picha

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA TUNDA PERA

Pera ni tunda bora lakini pia ni dawa, tambua umuhimu wa tunda hili kiafya

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA TUNDA PERA

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA TUNDA PERA

Pera ni katika matunda yanayopatikana maeneo mengi duniani. Tunda hili ni katika matunda yenye kutia afya zaidi katika miili yetu hasa kwa wale wenye maradhi sugu. Tunda hili hutumika mapaka majani yeke na kuleta faida nyingi sana. Hata wazee wetu wa zamani walikuwa wakitumia mmea huu kwa ajili ya tiba asili. Sasa hebu tuanze kuziona faida hizo:-

 

  1. pera huweza kushusha kiwango cha sukari kwenye damu. Ijapokuwa tunda hili lina utamu lakini ni katika matunda ambayo ni mujarabu kwa kushusha kiwango cha sukari. Hii ni habari njema kwa wenye kisukari na wale wenye tatizo la homoni ya insulin. Hapa tunazungumzia majani ya mpera ni si tunda lenyewe.

 

Katika tafiti iliyofanyiwa watu 19 imethibitisha kuwa kunywa majimaji yatokanayo na majani ya mpera husaidia katika kushusha kiwango cha sukari na athari hii huweza kuendelea mpaka masaa mawili. Tafiti nyingine aliyofanyiwa watu 20 wenye aina ya kisukari type 2 diabetes waliligundulika kuwa kunywa majani ya mpera kumeshusha sukari kwa asilimia 10%.

 

  1. Pera husaidia katika kuimarisha na kulinda afya ya moyo. Wataalamu wa afya wanatueleza kuwa pera lina mitamini vingi pamoja na antioxdant nyingi. Ambapo kwa pamoja vitu hivi husaidia katika kulinda moyo usiharibiwe na mionz na mambo mengine.

 

Pia kiwango cha madini ya potassium (chumvi) iliyomo kwenye pera pamoja na kambakamba zilizomo kwenye pera husaidia katika kuimarisha afya ya moyo. Pia ulaji wa mapera unaweza kuondoa cholesterol zilizo mbaya (LDL cholesterol) na kuongeza cholesterol nzuri). Hivyo hupunguza nafasi ya kupata maradhi ya shinikizo la damu la juu yaani presha ya kupanda na kupata kiharusi yaani kupalalaizi. (stroke).

 

  1. Husaidia kupunguza maumivu ya tumbo la chango kwa wanawake. Wanawake wengi wanapata maumivu makali wakati wa siku zao. Tafiti zinaonesha kuwa kunywa majani ya mpera husaidia katika kupunguza maumivu haya.

 

Tafiti iliyofanyiwa wanawake 197 ambao huwa wanapata maumivu wakati wa kupata sikuzao, tafiti imeonesha kuwa unywaji wa miligram 6 za maji ya majani ya mpera husaidia kupunguza maumivu haya. Pia utafiti zaidi umeonesha kuwa majani ya mpera husaidi kupunguza maumivu haya mara dufu tofauti na kutumia dawa za kupunguza maumivu. Pia tafiti zinaonesha kuwa majani ya mpera hupunguza maumivu wakati wa kukojoa kwa wale wanaopata maumivu haya.

 

  1. Husaidia katika mmeng’enyo wa chakula. Pera ni katika matunda yenye kambakamba kitaalamu hufahamika kama fiber. Hizi husaidia katika kuboresha mchakato wa kukimeng’enya chakula uende vyema. Hivyo husaidia kutokupata tatizo la kutokupata choo. Tafiti zinaonesha kuwa pera moja hukusanya asilimia 12% ya fiber zinazohitajika mwilini kwa siku.

 

Pia majani ya pera yakitengenezwa majimaji yake husaidia katika kuboresha afya ya mfumo mzima wa mmeng’enyo wa chakula. Kwa wale wenye tatizo la kuharisha majani ya mpera ni mujarabu sana katika kuondoa ama kupunguza tatizo. Pia kuna tafiti nyingi zinaonesha kuwa pera husaidia katika kuuwa vijidudu vibaya ndani ya matumbo yetu.

 

  1. Husaidia katika kupunguza uzito. Wataalamu wa afya wanatueleza kuwa pera husaidia katika kupunguza uzito. Ni kuwa pera lina calory chache na lina fiber nyingi. Kwa pamoja hizi husaidia katika kumfanya mtu ahisi kushiba mapema na hivyo kumpunguzia kula sana. Hali hii husaidia katika kupunguza uzito mwili.

 

  1. Husaidia kulinda mwili dhidi ya maradhi ya saratani (cancer). Tafiti zinaonesha kuwa pera lina anticancer effect hizi hisaidi sana miili yetu kuzuia uwezekano wa kupata maradhi ya saratani au kansa, pia husaidia kuuwa seli za saratani ndani ya miili yetu.

 

  1. Huboresha mfumo wa kinga mwilini. Pera ni katika matunda yenye vitamini C vingi. Na ijulikane kuwa vitamin C ni katika vitamini ambavyo husaidia kuupa nguvu mwili kwa ajili ya kupambana na maradhi.

 

  1. Huboresha afya ya ngozi. Kwa afya njema ya ngozi, pera ni mujarabu katika kuhakikisha ngozi inabakia salama muda wote. Kuondoa mikunyomikunjo kwenye ngozi, na kuuwa baadhi ya bakteria kwenye ngozi na kuondoa chunjua.

 



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 5223

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 ai web app    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Faida za kula Nyanya

Nyanya ni katika viungio vya mboga, kuna faida kubwa za kiafya katika nyanya

Soma Zaidi...
Vinywaji vyakula salama kwa mwenye Presha ya kupanda

Je umesha wahi kujiuliza kuwa ni vinywaji vipi mwenye presha ya kupanda anafaha kutumia, Unadhani ni maji, mvinyo wa pombe, chai na kahawa. Bila shaka ungependa kujuwa zaidi kuhusu jambo hili. Makala hii ni kwa ajili yako

Soma Zaidi...
Vyakula salama na vilivyo hatari kwa mwenye kisukari, na vipi atajikinga na kisukari

Makala hii inakwenda kukupa elimu juu ya vyakula na vinywaji vilivyo salama kwa mtu mwenye kisukari, na ni vyakula vipi ni hatari kwa mwenye kisukari. Pia utajifunza njia za kujilinda na kupata kisukari.

Soma Zaidi...
Faida za kula magimbi (taro roots)

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula magimbi

Soma Zaidi...
Vyakula salama kwa mwenye kisukari

Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya vyakula salama kwa mwenye kisukari

Soma Zaidi...
Faida za kula mayai

Posti hii inahusu zaidi faida anazozipata mtu anayekula mayai hasa wakati wa kifua kinywa, tunajua wazi kuwa mayai yana kiwango kikubwa cha protini pamoja na hayo kuna faida nyingi za kutumia mayai hasa wakati wa asubuhi kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Vyakula vya vitamin E

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya vitamin E

Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
VYANZO VYA VYAKULA VYA VITAMINI NA FAIDA ZAKE

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
utaratibu wa lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...