picha

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

2. Fangasi wa mapunye;

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni. Kitaalamu fangasi hawa hujulikana kama tinea” au “dermatophytosis.  Na kwa maarufu sana wanafahamika kama ringworm kwa kuwa wanatoa mabako ya mduara kwenye ngozi.

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa kwenye ngozi, kuta, nguo, taulo na maeneo mengine. Miongoni mwa dalili zao ni kuona maduara kwenye ngozi, mara nyingi dalili za fangasi hawa huweza kuonekana kuanzia siku 4 mpaka 14 baada ya ngozi kupata maambukizi ya fangasi hawa. zifuatazo ni katika dalili za fangasi hawa:-

  • Kuwasha kwa ngozi na maumivu wakati mwingine
  • Kuwepo kwa mapele ama ukurutu uliotengeneza umbo la duara
  • Ngoz kuwa nyekundu, kupasuka ama kuwa kavu
  • Kukatika ama kunyonyoka kwa nywele kwenye sehemu iliyo athirika

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa katika maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha dalili tofautitofauti kulingana na eneo lililo athirika. Kwa mfano;-

 

Fangasi hawa wakiwa kwenye nyayo (sthlete’s foot) huweza kuonesha dalili kama nyayo kuwa nyekundu, kuvimba ama kujaa maji, ngoxi kutoka ama kubabuka, kuwasha kwa ngozi katikati ya vidole na kidole na mara nyingi kati ya kidole kidogo na kinachomfatilia. Wakati mwingine kisigino na nyayo huweza kuathirika na kuweka mabumbuza.

 

Kwenye kichwa, fangasi hawa huweka maduara yaliyo nyonyoka ngozi, yakiwa na ukurutu, ngozi kavu, na kuwasha. Maduara haya maarufu tunayaita mapunye, yanaweza kuwa mengi na kuungana kufanya duara moja kubwa. Mara nyingi sana fangasi wa kichwani huwapata sana watoto kuliko watu wazima.

 

Kwenye pachipachi za mapaja (jock itch). Fangasi hawa hukaa sehemu ya ndani ya mapaja karibu na sehemu za siri ama kuzungukia eneo hilo, lakini wanashambulia mapaja. Miongoni mwa dalili zao ni mapaja kufanya wekundu, kuwasha na hali inaweza kuwa mbaya mpaka ngozi ikababuka na hatimaye kufanya vidonda kwa kujikuna. Wanaweza kushambulia pia korodani na kufanya ibabuke, iwe nyekundu na kuweka vidonda.

 

Fangasi wa kwenye ndevu (tinea barbae). fangasi hawa wanashambulia maeneo ambayo ndevu zinapatikana kama kwenye kidevu na shavu. Dalili zao ni kuwasha kwa kidevu, shavu, na sehemu ya juu ya shingo. Fangasi hawa wanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha mapele yenye usaha kwenye eneo hili.

 

Huweza kuwapata wenye ndevu ama ambao wananyoa ndevu. Dalilizao  ni kama za fangasi wa maeneo mengine, kama eneo kuwa jekundu, kuwasha kuwa na madoamadoa na kunyonyoka kwa ndevu katika eneo lililo athirika.

 

Walio hatarini zaidi kupata fangasi hawa

Watu wote wanaweza kupata fangasi hawa wa mapunye. Lakini kuna watu wengine wapo hatarini zaidi. Na hii ni kutokana na shughuli zao wanazofanya, mazingira wanayoishi ama staili za maisha yao.

  • Watu wenye mfumo wa kinga dhaifu
  • Watu wanotumia changia sehemu moja ya kuwekea nguo
  • Watu wanaofanya shughuli ambazo hugusana gusana kwa mfano wanaofanya miereka.
  • Watu wanaovaa nguo za kubana sana
  • Watu wanaogusana gusana na wanyama wenye mapunye.

 

Namna ya kujilinda na mapunye

  1. Weka ngozi yako katika hali ya usafi
  2. Vaa viatu ambavyo vinaruhusu hewa kupita kwenye nyayo zako
  3. Usitembee miguu peku hasa kwenye maeneo yenye watu wengi
  4. Kata kucha zako ziwe fupi na ziweke katika hali ya usafi
  5. Badilisha soksi zako na nguo za ndani (chipi, boksa n.k) japo mara moja kwa siku
  6. Usichangie nguo zako na mtu mwingine
  7. Kama uanfanya kazi inayohitaji kugusana gusana kwa ngozi hakikisha unaoga mara kwa mara kwa siku.


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 9327

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 ai web app     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Kutokwa na uchafu mweupe ukeni: Ni ugonjwa?

Kutokwa na uchafu ukeni ni jambo la kawaida kwa kila mwanamke aliyefikia umri wa kuvunja ungo. Hata hivyo, wengi hukumbwa na hofu pindi wanapoona mabadiliko katika rangi, harufu, au wingi wa uchafu huo. Makala hii inafafanua tofauti kati ya uchafu wa kawaida (physiological discharge) na ule unaoashiria ugonjwa (pathological discharge), na kutoa mwongozo wa wakati wa kutafuta msaada wa kitaalamu.

Soma Zaidi...
Dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo

Zijuwe dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo, kama kiungulia, tumbo kujaa, maumivu ya umbo..

Soma Zaidi...
Chakula bora kwa watoto chini ya miaka mitano.

Miaka mitano ya kwanza ya maisha ni kipindi cha ukuaji wa kasi, ambapo lishe sahihi inaamua msingi wa afya ya kimwili na kiakili kwa maisha yote. Makala haya yanachunguza mahitaji ya lishe kwa watoto wadogo, kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya vyakula bora, na kutoa mwongozo wa namna ya kujenga tabia njema za ulaji ili kuzuia utapiamlo na magonjwa yasiyoambukiza.

Soma Zaidi...
Usingizi mzuri: Faida zake kiafya na jinsi ya kuupata.

Usingizi mzuri ni nguzo ya msingi ya afya ya binadamu, ikiwa na umuhimu sawa na lishe bora na mazoezi ya viungo. Katika ulimwengu wa sasa wenye shughuli nyingi, wengi wetu hupuuza umuhimu wa kupata usingizi wa kutosha. Makala haya yanachunguza faida za ajabu za usingizi kwa mwili na akili, pamoja na mbinu za kisayansi unazoweza kuzitumia ili kuhakikisha unapata mapumziko bora kila usiku.

Soma Zaidi...
Namna ya Kudumisha Upendo Kwenye Ndoa

Kudumisha upendo katika ndoa ni mchakato endelevu unaohitaji jitihada, uelewano, na heshima kutoka kwa pande zote mbili. Post hii inatoa mwongozo wa vitendo kuhusu jinsi ya kurejesha cheche ya mapenzi na kuimarisha uhusiano wenu wa ndoa ili uwe na furaha ya kudumu.

Soma Zaidi...
Dalili za Maambukizi kwenye mifupa

Posti hii inahusu zaidi dalili za Maambukizi kwenye mifupa, ni dalili ambazo ukionyesha kwa mtu mwenye Maambukizi kwenye mifupa.

Soma Zaidi...