picha

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

2. Fangasi wa mapunye;

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni. Kitaalamu fangasi hawa hujulikana kama tinea” au “dermatophytosis.  Na kwa maarufu sana wanafahamika kama ringworm kwa kuwa wanatoa mabako ya mduara kwenye ngozi.

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa kwenye ngozi, kuta, nguo, taulo na maeneo mengine. Miongoni mwa dalili zao ni kuona maduara kwenye ngozi, mara nyingi dalili za fangasi hawa huweza kuonekana kuanzia siku 4 mpaka 14 baada ya ngozi kupata maambukizi ya fangasi hawa. zifuatazo ni katika dalili za fangasi hawa:-

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa katika maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha dalili tofautitofauti kulingana na eneo lililo athirika. Kwa mfano;-

 

Fangasi hawa wakiwa kwenye nyayo (sthlete’s foot) huweza kuonesha dalili kama nyayo kuwa nyekundu, kuvimba ama kujaa maji, ngoxi kutoka ama kubabuka, kuwasha kwa ngozi katikati ya vidole na kidole na mara nyingi kati ya kidole kidogo na kinachomfatilia. Wakati mwingine kisigino na nyayo huweza kuathirika na kuweka mabumbuza.

 

Kwenye kichwa, fangasi hawa huweka maduara yaliyo nyonyoka ngozi, yakiwa na ukurutu, ngozi kavu, na kuwasha. Maduara haya maarufu tunayaita mapunye, yanaweza kuwa mengi na kuungana kufanya duara moja kubwa. Mara nyingi sana fangasi wa kichwani huwapata sana watoto kuliko watu wazima.

 

Kwenye pachipachi za mapaja (jock itch). Fangasi hawa hukaa sehemu ya ndani ya mapaja karibu na sehemu za siri ama kuzungukia eneo hilo, lakini wanashambulia mapaja. Miongoni mwa dalili zao ni mapaja kufanya wekundu, kuwasha na hali inaweza kuwa mbaya mpaka ngozi ikababuka na hatimaye kufanya vidonda kwa kujikuna. Wanaweza kushambulia pia korodani na kufanya ibabuke, iwe nyekundu na kuweka vidonda.

 

Fangasi wa kwenye ndevu (tinea barbae). fangasi hawa wanashambulia maeneo ambayo ndevu zinapatikana kama kwenye kidevu na shavu. Dalili zao ni kuwasha kwa kidevu, shavu, na sehemu ya juu ya shingo. Fangasi hawa wanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha mapele yenye usaha kwenye eneo hili.

 

Huweza kuwapata wenye ndevu ama ambao wananyoa ndevu. Dalilizao  ni kama za fangasi wa maeneo mengine, kama eneo kuwa jekundu, kuwasha kuwa na madoamadoa na kunyonyoka kwa ndevu katika eneo lililo athirika.

 

Walio hatarini zaidi kupata fangasi hawa

Watu wote wanaweza kupata fangasi hawa wa mapunye. Lakini kuna watu wengine wapo hatarini zaidi. Na hii ni kutokana na shughuli zao wanazofanya, mazingira wanayoishi ama staili za maisha yao.

 

Namna ya kujilinda na mapunye

  1. Weka ngozi yako katika hali ya usafi
  2. Vaa viatu ambavyo vinaruhusu hewa kupita kwenye nyayo zako
  3. Usitembee miguu peku hasa kwenye maeneo yenye watu wengi
  4. Kata kucha zako ziwe fupi na ziweke katika hali ya usafi
  5. Badilisha soksi zako na nguo za ndani (chipi, boksa n.k) japo mara moja kwa siku
  6. Usichangie nguo zako na mtu mwingine
  7. Kama uanfanya kazi inayohitaji kugusana gusana kwa ngozi hakikisha unaoga mara kwa mara kwa siku.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 6646

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Dalili za mawe kwenye kibofu Cha mkono

Mawe ya kibofu ni mkusanyiko mgumu wa madini kwenye kibofu chako. Mawe kwenye kibofu hukua wakati mkojo kwenye kibofu chako unapokolea, na kusababisha madini katika mkojo wako kung'aa.

Soma Zaidi...
Dalili na sababu za mawe kwenye in yaani liver stone au intrahepatic stones

Katika post hii utakwend akujifunza kuhusu tatizo la kuwa na vijiwe kwenye ini vijiwe hivi hufahamika kama intrahepatic stones.

Soma Zaidi...
Maumivu, kizunguzungu, kichefuchefu na kutoka na damu ni dalili zamimba?

Je unapata dalili zisizoeleweka ni ni za mimba ama laa. Hapa nitakujuza hali baadhi ya wanawake zinazowatokea.

Soma Zaidi...
Aina za kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za kisukari

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri.

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa vipele kwenye midomo na sehemu za siri .Ni ugonjwa ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster

Soma Zaidi...
DALILI ZA MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kuwashwa, kutapika damu, moyo kuumwa, ukuaji hafifu, udhaifu na kuchoka

DALILI ZA MINYOO Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa coma

Coma ni hali ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu ambayo inaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali Jeraha la Kichwa, Kiharusi, Uvimbe kwenye ubongo, ulevi wa dawa za kulevya au pombe, au hata ugonjwa wa msingi,

Soma Zaidi...
Sababu za vidonda sugu vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za vidonda vya tumbo sugu

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisukari ambao husababisha kupoteza fahamu ( coma ya kisukari)..

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kisukari unaopelekea kukosa fahamu ni tatizo linalohatarisha maisha kisukari ambalo husababisha kupoteza fahamu. Ikiwa una kisukari, sukari ya juu ya damu (hyperglycemia) au sukari iliyopungua sana (hypoglyc

Soma Zaidi...
Bawasili usababishwa na nini?

Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.

Soma Zaidi...