Haki za kijamii za mwanamke katika uislamu

Haki za kijamii za mwanamke katika uislamu

Haki za kijamii
Pamoja na haki za kiuchumi, Uislam unampa mwanamke haki za kijamii zifuatazo:



Kwanza, mwanamke amepewa uhuru kamili wa kuolewa na mwanamume ampendaye. Ndoa ya Kiislamu haisihi iwapo mwanamke atalazimishwa kuolewa kinyume na ridhaa yake. Vile vile hapana ruhusa ya kumkataza mwanamke asiolewe na mwanamume ampendaye ndani ya mipaka ya sheria ya Kiislamu.



Pili, mwanamke amepewa haki zote za kisheria za kumuacha mumewe ambaye amekosa nguvu za kiume (impotent), ambaye ni katili kwake na ambaye anamchukia.



Tatu, mwanamume ameamrishwa kutumia madaraka aliyopewa juu ya mkewe kwa huruma na upendo. Kama Qur'an inavyoagiza:
"... basi kaeni nao kwa wema ..." (4: 19). Wala msisahau kufanyiana Ihsani baina yenu ..." (2:237).



Na Mtume (s.a.w) amesema: 'Wabora wenu ni wale walio wema kwa wake zao na watu wao (katika familia)". Kama mwanamume atatumia vibaya madaraka yake, mwanamke ana kila haki ya kukiendea chombo cha sheria na kumshitakia mumewe ambaye hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.


Nne, wanawake wajane na waliotengana na waume zao wanahaki na uhuru kamili wa kuolewa tena. Haki hii haijapatikana kwa jamii nyingi ulimwenguni.
Tano, kuna usawa kamili kati ya wanaume na wanawake kwa upande wa sheria za madai na jinai. Sheria ya Kiislamu haibagui wala haipendelei mwanamume au mwanamke katika kulinda haki za watu na haki zajamii kwa ujumla. Kwa mfano hukumu ya Kiislamu kwa mwizi ni kukatwa mkono, awe mwanamume au mwanamke kama inavyobainishwa katika Qur'an;


Na mwizi mwanamume na mwizi mwanamke, ikateni mikono yao, malipo ya yale waliyoyachuma. Ndiyo adhabu itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye He/dma (5:38).



Kuhusu adhabu ya wazinifu tunafahamishwa: Mzinfu mwanamke na mzinfu mwanamume mpigeni kila mmoja katika wao mj/eledi mia. Wala isiwashikeni kwa ajili yao huruma katika kupitisha hukumu hii ya Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Na lishuhudie adhabu hiyo kundi la Waislam. (24:2).
Sita, vile vile wanawake nao kama wanaume wanaruhusiwa kutoa ushahidi mahakamani au pale ushahidi wao unapohitajika. Bali katika kipengele hiki itatubidi tuwe wazi kwa kujibu maswali mbali mbali yanayoweza kuulizwa kama vile:


Kwa nini wanatakiwa mashahidi wawili wanawake badala ya shahidi mmoja mwanamume? Je, hii ma maana kuwa Uislamu unamhesabu mwanamke kuwa ni nusu ya mwanamume? La! Hasha. Kama katika suala Ia urithi, ukitazama kwa sura ya nje unaweza kudhani kuwa mwanamke ameonelewa na mwanamume kapendelewa kwa mwanamume kupewa mara mbili ya mwanamke. Hivyo hivyo katika suala Ia ushahidi, kwa kutakiwa wanawake wawili haina maana kuwa Uislamu unamuona mwanamke kuwa ni nusu ya mwanamume. Lau ingekuwa hivyo, Uislam ungeweza kuukataa ushahidi wake moja kwa moja. Na katika karne ya 7A.D iliposhuka Qur'an hata huko kuukubali ushahidi wa mwanamke kulionekana ni kioja na kuruka mipaka.


Na mshuhudishe mashahidi wawili katika watu wenu wanaume. Lakini ikiwa hakuna wanaume wawili, basi mwanamume mmoja na wanawake wawili; katika wale mnaowakubali kuwa mashahidi. Ili kama mmoja wao akipotea, mmoja wao amkumbushe mwingine "(2:282).



Ushahidi unaotajwa katika aya hii unahusiana na mikataba ya mambo ya fedha. Mashahdi wanatakiwa wawe ama wanaume wawili au mwanamume mmoja na wanawake wawili. Na sababu ya kuwaweka wanawake wawili imetajwa nayo ni kuwa akisahau mmoja mwenzake atamkumbusha. Swali Ia kujiuliza hapa ni kuwa kwa nini ihofiwe kuwa mwanamke ndiye atakayesahau na siyo mwanamume? Tatizo lililopo hapa kwa kiasi fulani linatokana na kasoro za kutafsiri neno "tadhila" kama kusahau. Neno "tadhila" halina maana ya kutokuwa na kumbukumbu (memory). Kwani mara nyingi wanawake hukumbuka zaidi kumbukumbu zao za kuzaliwa kuliko hata wanaume. Katika Uislam mwanamke ambaye kwa kawaida atakuwa anatimiza majukumu yake kama mke au mama aweza kujishughulisha na hayo kiasi Cha kumfanya asiwe hadhiri sana wakati wa majadiliano yanayohusu kuandikiana mikataba ya masuala ya fedha, masuala ambayo hahusiki nayo mara kwa mara.


Hii ni kwa kawaida, lakini haina maana kuwa kila mwanamke lazima atakuwa hivyo. Hata hivyo kwa sababu lengo Ia sheria ni kulinda haki za watu, sheria imeweka hadhri hiyo iii kuhakikisha kuwa haki za watu zinahifadhiwa. Na lengo si kumdhalilisha mwanamke. Kwani Iau ushahidi wa mwanamke ungekuwa unakataliwa tu kwa sababu mwanamke ni kiumbe dhalili basi Hadith zilizopokewa kutoka kwa wanawake zingekataliwa. Lakini Hadith zilizopokewa kutoka kwa Bibi Aisha kwa mfano ni sehemu ya msingi wa sheria yenyewe. Ni upi ushahidi mzito zaidi, wa kupokea Hadith au wa kuandikishiana mikataba ya pesa? Yote hayo yanaonesha kuwa lengo ni kuhifadhi haki za watu zisipotee kwa sababu ya kughafilika na siyo kumdunisha mwanamke.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 678

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Je ni nani mwenye haki ya kutaliki

Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Dhana ya kumiliki raslimali katika uislamu

Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu.

Soma Zaidi...
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?

Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga?

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu

Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii.

Soma Zaidi...
Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu

Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha

Soma Zaidi...
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
kuletewa ujumbe

(c)Kuletewa Ujumbe na Malaika kutoka kwa Allah (s.

Soma Zaidi...