Dalili za minyoo na sababu zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake

Dalili za minyoo, sababu zake na kuiepuka minyoo.

 

 

Minyoo ni katika wadudu vimelea vinavyowapa shida watu wengi leo hii. Minyoo sio virusi wala bakteria kama ambavyo watu wengi wamekuwa wakidhania.minyoo ipo katika makundi meengi na huishi katika maeneo mbalimbali kwenye miili yetu ikiwemo tumbo, ini, utumbo, ubongo na kwenye damu na maeneo mengine. Dalili za minyoo hutofautiana sana kulingana na aina ya minyoo na wapi ipo. Lakini zipo dalili zenye kufanana kwa minyoo wote. Katika makala hii nitakwenda kukujuza baadhi ya dalili za minyoo katika mwili wako, pia tutaona sababu za kupata minyoo, wapi minyoo inapatikana na vipi tutaizuia:-

 

Utaweza kupata minyoo katika hali zifuatazo:-

1.kula kitu kisichooshwa kwema kwa maji yaliyo safi na salama

2.Kunywa maji ambayo si masafi na si salama

3.Kula nyama ambayo haikuiva vyema, ama nyama mbichi

4.Kutembea pekupeku kwenye ardhi yeye minyoo

5.Kula udongo,

6.Kinyesi cha wanyama na binadamu

 

 

DALILI ZA MINYOO

Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-

1.Kichefuchefu

2.Kukosa hamu ya kula

3.Maumivu ya tumbo

4.Kupungua uzito

5.Uchovu wa viungo

6.Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi

7.Kuona minyoo kwenye kinyesi.

8.Kuona damu kwenye kinyesi

9.Tumbo kujaa

 

Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-

 

1.minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:

A.Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo

B.Kuwa na alegi

C.Kuwa na homa

D.Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa

 

2.minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-

A.Kuwashwa

B.Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini

C.Kuwa na uchovu wa hali ya juu.

 

3.minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-

A.Kupata homa

B.Kuvimba kwa uso

C.Maumivu ya misuli na kuchoka

D.Maumivu ya kichwa

E.Kutokupenda kupigwa na mwanga

F.Matatizo katika macho (conjuctivist)



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-03     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1489


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Samaani nilikuwa nauriza ninasumburiwa na fanga ya mdomoni naomba ushauri
Fangasi mdomoni wanaweza kuwa tatizo endapo hawatatibiwa mapema. Wanaweza kuongeza majeraha kwenye kinywa. Soma Zaidi...

Dalili za kifua kikuu (tuberculosis)
Kifua kikuu ni ugonjwa sugu wa kuambukiza na anuwai ya magonjwa ya kiafya yanayosababishwa na Mycobacterium tuberculosis complex. Kwa binadamu sababu ya kawaida ni Mycobacterium tuberculosis. Soma Zaidi...

Njia za kuangalia sehemu yenye maumivu
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia sehemu yenye maumivu, hili kugundua mahali mtu anaumia ushirikiano mkubwa unahitajika kati ya mgonjwa na mhudumu. Soma Zaidi...

Dalili za upotevu wa kusikia
posti hii inazungumzia kuhusiana na Upotevu wa kusikia'unaotokea hatua kwa hatua kadri umri unavyozeeka (presbycusis) ni jambo la kawaida. T Kwa wale walio na umri wa zaidi ya miaka 75, idadi ya watu walio na' upotezaji wa kusikia'inakaribia 1 kati y Soma Zaidi...

Madhara ya kutotibu ugonjwa wa makende kushindwa kushuka
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya makende kushindwa t, hiki ni tatizo na huleta madhara Soma Zaidi...

Saratani ya tishu zinazounda Damu mwilini (leukemia)
Post hii inaelezea kuhusiana na'Saratani'ya tishu zinazounda damu mwilini, ikijumuisha uboho na mfumo wa limfu.ugonjwa huu kitaalamu huitwa leukemia. Soma Zaidi...

Fahamu Ugonjwa wa uchovu sugu.
Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa uchovu sugu ni ugonjwa tata unaoonyeshwa na uchovu mwingi ambao hauwezi kuelezewa na hali yoyote ya matibabu. Uchovu unaweza kuwa mbaya zaidi kwa shughuli za kimwili au kiakili, lakini haiboresha kwa kupumzika Soma Zaidi...

Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu
kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako Soma Zaidi...

Nini husababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu kwa wanawake na wanaume
Somo hili linakwenda kukueleza vitu vinavyosababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu Soma Zaidi...

Nini chanzo cha malaria
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu chanzo cha ugonjwa wa malaria Soma Zaidi...

Mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu
Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu Soma Zaidi...

Dalili za mtoto Mwenye UTI
Posti hii inahusu zaidi dalili za mtoto Mwenye UTI,ni dalili ambazo uwapata watoto wadogo chini ya umri wa miaka mitano. Soma Zaidi...