Uthibitisho Kuwa Qur’an ni Neno la Mwenyezi Mungu (s.w)

Uthibitisho Kuwa Qur'an ni Neno la Mwenyezi Mungu (s.w)

Uthibitisho Kuwa Qur'an ni Neno la Mwenyezi Mungu (s.w)

a) Uthibitisho Kutokana na Qur'an Yenyewe

i. Kutojua kusoma na kuandika kwa Mtume Muhammad (s.a.w)

- Mtume (s.a.w) kutokujua kusoma na kuandika ni ushahidi tosha kuwa

asingeweza kutunga Kitabu mfano wa Qur'an. Rejea Qur'an (7:158), (29:48)


ii. Qur'an yenyewe inajieleza kuwa ni Kitabu cha Allah (s.w) kama ifuatavyo; 'Uteremsho wa Kitabu hiki umetoka kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye Nguvu na Mwenye Hikima' (45:2)
Pia rejea Qur'an (4:166), (32:2-3), (35:31), (25:1), n.k



iii. Hali aliyokuwa nayo Mtume (s.a.w) wakati akipokea wahyi

- Mtume (s.a.w) alikuwa akiogopa kuwa atasahau anayoteremshiwa, akawa na pupa kuyakariri, hii ni ushahidi kuwa hayakuwa maneno yake.
Rejea Qur'an (75:16-18), (87:6-7)



iv. Qur'an kushuka kidogo kidogo kwa kipindi cha miaka 23 kimatukio.

- Kama Qur'an aliitunga Mtume (s.a.w) angeliitunga yote kwa pamoja tena kwa haraka ili kuitumia kuongoza jamii.
Rejea Qur'an (17:106), (25:32), (76:23)



v. Mtume (s.a.w) kukosolewa ndani ya Qur'an

- Kama Mtume Muhammad (s.a.w) angelikuwa ndiye mtunzi wa Qur'an asingelikosolewa mara nyingi katika Kitabu alichokitunga mwenyewe. Rejea Qur'an (33:1-3), (66:1), (80:1-12), n.k


vi. Kutokea kweli matukio yalitabiriwa katika Qur'an

- Mifano ya matukio ni; Waislamu kuwashinda Warumi na Maquishi na kuwa katika hali ya furaha na amani, utabiri wa kuangamia Abu Lahab. Rejea Qur'an (30:2-3), (111:1-5), (93:4-5), (94:5-6), (48:1), n.k



vii. Mpangilio na muundo wa aya na sura za Qur'an wakati wa kushuka kwake na kuandikwa katika msahafu.
- Aya na sura za Qur'an zimepangiliwa ki-idadi na kimuundo kwa namna ya ajabu ambayo hakuna mwanaadamu yeyote anayeweza kufanya hivyo.


Mfano: neno mbingu saba limetajwa mara saba, neno 'Yaum' (siku)

limetajwa mara 365, neno 'shahri' (mwezi) limetajwa mara 12, n.k.

Rejea Qur'an (3:59), (2:87), (2:33-37), (20:115-121), n.k



viii. Wanaadamu kushindwa kutunga na kuandika Kitabu mfano wa Qur'an

- Qur'an imetoa changamoto kwa kuwataka wanaadamu kutunga kitabu au sura moja au aya moja tu mfano wa Qur'an hakuna aliyeweza.
Rejea Qur'an (17:88), (11:13), (2:23), (10:38), n.k



ix. Maudhui ya Qur'an na mvuto wa ujumbe wake

- Qur'an inaathiri na kugonga nyoyo za watu hata ambao si waislamu, mfano Umar Ibn Khattab na mshairi Labib ibn Rabiah kabla ya kusilimu. Rejea Qur'an (20:1-7), (4:82), (39:23), n.k


x. Ahadi ya Kuhifadhiwa na kulindwa Qur'an na kubakia katika asili yake

- Ni Qur'an pekee ambayo mwanaadamu hawezi kukiharibu kwa namna

yeyote ile ya kuongeza au kupungaza chochote.

Rejea Qur'an (15:9)





b) Ushahidi kutokana na Historia (Hadith)

- Historia ilivyokuwa inashuka Qur'an na namna ambavyo Mtume (s.a.w)

alikuwa akiipokea ni ushahidi pia kama ifuatavyo;



i. Mtume (s.a.w) kushikwa na hofu na wasiwasi sana alipotembelewa na

Malaika Jibril (a.s) katika Jabal (Pango la) Hiraa.

ii. Mtume (s.a.w) alikuwa anabadilika haiba yake na kutokwa na jasho jingi wakati wa kupokea wahyi.
Rejea Hadith ya Bi Aisha (r.a)




                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 344


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Nasaha za Lut(a.s) kwa Watu Wake
Nabii Lut(a. Soma Zaidi...

Kuanzishwa kwa vitenge vya ulinza na Usalama, na usalama wa taifa
Soma Zaidi...

Maana ya Hija na Umuhimu wa kuhiji
Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME SULAIMAN(A.S)
Sulaiman(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISHAQA NA YAQUB
Soma Zaidi...

Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani
(a) UgirikiTunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika. Soma Zaidi...

Swala ya Idi al-fitir na namna ya kuiendea
Soma Zaidi...

nguzo za uislamu: Kutoa zaka, lengo la kutoa zaka na faida zake
Kutoa Zakat. Soma Zaidi...

Kisa cha Malkia wa Sabaa.
Sabaa ulikuwa mji katika nchi inayojulikana leo kama Yemen. Soma Zaidi...

HISTORIA NA MAISHA YA MTUME IDRISA (A.S)
Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a. Soma Zaidi...

Maharimu ni wanawake na wanaume walioharamishwa kuoana
Soma Zaidi...

Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...