picha

Uthibitisho Kuwa Qur’an ni Neno la Mwenyezi Mungu (s.w)

Uthibitisho Kuwa Qur’an ni Neno la Mwenyezi Mungu (s.w)

Uthibitisho Kuwa Qur’an ni Neno la Mwenyezi Mungu (s.w)

a) Uthibitisho Kutokana na Qur’an Yenyewe

i. Kutojua kusoma na kuandika kwa Mtume Muhammad (s.a.w)

- Mtume (s.a.w) kutokujua kusoma na kuandika ni ushahidi tosha kuwa

asingeweza kutunga Kitabu mfano wa Qur’an. Rejea Qur’an (7:158), (29:48)


ii. Qur’an yenyewe inajieleza kuwa ni Kitabu cha Allah (s.w) kama ifuatavyo; “Uteremsho wa Kitabu hiki umetoka kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye Nguvu na Mwenye Hikima” (45:2)
Pia rejea Qur’an (4:166), (32:2-3), (35:31), (25:1), n.k



iii. Hali aliyokuwa nayo Mtume (s.a.w) wakati akipokea wahyi

- Mtume (s.a.w) alikuwa akiogopa kuwa atasahau anayoteremshiwa, akawa na pupa kuyakariri, hii ni ushahidi kuwa hayakuwa maneno yake.
Rejea Qur’an (75:16-18), (87:6-7)



iv. Qur’an kushuka kidogo kidogo kwa kipindi cha miaka 23 kimatukio.

- Kama Qur’an aliitunga Mtume (s.a.w) angeliitunga yote kwa pamoja tena kwa haraka ili kuitumia kuongoza jamii.
Rejea Qur’an (17:106), (25:32), (76:23)



v. Mtume (s.a.w) kukosolewa ndani ya Qur’an

- Kama Mtume Muhammad (s.a.w) angelikuwa ndiye mtunzi wa Qur’an asingelikosolewa mara nyingi katika Kitabu alichokitunga mwenyewe. Rejea Qur’an (33:1-3), (66:1), (80:1-12), n.k


vi. Kutokea kweli matukio yalitabiriwa katika Qur’an

- Mifano ya matukio ni; Waislamu kuwashinda Warumi na Maquishi na kuwa katika hali ya furaha na amani, utabiri wa kuangamia Abu Lahab. Rejea Qur’an (30:2-3), (111:1-5), (93:4-5), (94:5-6), (48:1), n.k



vii. Mpangilio na muundo wa aya na sura za Qur’an wakati wa kushuka kwake na kuandikwa katika msahafu.
- Aya na sura za Qur’an zimepangiliwa ki-idadi na kimuundo kwa namna ya ajabu ambayo hakuna mwanaadamu yeyote anayeweza kufanya hivyo.


Mfano: neno mbingu saba limetajwa mara saba, neno “Yaum” (siku)

limetajwa mara 365, neno “shahri” (mwezi) limetajwa mara 12, n.k.

Rejea Qur’an (3:59), (2:87), (2:33-37), (20:115-121), n.k



viii. Wanaadamu kushindwa kutunga na kuandika Kitabu mfano wa Qur’an

- Qur’an imetoa changamoto kwa kuwataka wanaadamu kutunga kitabu au sura moja au aya moja tu mfano wa Qur’an hakuna aliyeweza.
Rejea Qur’an (17:88), (11:13), (2:23), (10:38), n.k



ix. Maudhui ya Qur’an na mvuto wa ujumbe wake

- Qur’an inaathiri na kugonga nyoyo za watu hata ambao si waislamu, mfano Umar Ibn Khattab na mshairi Labib ibn Rabiah kabla ya kusilimu. Rejea Qur’an (20:1-7), (4:82), (39:23), n.k


x. Ahadi ya Kuhifadhiwa na kulindwa Qur’an na kubakia katika asili yake

- Ni Qur’an pekee ambayo mwanaadamu hawezi kukiharibu kwa namna

yeyote ile ya kuongeza au kupungaza chochote.

Rejea Qur’an (15:9)





b) Ushahidi kutokana na Historia (Hadith)

- Historia ilivyokuwa inashuka Qur’an na namna ambavyo Mtume (s.a.w)

alikuwa akiipokea ni ushahidi pia kama ifuatavyo;



i. Mtume (s.a.w) kushikwa na hofu na wasiwasi sana alipotembelewa na

Malaika Jibril (a.s) katika Jabal (Pango la) Hiraa.

ii. Mtume (s.a.w) alikuwa anabadilika haiba yake na kutokwa na jasho jingi wakati wa kupokea wahyi.
Rejea Hadith ya Bi Aisha (r.a)




                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: General Main: Post File: Download PDF Views 3172

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 web hosting     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

HISTORIA YA UANDISHI WA HADITHI

Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.

Soma Zaidi...
Lengo la swala

Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake.

Soma Zaidi...
mgawanyiko katika quran

MGAWANYIKO KATIKA QURAN Juzuu, Sura, Aya, Manzil, Qara Wataalamu wa elimu za Qurani katika fani za uandishi na usomaji wameigawanya Qurani katika mafungu ili kuwezesha urahisi kwa wasomaji wa qurani.

Soma Zaidi...
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Mjue Muislamu aliyeanzisha Chuo kikuu cha kwanza dunani

Chuo kikuu cha wanza duniani cha Elimu kielimu hakukihusu tu waislamu bali hata ambao sio waislamu walipata fursa ya kujifunza.

Soma Zaidi...