picha

Dua ya kuzuru makaburi, na utaratibu wa kuzuru makaburi

Kuzuru makaburi ni katika matendo ya sunah yaani unapata thawabu kwa kwenda klizuru kaburi.

Dua ya kuzuru makaburi, na utaratibu wa kuzuru makaburi

UTARATIBU NA DUA YA KUZURU MAKABURI

Kuzuru makaburi ni katika matendo ya sunah yaani unapata thawabu kwa kwenda klizuru kaburi. Ni katika matendo yanayotukumbusha kifo. Hata mtume allikuwa akienda kuzuru makaburi mara kadhaa. Hata mwishoni mwa siku za mwisho za uhai wake alikwenda kuzuru makaburi na kuwaaga waliokufa na kuwaombea dua.



Hapo mwanzo wanawake walikatazwa kuzuru makaburi kwa maneno ya Mtume aliposema “wamelaaniwa wanawake wenye kuzuru makaburi”. lakini baadaye mtume akawaruhusu wanawake kuzuru makaburi. Kwa ufupi ibada hii ni kwa waislamu wote na haina siku maalumu ama wakati maalumu. Kwani Mtume alikuwa anakwenda kuzuru makaburi hadi wakati wa usiku.



Kuzuru makaburi sio lakima uwe na udhu. Unaweza kuzuru hata ukiwa hupo twahara. Ukifika kwanza unaanza kusalimia (kutoa salamu) kisha unaomba dua pia ukiwa makaburini unaweza kulimia ama kusafishai kaburi ama makaburi. Ama kujazia udongo haya yote sio ya lazima. Kisha utaomba dua



Dua ya kuzuru kaburi
لسَّلامُ عَلَـيْكُمْ أَهْلَ الدِّيارِ مِنَ المؤْمِنيـنَ وَالْمُسْلِمينَ، وَإِنّا إِنْ شاءَ اللهُ بِكُـمْ لاحِقُـونَ، (وَيَرْحَمُ اللَّهُ الْمُسْتَقْدِمِينَ مِنَّا وَالْمُسْتَأْخِرِينَ) أَسْـاَلُ اللهَ لَنَـا وَلَكُـمْ العَـافِيَةَ.

Assalaamu ’alaykum ahlad-diyaar minal Mu-uminiyna wal Muslimiyn, wainnaa In Shaa Allaahu bikum laahiquwn. (Wa yarhamu-Allaahu al-mustaqdimiyna minnaa wal musta-akhiriyna). As-alu-Allaaha lanaa walakumul-’aafiyah

Amani ishuke juu yenu watu wa nyumba za Waumini na Waislamu, nasi apendapo Allaah tutakutana nanyi (Na Allaah Awarehemu wa mwanzo na wa mwisho). Namuomba Allaah Atupe sisi nanyi Al-’Aafiyah
al-hidaayah.com

Mwenye kuzuru makaburi anaruhusiwa kwenda akiwa peke yake ama akiwa na wenzie. Halikadhalika hakuna mavazi ya rangi maalumu wakati wa kuzuru ama kuzika. Hakuna haja ya kunyoa nywele wana kuandaa vyakula. Hairuusiwi kuyataja mabaya ya aliuyefariki ama kukaa juu ya kaburi. Pia hairuhusiwi kuzungumza mabo maovu maeneo ya makaburi.

Kwa hakika kuzuru makaburi ni ibada inayotaka utulivu wa nafsi. Kwani inatakikana moyo upate mawaidha kutokana na kutembelea kaburi. Mwenye kuzuru kaburi apate athari ya kuyaogopa mauti ili apate kufanya maandalizi.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 6900

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 web hosting     👉4 ai web app     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu

Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.

Soma Zaidi...
Uzuri wa Benki za kiislamu

Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine?

Soma Zaidi...
Namna ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.

Post hii inakwenda kukugundisha jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...
Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s.a.w)

Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s.

Soma Zaidi...