweza kuonesha dalili kama nyayo kuwa nyekundu, kuvimba ama kujaa maji, ngoxi kutoka ama kubabuka, kuwasha kwa ngozi katikati ya vidole na kidole na mara nyingi kati ya kidole kidogo na kinachomfatilia. Wakati mwingine kisigino na nyayo huweza kuathirika na kuweka mabumbuza.
Kwenye kichwa, fangasi hawa huweka maduara yaliyo nyonyoka ngozi, yakiwa na ukurutu, ngozi kavu, na kuwasha. Maduara haya maarufu tunayaita mapunye, yanaweza kuwa mengi na kuungana kufanya duara moja kubwa. Mara nyingi sana fangasi wa kichwani huwapata sana watoto kuliko watu wazima.
Kwenye pachipachi za mapaja (jock itch). Fangasi hawa hukaa sehemu ya ndani ya mapaja karibu na sehemu za siri ama kuzungukia eneo hilo, lakini wanashambulia mapaja. Miongoni mwa dalili zao ni mapaja kufanya wekundu, kuwasha na hali inaweza kuwa mbaya mpaka ngozi ikababuka na hatimaye kufanya vidonda kwa kujikuna. Wanaweza kushambulia pia korodani na kufanya ibabuke, iwe nyekundu na kuweka vidonda.
Fangasi wa kwenye ndevu (tinea barbae). fangasi hawa wanashambulia maeneo ambayo ndevu zinapatikana kama kwenye kidevu na shavu. Dalili zao ni kuwasha kwa kidevu, shavu, na sehemu ya juu ya shingo. Fangasi hawa wanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha mapele yenye usaha kwenye eneo hili.
Huweza kuwapata wenye ndevu ama ambao wananyoa ndevu. Dalilizao ni kama za fangasi wa maeneo mengine, kama eneo kuwa jekundu, kuwasha kuwa na madoamadoa na kunyonyoka kwa ndevu katika eneo lililo athirika.
Walio hatarini zaidi kupata fangasi hawa
Watu wote wanaweza kupata fangasi hawa wa mapunye. Lakini kuna watu wengine wapo hatarini zaidi. Na hii ni kutokana na shughuli zao wanazofanya, mazingira wanayoishi ama staili za maisha yao.
- Watu wenye mfumo wa kinga dhaifu
- Watu wanotumia changia sehemu moja ya kuwekea nguo
- Watu wanaofanya shughuli ambazo hugusana gusana kwa mfano wanaofanya miereka.
- Watu wanaovaa nguo za kubana sana
- Watu wanaogusana gusana na wanyama wenye mapunye.
Namna ya kujilinda na mapunye
- Weka ngozi yako katika hali ya usafi
- Vaa viatu ambavyo vinaruhusu hewa kupita kwenye nyayo zako
- Usitembee miguu peku hasa kwenye maeneo yenye watu wengi
- Kata kucha zako ziwe fupi na ziweke katika hali ya usafi
- Badilisha soksi zako na nguo za ndani (chipi, boksa n.k) japo mara moja kwa siku
- Usichangie nguo zako na mtu mwingine
- Kama uanfanya kazi inayohitaji kugusana gusana kwa ngozi hakikisha unaoga mara kwa mara kwa siku.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Bongolite - Game zone - Play free game π2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π3 web hosting π4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π5 kitabu cha Simulizi π6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Madhara ya kushindwa kupitisha mkojo.
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kushindwa kupitisha mkojo, ni madhara makubwa yanayotokea kwa mtu iwapo akishindwa kupitisha mkojo.
Soma Zaidi...Dalili za mimba kutunga nje ya kizazi (Ectopic Pregnancy).
Mimba kutunga nje ya kizazi (Ectopic Pregnancy) ni hali ya dharura ya kitabibu ambapo yai lililorutubishwa linajipandikiza nje ya mji wa mimba, mara nyingi katika mirija ya uzazi (Fallopian tubes). Hali hii ni hatari sana kwa maisha ya mama kwani kiumbe kinachokua hakiwezi kustahimili kukua nje ya mji wa mimba, na kinaweza kusababisha mrija kupasuka na kusababisha damu nyingi kuvuja ndani ya tumbo.
Soma Zaidi...Athari za mabadiliko ya misimu (Seasonal Affective Disorder).
Seasonal Affective Disorder (SAD)βaina ya sonona inayochochewa na mabadiliko ya hali ya hewa na misimu. Makala haya yanachambua dalili zake, sababu za kisayansi, na jinsi ya kukabiliana nayo ili ubaki na furaha na utulivu mwaka mzima.
Soma Zaidi...Athari za unywaji pombe na sigara wakati wa ujauzito.
Ujauzito ni kipindi muhimu ambacho afya ya mama huathiri moja kwa moja ukuaji na ustawi wa mtoto aliye tumboni. Makala hii inachunguza kwa kina madhara ya kiafya yanayotokana na matumizi ya pombe na sigara wakati wa ujauzito. Tunajadili jinsi vitu hivi vinavyovuka kizuizi cha plasenta (placenta) na kuathiri mfumo wa neva, viungo, na ukuaji wa mtoto, huku tukitoa ushauri wa kitaalamu wa jinsi ya kuacha tabia hizi kwa ajili ya usalama wa mtoto na mama.
Soma Zaidi...Uchovu wa akili na mwili (Burnout): Dalili na ahueni.
Andika post ya blog yenye kichwa 'Uchovu wa akili na mwili (Burnout): Dalili na ahueni.', muhtasari, utangulizi, maudhui, fact check (Je! wajuwa?) na hitimisho. Post iwe ndefu zaidi ya maneno 1200 na iwe tayari kwa ajili ya SEO. Andika kwa kiswahili cha kitaalamu.bold heading
Soma Zaidi...Homa ya ini Nini Nini, na husababishwa na nini
Katika post hii utajifunza maana ya homa ya ini. Pia utajifunza chanzo kinachosababisha homa ya ini. Makala hii itakuwa endelevu hivyo usikose muendelezo wake.
Soma Zaidi...