picha

Dalili za minyoo na sababu zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake

Dalili za minyoo, sababu zake na kuiepuka minyoo.

 

 

Minyoo ni katika wadudu vimelea vinavyowapa shida watu wengi leo hii. Minyoo sio virusi wala bakteria kama ambavyo watu wengi wamekuwa wakidhania.minyoo ipo katika makundi meengi na huishi katika maeneo mbalimbali kwenye miili yetu ikiwemo tumbo, ini, utumbo, ubongo na kwenye damu na maeneo mengine. Dalili za minyoo hutofautiana sana kulingana na aina ya minyoo na wapi ipo. Lakini zipo dalili zenye kufanana kwa minyoo wote. Katika makala hii nitakwenda kukujuza baadhi ya dalili za minyoo katika mwili wako, pia tutaona sababu za kupata minyoo, wapi minyoo inapatikana na vipi tutaizuia:-

 

Utaweza kupata minyoo katika hali zifuatazo:-

1.kula kitu kisichooshwa kwema kwa maji yaliyo safi na salama

2.Kunywa maji ambayo si masafi na si salama

3.Kula nyama ambayo haikuiva vyema, ama nyama mbichi

4.Kutembea pekupeku kwenye ardhi yeye minyoo

5.Kula udongo,

6.Kinyesi cha wanyama na binadamu

 

 

DALILI ZA MINYOO

Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-

1.Kichefuchefu

2.Kukosa hamu ya kula

3.Maumivu ya tumbo

4.Kupungua uzito

5.Uchovu wa viungo

6.Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi

7.Kuona minyoo kwenye kinyesi.

8.Kuona damu kwenye kinyesi

9.Tumbo kujaa

 

Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-

 

1.minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:

A.Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo

B.Kuwa na alegi

C.Kuwa na homa

D.Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa

 

2.minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-

A.Kuwashwa

B.Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini

C.Kuwa na uchovu wa hali ya juu.

 

3.minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-

A.Kupata homa

B.Kuvimba kwa uso

C.Maumivu ya misuli na kuchoka

D.Maumivu ya kichwa

E.Kutokupenda kupigwa na mwanga

F.Matatizo katika macho (conjuctivist)

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2923

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 web hosting     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Dalili za saratani ya koo

Saratani ya Koo inarejelea Vivimbe vya Saratani vinavyotokea kwenye koo lako (koromeo), sanduku la sauti (larynx) au tonsils.

Soma Zaidi...
Matatizo yanayosababisha mshtuko wa moyo.

Mshtuko wa moyo hutokea wakati mtiririko wa damu kwa moyo umezuiwa, mara nyingi kwa mkusanyiko wa mafuta, cholesterol na vitu vingine, ambayo huunda plaque katika mishipa inayolisha moyo (mishipa ya moyo). Mtiririko wa damu ulioingiliwa unaweza kuharibu

Soma Zaidi...
Dalili za saratani (cancer)

Posti hii inahusu zaidi dalili za kansa, ni dalili ambazo utokea kwa mtu Mwenye tatizo la ugonjwa wa Kansa ingawa sio lazima dalili hizi kutokea tukadhani kuwa ni Kansa Ila zilizonyingi huwa ni kweli dalili za kansa.

Soma Zaidi...
Mashambulizi ya hofu (Panic Attacks): Hatua za kuchukua yanapotokea.

​Mashambulizi ya hofu (panic attacks) ni hali ya ghafla ya woga mkali inayoweza kuambatana na dalili za kimwili zinazotisha. Makala haya yanafafanua kwa kina nini ni mashambulizi ya hofu, hatua za haraka za kuchukua yanapotokea, na umuhimu wa kutafuta msaada wa kitaalamu ili kudhibiti afya ya akili kwa muda mrefu.

Soma Zaidi...
Sababu za miguu kufa ganzi.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya mfumo wa mkojo (UTI): Dalili zake kwa wanaume na wanawake.

​Maambukizi ya mfumo wa mkojo (Urinary Tract Infection - UTI) hutokea wakati bakteria wanapoingia kwenye mfumo wa mkojo na kusababisha maambukizi. Mfumo huu unajumuisha figo, mirija ya mkojo (ureters), kibofu cha mkojo, na mrija wa kutolea mkojo (urethra). Ingawa wanawake wako katika hatari zaidi ya kupata UTI kutokana na maumbile ya mwili wao, wanaume pia wanaweza kupata maambukizi haya. Makala haya yanafafanua dalili za kawaida na wakati wa kutafuta msaada.

Soma Zaidi...