Dalili za minyoo na sababu zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake

Dalili za minyoo, sababu zake na kuiepuka minyoo.

 

 

Minyoo ni katika wadudu vimelea vinavyowapa shida watu wengi leo hii. Minyoo sio virusi wala bakteria kama ambavyo watu wengi wamekuwa wakidhania.minyoo ipo katika makundi meengi na huishi katika maeneo mbalimbali kwenye miili yetu ikiwemo tumbo, ini, utumbo, ubongo na kwenye damu na maeneo mengine. Dalili za minyoo hutofautiana sana kulingana na aina ya minyoo na wapi ipo. Lakini zipo dalili zenye kufanana kwa minyoo wote. Katika makala hii nitakwenda kukujuza baadhi ya dalili za minyoo katika mwili wako, pia tutaona sababu za kupata minyoo, wapi minyoo inapatikana na vipi tutaizuia:-

 

Utaweza kupata minyoo katika hali zifuatazo:-

1.kula kitu kisichooshwa kwema kwa maji yaliyo safi na salama

2.Kunywa maji ambayo si masafi na si salama

3.Kula nyama ambayo haikuiva vyema, ama nyama mbichi

4.Kutembea pekupeku kwenye ardhi yeye minyoo

5.Kula udongo,

6.Kinyesi cha wanyama na binadamu

 

 

DALILI ZA MINYOO

Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-

1.Kichefuchefu

2.Kukosa hamu ya kula

3.Maumivu ya tumbo

4.Kupungua uzito

5.Uchovu wa viungo

6.Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi

7.Kuona minyoo kwenye kinyesi.

8.Kuona damu kwenye kinyesi

9.Tumbo kujaa

 

Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-

 

1.minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:

A.Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo

B.Kuwa na alegi

C.Kuwa na homa

D.Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa

 

2.minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-

A.Kuwashwa

B.Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini

C.Kuwa na uchovu wa hali ya juu.

 

3.minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-

A.Kupata homa

B.Kuvimba kwa uso

C.Maumivu ya misuli na kuchoka

D.Maumivu ya kichwa

E.Kutokupenda kupigwa na mwanga

F.Matatizo katika macho (conjuctivist)

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2061

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mambo yanayosababisha kiuno au mgongo kuwa na maumivu

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kusababishwa mgongo wAko au kiuno kwa na maumivu, Mgongo ukiwa na maumivu makali Sana yanaweza kusababishwa shida kubwa ata utakapokaa au ukilala au ukitumia bado maumivu yanakuwepo.

Soma Zaidi...
Dalili zake mtoto mwenye Ugonjwa wa Maambukizi kwenye koo

Pisti hii inahusu zaidi dalili za mtoto mwenye Maambukizi ya ugonjwa wa Dondakoo, tunajua wazi kuwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wadogo ambao wako chini ya miaka mitano, kwa hiyo zifuatazo ni baadhi ya Dalili zinazoweza kujitokeza kwa watoto hawa.

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUISHI NA VIDONDA VYA TUMBO

NAMNA YA KUISHI NA VIDONDA VYA TUMBO Unaweza kupata nafuu kutoka kwa maumivu ya kidonda cha tumbo ikiwa utafata taratibu za kiafya kama:- 1.

Soma Zaidi...
Dalili za Ukimwi

Makala hii itaeleza dalili za ukimwi, dalili za VVU, magonjwa nyemelezi na matumizi ya ARV

Soma Zaidi...
Tufanyeje ili kuepuka kuaribika kwa figo?

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia kuaribika kwa figo, hizi ni njia zinazotumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuaribika kwa figo na hasa wale ambao hawajapata tatizo hili wazitumie ili tuone kama tutaweza kupunguza tatizo hili.

Soma Zaidi...
Dalili kuu za Malaria mwilini

Malaria husababishwa na vijidudu vidogo parasite wanaojulikana kama plasmodium. Vijidudu hivi hubebwa na mbu aina ya anophelesi. Kuna ina nyingi za plasmodium lakini aina 5 tu ndizo husababisha malaria

Soma Zaidi...
Dalili za maambukizi kwenye ovari

Posti hii inahusu zaidi dalili za maambukizi kwenye ovari, ni maambukizi ambayo hutokea kwenye ovari na kusababisha matatizo makubwa kama mgonjwa haujatibiwa mapema.

Soma Zaidi...
Matibabu ya fangasi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu matibabu ya fangasi

Soma Zaidi...
Maambukizi kwenye uume

Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye uume, maambukizi hata utokea kwenye kichwa Cha uume kwa kitaalamu huitwa Balanitis, zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
Mate yanaweza kuambukiza ukimwi

Jibu ni hapana, matehayawezi kuambukiza HIV. Lakini swali unalotakiwa kulijibu je ni kwa nini mate hayaambukizi. Makala hii itakwend akukupa majibu haya

Soma Zaidi...