Madai ya Makafiri Dhidi ya Qur’an na Udhaifu Wake

i.

Madai ya Makafiri Dhidi ya Qur'an na Udhaifu Wake

Madai ya Makafiri Dhidi ya Qur'an na Udhaifu Wake

i. Dai kuwa Qur'an ni mashairi aliyotunga Muhammad (s.a.w)

- Maquraishi wa Makka walidai kuwa Qur'an ni mashairi aliyotunga

Muhammad kwa ujuzi na ueledi mkubwa wa historia ya Waarabu.



Udhaifu wa dai hili:

- Ujumbe wa Qur'an unatofautiana sana na ule wa mashairi kimvuto na taathira kama mshairi mashuhuri Labiib Ibn Rabiah alikiri hilo.




ii. Dai kuwa Qur'an ni zao la njozi za Mtume (s.a.w) zilizovurugika

- Waandishi kama akina Anderson na Watt walidai kuwa Qur'an ni zao la

mawazo na dhana tu za Muhammad zilizovurugika.



Udhaifu wa dai hili:

- Dhana hizi hazina ukweli wowote kwa sababu haijawahi kutokea katika historia ya mwanaadamu kuuunda kitabu kwa ndoto mithili ya Qur'an. Rejea Qur'an (21:5)


iii. Dai kuwa Qur'an ni zao la mwenye kifafa na aliyepagawa na shetani

- Baadhi ya waandishi wa kikafiri wamedai bila ushahidi wowote kuwa

Mtume Muhammad (s.a.w) alitunga Qur'an akiwa katika hali ya kifafa.



Udhaifu wa dai hili:

- Dai hili halina ukweli wowote kwani haijawahi kutokea katika historia ya mwanadamu mtu mwenye kifafa kuunda Kitabu chenye wafuasi wengi. Rejea Qur'an (10:38)



iv. Dai kuwa Qur'an ni aya za shetani

- Salman Rushdie alidai kuwa Muhammad hakushukiwa na wahyi wowote

isipokuwa ni mawazo yake akiongozwa na shetani katika kuandika Qur'an.



Udhaifu wa dai hili:

- Qur'an yenyewe inadhihirisha kuwa si aya za shetani, na kama ingelikuwa

ni aya za shetani kwa nini adhhirishe uadui wake kwa wanaadamu?

Rejea Qur'an (81:25), (6:112), (35:6), (17:88), (4:82)



v. Dai kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) aliandika Qur'an kwa msaada wa Mayahudi na Wakristo

- Makafiri wanadai kuwa Mtume (s.a.w) aliandika Qur'an kwa kunakili

mafundisho ya Biblia kutokana na baadhi ya aya kufanana.



- Pia wanadai kuwa alifundishwa na Ujumbe wa Qur'an alipokutana na Padri

Bahirah katika safari yake ya Shamu akiwa na miaka 12.



Udhaifu wa madai haya:

- Mtume Muhammad (s.a.w) hakujua kusoma wala kuandika na alisema

Qur'an inatoka kwa Allah (s.w) vinginevyo ingelikuwa na hitilafu nyingi.



- Nakala ya kwanza ya Agano la Kale iliyotafsiriwa kwa lugha ya Kiarabu ilipatikana miaka 200 baada ya kutawafu (kufa) Mtume (s.a.w).


- Mtume (s.a.w) alikutana na Padri Bahirah akiwa na miaka 12, sio jambo rahisi kufundishwa ujumbe muda huo na aje kuufundisha baada ya miaka
28.

Rejea Qur'an (16:103)



vi. Dai kuwa Muhammad (s.a.w) alitunga Qur'an ili kuleta umoja na ukombozi wa

Waarabu

- Wako baadhi ya Makafiri wanaodai kuwa Muhammad (s.a.w) aliitunga

Qur'an ili awaunganishe na kuwakomboa Waarabu.



Udhai wa dai hili:

- Dai hilo sio la kweli kwa sababu hakuna msisitizo wowote ndani ya Qur'an juu ya ukombozi na umoja wa Waarabu na Qur'an inapingana na ukabila.


- Pia Mtume (s.a.w) angelikubali pendekezo la Maquraishi kuwa kiongozi wa

Waarabu ili atumie fursa hiyo kujenga umoja wa Waarabu.

Rejea Qur'an (3:42)



vii. Dai kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur'an ili kurekebisha tabia za

Waarabu.

- Wapo Makafiri wanaodai kuwa Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur'an ili

kujenga mwenendo na tabia nzuri za ndugu zake Waarabu.



Udhaifu wa dai hili:

- Kujenga tabia na mwenendo mzuri wa watu ni jambo zuri ambalo halihiajii kutumia udanganyifu au uongo wa aina yeyote.
Rejea Qur'an (6:93), (5:101)



viii. Dai kuwa Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur'an ili ajinufaishe kiuchumi.

- Baadhi ya watu wanadai kuwa Muhammad (s.a.w) kwa ajili ya kujinufaisha kiuchumi.


Udhaifu wa dai hili:

- Kama Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur'an kujinufaisha kiuchumi mbona

hali yake kiuchumi ilizidi kuwa duni hata baada ya Utume.

Rejea Qur'an (33:28-29)



ix. Dai kuwa Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur'an ili kuwania madaraka na ukubwa

- Makafiri wamedai pia kuwa Muhammad (s.a.w) alitunga Qur'an ili kujipatia

madaraka na ukubwa kwa Waarabu.



Udhaifu wa dai hili:

- Mtume Muhammad (s.a.w) ni mtu aliyejulikana sana ulimwenguni, hivyo

hakuwa na haja ya kutumia Qur'an kuomba madaraka.



- Mtume (s.a.w) mwenyewe alikataa ofa ya kuwa kiongozi wa Waarabu walipomtaka ili aache kazi ya kulingania Uislamu.
Rejea Qur'an (9:61), (45:9), (28:86), (18:110), (6:50)



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 495


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

mambo gani ni haramu kwa mwenye damu ya Hedhi na nifasi (damu ya uzazi)
Soma Zaidi...

Kitabu Cha Quran na sayansi
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Nani Muadilifu na zipi sifa za mtu muadilifu kwenye uislamu
Uadilifu ni usimamizi'wa ukweli na kutoa'haki'kwa kila anayestahiki'kulingana na ukweli. Soma Zaidi...

HISTORIA NA MAISHA YA NABII ISMAIL(A.S)
Ismail(a. Soma Zaidi...

Zifahamu njia za kutwaharisha, aina za maji, udongo na Namna ya kujitwaharisha
Soma Zaidi...

NAMNA YA KUSWALI SWALA YA IJUMAA, JENEZA, SWALA YA JAMAA NA SWALA YA SUNNHA (tarawehe, tahajudi na qiyamu layl)
1. Soma Zaidi...

Kitabu Cha Form Two Chemistry
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Tamko la suluhu baada ya vita vya Siffin
Soma Zaidi...

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena. Soma Zaidi...

sura ya 02
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Sababu kuu za maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, Tumbo la ngiri na chango
Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, na tumbo la ngiri kwa wanaume, na tumbo la chango kwa wanawake Soma Zaidi...

Namna ya kuoga josho, kujitwaharisha damu ya Hedhi, damu ya kuzaa Nifasi na Janaba
Soma Zaidi...