Dalili za minyoo na sababu zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake

Dalili za minyoo, sababu zake na kuiepuka minyoo.

 

 

Minyoo ni katika wadudu vimelea vinavyowapa shida watu wengi leo hii. Minyoo sio virusi wala bakteria kama ambavyo watu wengi wamekuwa wakidhania.minyoo ipo katika makundi meengi na huishi katika maeneo mbalimbali kwenye miili yetu ikiwemo tumbo, ini, utumbo, ubongo na kwenye damu na maeneo mengine. Dalili za minyoo hutofautiana sana kulingana na aina ya minyoo na wapi ipo. Lakini zipo dalili zenye kufanana kwa minyoo wote. Katika makala hii nitakwenda kukujuza baadhi ya dalili za minyoo katika mwili wako, pia tutaona sababu za kupata minyoo, wapi minyoo inapatikana na vipi tutaizuia:-

 

Utaweza kupata minyoo katika hali zifuatazo:-

1.kula kitu kisichooshwa kwema kwa maji yaliyo safi na salama

2.Kunywa maji ambayo si masafi na si salama

3.Kula nyama ambayo haikuiva vyema, ama nyama mbichi

4.Kutembea pekupeku kwenye ardhi yeye minyoo

5.Kula udongo,

6.Kinyesi cha wanyama na binadamu

 

 

DALILI ZA MINYOO

Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-

1.Kichefuchefu

2.Kukosa hamu ya kula

3.Maumivu ya tumbo

4.Kupungua uzito

5.Uchovu wa viungo

6.Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi

7.Kuona minyoo kwenye kinyesi.

8.Kuona damu kwenye kinyesi

9.Tumbo kujaa

 

Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-

 

1.minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:

A.Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo

B.Kuwa na alegi

C.Kuwa na homa

D.Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa

 

2.minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-

A.Kuwashwa

B.Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini

C.Kuwa na uchovu wa hali ya juu.

 

3.minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-

A.Kupata homa

B.Kuvimba kwa uso

C.Maumivu ya misuli na kuchoka

D.Maumivu ya kichwa

E.Kutokupenda kupigwa na mwanga

F.Matatizo katika macho (conjuctivist)

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2168

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Ninashida Kuna mtu anaumwa pressure Kila anap pima Iko juu il mwil aumuumi at kidg n dawa anatumia unawez kunisaidiaj

Kama unasumbuliwa na presha post hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakuoatia ushauri kutokana na swali alilouliza mdau wetu.

Soma Zaidi...
Ni bakteria gani husababisha ugonjwa wa pumu

Post hii inakwenda kujibu swali linalosema je ni bakteria aina gani husababisha igonjwa wa pumu.

Soma Zaidi...
Hatua za Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.

Posti hii inahusu zaidi hatua mbalimbali za Ugonjwa wa Ukimwi, kawaida Ugonjwa huu huwa na hatua kuu nne ila kila hatua huwa na sifa zake kwa hiyo tunapaswa kujua hatua za Ugonjwa huu na kujaribu kuzuia maambukizi yasisambae kabisa.

Soma Zaidi...
Sababu kuu za maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, Tumbo la ngiri na chango

Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, na tumbo la ngiri kwa wanaume, na tumbo la chango kwa wanawake

Soma Zaidi...
Maambukizi ya Kawaida ya zinaa (Chlamydia)

maambukizi ya kawaida ya zinaa (STI), Hujulikana Kama Chlamydia. Huenda usijue una Ugonjwa huu kwa sababu watu wengi hawapati dalili au ishara, kama vile maumivu ya sehemu za siri na kutokwa na uchafu kutoka kwa uke au uume. Maambukizi haya huathiri

Soma Zaidi...
Namna Maambukizi kwenye milija na ovari yanavyotokea

Post hii inahusu zaidi namna Maambukizi kwenye milija na ovari ambayo yanatokea,Mara nyingi usababisha na bakteria wanaoweza kuingia kupitia sehemu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Magonjwa ya moyo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu magonjwa ya moyo

Soma Zaidi...
Mbinu za kuzuia na kuepukana na maradhi ya uti wa mgongo

Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.

Soma Zaidi...
Je unaweza kupata ujauzito bila ya kupata hedhi miezi 9 baada ya kujifunguwa?

Baada ya kujifungua mwili wa mwanamke huwa na mabadiliko tofauti na siku za nyuma. Kwa mfano hatapatavtena hedhi, hatoweza kupata ujauzito kwa muda wa mwezi ama zaidi. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...