image

Haki za kijamii za mwanamke katika uislamu

Haki za kijamii za mwanamke katika uislamu

Haki za kijamii
Pamoja na haki za kiuchumi, Uislam unampa mwanamke haki za kijamii zifuatazo:



Kwanza, mwanamke amepewa uhuru kamili wa kuolewa na mwanamume ampendaye. Ndoa ya Kiislamu haisihi iwapo mwanamke atalazimishwa kuolewa kinyume na ridhaa yake. Vile vile hapana ruhusa ya kumkataza mwanamke asiolewe na mwanamume ampendaye ndani ya mipaka ya sheria ya Kiislamu.



Pili, mwanamke amepewa haki zote za kisheria za kumuacha mumewe ambaye amekosa nguvu za kiume (impotent), ambaye ni katili kwake na ambaye anamchukia.



Tatu, mwanamume ameamrishwa kutumia madaraka aliyopewa juu ya mkewe kwa huruma na upendo. Kama Qur'an inavyoagiza:
"... basi kaeni nao kwa wema ..." (4: 19). Wala msisahau kufanyiana Ihsani baina yenu ..." (2:237).



Na Mtume (s.a.w) amesema: 'Wabora wenu ni wale walio wema kwa wake zao na watu wao (katika familia)". Kama mwanamume atatumia vibaya madaraka yake, mwanamke ana kila haki ya kukiendea chombo cha sheria na kumshitakia mumewe ambaye hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.


Nne, wanawake wajane na waliotengana na waume zao wanahaki na uhuru kamili wa kuolewa tena. Haki hii haijapatikana kwa jamii nyingi ulimwenguni.
Tano, kuna usawa kamili kati ya wanaume na wanawake kwa upande wa sheria za madai na jinai. Sheria ya Kiislamu haibagui wala haipendelei mwanamume au mwanamke katika kulinda haki za watu na haki zajamii kwa ujumla. Kwa mfano hukumu ya Kiislamu kwa mwizi ni kukatwa mkono, awe mwanamume au mwanamke kama inavyobainishwa katika Qur'an;


Na mwizi mwanamume na mwizi mwanamke, ikateni mikono yao, malipo ya yale waliyoyachuma. Ndiyo adhabu itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye He/dma (5:38).



Kuhusu adhabu ya wazinifu tunafahamishwa: Mzinfu mwanamke na mzinfu mwanamume mpigeni kila mmoja katika wao mj/eledi mia. Wala isiwashikeni kwa ajili yao huruma katika kupitisha hukumu hii ya Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Na lishuhudie adhabu hiyo kundi la Waislam. (24:2).
Sita, vile vile wanawake nao kama wanaume wanaruhusiwa kutoa ushahidi mahakamani au pale ushahidi wao unapohitajika. Bali katika kipengele hiki itatubidi tuwe wazi kwa kujibu maswali mbali mbali yanayoweza kuulizwa kama vile:


Kwa nini wanatakiwa mashahidi wawili wanawake badala ya shahidi mmoja mwanamume? Je, hii ma maana kuwa Uislamu unamhesabu mwanamke kuwa ni nusu ya mwanamume? La! Hasha. Kama katika suala Ia urithi, ukitazama kwa sura ya nje unaweza kudhani kuwa mwanamke ameonelewa na mwanamume kapendelewa kwa mwanamume kupewa mara mbili ya mwanamke. Hivyo hivyo katika suala Ia ushahidi, kwa kutakiwa wanawake wawili haina maana kuwa Uislamu unamuona mwanamke kuwa ni nusu ya mwanamume. Lau ingekuwa hivyo, Uislam ungeweza kuukataa ushahidi wake moja kwa moja. Na katika karne ya 7A.D iliposhuka Qur'an hata huko kuukubali ushahidi wa mwanamke kulionekana ni kioja na kuruka mipaka.


Na mshuhudishe mashahidi wawili katika watu wenu wanaume. Lakini ikiwa hakuna wanaume wawili, basi mwanamume mmoja na wanawake wawili; katika wale mnaowakubali kuwa mashahidi. Ili kama mmoja wao akipotea, mmoja wao amkumbushe mwingine "(2:282).



Ushahidi unaotajwa katika aya hii unahusiana na mikataba ya mambo ya fedha. Mashahdi wanatakiwa wawe ama wanaume wawili au mwanamume mmoja na wanawake wawili. Na sababu ya kuwaweka wanawake wawili imetajwa nayo ni kuwa akisahau mmoja mwenzake atamkumbusha. Swali Ia kujiuliza hapa ni kuwa kwa nini ihofiwe kuwa mwanamke ndiye atakayesahau na siyo mwanamume? Tatizo lililopo hapa kwa kiasi fulani linatokana na kasoro za kutafsiri neno "tadhila" kama kusahau. Neno "tadhila" halina maana ya kutokuwa na kumbukumbu (memory). Kwani mara nyingi wanawake hukumbuka zaidi kumbukumbu zao za kuzaliwa kuliko hata wanaume. Katika Uislam mwanamke ambaye kwa kawaida atakuwa anatimiza majukumu yake kama mke au mama aweza kujishughulisha na hayo kiasi Cha kumfanya asiwe hadhiri sana wakati wa majadiliano yanayohusu kuandikiana mikataba ya masuala ya fedha, masuala ambayo hahusiki nayo mara kwa mara.


Hii ni kwa kawaida, lakini haina maana kuwa kila mwanamke lazima atakuwa hivyo. Hata hivyo kwa sababu lengo Ia sheria ni kulinda haki za watu, sheria imeweka hadhri hiyo iii kuhakikisha kuwa haki za watu zinahifadhiwa. Na lengo si kumdhalilisha mwanamke. Kwani Iau ushahidi wa mwanamke ungekuwa unakataliwa tu kwa sababu mwanamke ni kiumbe dhalili basi Hadith zilizopokewa kutoka kwa wanawake zingekataliwa. Lakini Hadith zilizopokewa kutoka kwa Bibi Aisha kwa mfano ni sehemu ya msingi wa sheria yenyewe. Ni upi ushahidi mzito zaidi, wa kupokea Hadith au wa kuandikishiana mikataba ya pesa? Yote hayo yanaonesha kuwa lengo ni kuhifadhi haki za watu zisipotee kwa sababu ya kughafilika na siyo kumdunisha mwanamke.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 230


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga
Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga. Soma Zaidi...

nguzo za uislamu: Kutoa zaka, lengo la kutoa zaka na faida zake
Kutoa Zakat. Soma Zaidi...

Mgawanyiko katika kuitumia mali unayomiliki
Unajuwa namna ambavyo matumizi ya mali yako, yanavyogawanywa? Jifunze hapa mgawanyiko wa mali yako. Soma Zaidi...

Uzuri wa Benki za kiislamu
Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine? Soma Zaidi...

Haki za raia katika dola ya kiislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Swala ya jamaa na mnamna ya kuswali swala ya jamaa, nyumbni, msikitini na kwa wanawake
Soma Zaidi...

Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu
Maana: ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa baina ya mume na mke mbele ya mashahidi wawili kwa kuzingatia sheria ya Kiislamu. Soma Zaidi...

Sanda ya mtoto
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu
Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa. Soma Zaidi...

Mifumo ya benki ya kiislamu.
Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha Soma Zaidi...

Misingi ya fiqh
Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu. Soma Zaidi...

Hukumu na sherei zinazohusu ajira na kazi katika uislamu
Wajibu wa KufanyakaziUislamu siyo tu unawahimiza watu kufanya kazi na kutokuwa wavivu bali kufanya kazi ni Ibada. Soma Zaidi...