picha

Dalili za minyoo na sababu zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake

Dalili za minyoo, sababu zake na kuiepuka minyoo.

 

 

Minyoo ni katika wadudu vimelea vinavyowapa shida watu wengi leo hii. Minyoo sio virusi wala bakteria kama ambavyo watu wengi wamekuwa wakidhania.minyoo ipo katika makundi meengi na huishi katika maeneo mbalimbali kwenye miili yetu ikiwemo tumbo, ini, utumbo, ubongo na kwenye damu na maeneo mengine. Dalili za minyoo hutofautiana sana kulingana na aina ya minyoo na wapi ipo. Lakini zipo dalili zenye kufanana kwa minyoo wote. Katika makala hii nitakwenda kukujuza baadhi ya dalili za minyoo katika mwili wako, pia tutaona sababu za kupata minyoo, wapi minyoo inapatikana na vipi tutaizuia:-

 

Utaweza kupata minyoo katika hali zifuatazo:-

1.kula kitu kisichooshwa kwema kwa maji yaliyo safi na salama

2.Kunywa maji ambayo si masafi na si salama

3.Kula nyama ambayo haikuiva vyema, ama nyama mbichi

4.Kutembea pekupeku kwenye ardhi yeye minyoo

5.Kula udongo,

6.Kinyesi cha wanyama na binadamu

 

 

DALILI ZA MINYOO

Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-

1.Kichefuchefu

2.Kukosa hamu ya kula

3.Maumivu ya tumbo

4.Kupungua uzito

5.Uchovu wa viungo

6.Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi

7.Kuona minyoo kwenye kinyesi.

8.Kuona damu kwenye kinyesi

9.Tumbo kujaa

 

Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-

 

1.minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:

A.Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo

B.Kuwa na alegi

C.Kuwa na homa

D.Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa

 

2.minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-

A.Kuwashwa

B.Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini

C.Kuwa na uchovu wa hali ya juu.

 

3.minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-

A.Kupata homa

B.Kuvimba kwa uso

C.Maumivu ya misuli na kuchoka

D.Maumivu ya kichwa

E.Kutokupenda kupigwa na mwanga

F.Matatizo katika macho (conjuctivist)

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3047

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 web hosting     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Dalili za jeraha kali kwenye ubongo

Posti hii inahusu zaidi dalili za jeraha kali kwenye ubongo, ni majeraha ambayo utokea kwenye ubongo pale ambapo mtu anapata ajali au amepigwa na kitu chochote kigumu kichwni, zifuatazo ni dalili za jeraha kali kwenye ubongo

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kichaa cha mbwa: Dalili na hatua za haraka.

Kichaa cha mbwa (Rabies) ni ugonjwa hatari wa virusi (Zoonotic disease) unaoambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu kupitia mate. Ugonjwa huu huathiri mfumo mkuu wa neva na, mara tu dalili zinapoanza kuonekana, huwa hauna tiba na husababisha kifo kwa asilimia karibu 100. Makala hii inaelezea utaratibu wa maambukizi, dalili za awali na za hatari, na hatua za dharura za kuokoa maisha pale mtu anapong'atwa na mnyama mwenye maambukizi.

Soma Zaidi...
Dalili za Kufunga kwa ulimi (tongue tie)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za Kufunga kwa ulimi (Tongue-tie) kuanzia Mtoto anavyo zalia mpaka navyokua ni hali inayotokea wakati wa kuzaliwa ambayo kitaalamu hujulikana kama ankyloglossia.

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo za mimba

​Wiki za kwanza za ujauzito ni kipindi cha mabadiliko makubwa ya ndani na nje ya mwili wa mwanamke. Makala hii inafafanua mabadiliko hayo ili kumsaidia mama kuelewa kinachoendelea na jinsi ya kukabiliana na hali hiyo kwa usalama.Utangulizi​Wakati mwingine, mabadiliko ya mwili huanza kujitokeza hata kabla hujapima na kupata majibu chanya ya mimba. Hii inatokana na msukosuko wa homoni unaolenga kutengeneza mazingira rafiki kwa ukuaji wa kiumbe kilichotungwa. Kuelewa dalili hizi ni muhimu ili uweze kujijali na kumpa mtoto wako nafasi nzuri zaidi ya ukuaji kuanzia siku ya kwanza.​Maudhui: Mabadiliko ya Mwili katika Wiki za Mwanzo​Katika kipindi hiki, mwili wako unafanya kazi kubwa kurekebisha mfumo wake:​Mabadiliko ya Homoni: Kiwango cha homoni za estrogen na progesterone hupanda kwa kasi ili kusaidia ujauzito, hali inayoweza kubadili hisia zako (mood swings).​Mabadiliko katika Matiti: Matiti yanaweza kuwa makubwa, mazito, na yenye maumivu mepesi kutokana na kuongezeka kwa mtiririko wa damu na kujiandaa kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa.​Mabadiliko ya Mfumo wa Chakula: Unaweza kuhisi kichefuchefu, hasa asubuhi, au kupata mabadiliko ya ladha (kuchukia vyakula fulani ulivyokuwa unapenda awali).​Uchovu: Mwili hutumia nishati nyingi katika wiki za mwanzo kuunda mfumo wa kondo la nyuma (placenta), hali inayokufanya uhisi uchovu na usingizi wa mara kwa mara.​Kukojoa Mara kwa Mara: Uterasi inapoanza kukua na shinikizo la damu kuongezeka, kibofu cha mkojo hupata shinikizo zaidi, jambo linalokufanya utake kwenda chooni mara kwa mara.​Fact Check: Je, mabadiliko haya ni hatari?​Ukweli: Mabadiliko mengi unayoyahisi ni ya kawaida kabisa na ni ishara kuwa mwili wako unakubali ujauzito. Hata hivyo, si kila mwanamke anapata dalili hizi zote.​Tahadhari: Ikiwa utapata dalili hizi, unapaswa kuonana na daktari mara moja:​Maumivu makali ya tumbo (upande mmoja au sehemu ya chini).​Kutokwa na damu nyingi ukeni (vaginal bleeding).​Homa kali au maumivu wakati wa kukojoa.​Kutapika sana kiasi cha kushindwa kuhifadhi maji mwilini.​Hitimisho​Mabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo ni ishara ya maajabu ya kimaumbile yanayotokea ndani yako. Ingawa baadhi ya hali hizi zinaweza kuwa kero, kumbuka kuwa ni za muda mfupi. Kula mlo kamili, kunywa maji ya kutosha, na kupumzika ipasavyo kutakusaidia kupitia kipindi hiki kwa urahisi zaidi. Usisahau kuhudhuria kliniki mapema ili kupata ushauri wa kitaalamu na ufuatiliaji wa ukuaji wa mtoto wako

Soma Zaidi...
Njia za Kuongeza Mbegu za Kiume

​Uzazi wa mwanaume unategemea kwa kiasi kikubwa ubora na wingi wa mbegu za kiume. Makala haya yanalenga kutoa mwongozo wa njia za asili na mabadiliko ya mtindo wa maisha yanayoweza kusaidia kuongeza uzalishaji na kuboresha ubora wa mbegu hizo.

Soma Zaidi...
Kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI

Soma Zaidi...