Katika somo hili, utajifunza mbinu mbalimbali za kubadilisha muonekano wa maandishi kwa kutumia CSS, kama vile kupamba maandishi kwa mistari, kivuli, nafasi kati ya herufi, na mpangilio wa maneno.
Baada ya kujifunza jinsi ya kudhibiti fonti kwenye CSS, hatua inayofuata ni kupamba maandishi ili yawe na mvuto na usomaji bora. Upambaji huu hufanywa kwa kutumia properties za CSS kama text-decoration, text-shadow, letter-spacing, word-spacing, na text-align. Hizi husaidia kufanya maandishi yaonekane kwa mtindo maalum au wa kipekee.
text-decorationInatumika kuweka mistari kwenye maandishi kama vile mstari wa chini, juu, au mstari wa kupitisha kati.
a {
text-decoration: underline;
}
Chaguzi:
none – Hakuna mistari
underline – Mistari ya chini ya maandishi
overline – Mistari ya juu ya maandishi
line-through – Mistari katikati ya maandishi
text-shadowInatumika kuongeza kivuli kwenye maandishi.
h1 {
text-shadow: 2px 2px 5px gray;
}
Format:text-shadow: horizontal vertical blur-radius color;
horizontal – umbali wa kivuli upande wa kulia au kushoto
vertical – umbali wa kivuli juu au chini
blur-radius – kipenyo cha kivuli
color – rangi ya kivuli
letter-spacingHudhibiti nafasi kati ya kila herufi.
p {
letter-spacing: 2px;
}
Thamani hasi hupunguza nafasi
Thamani chanya huongeza nafasi
word-spacingHudhibiti nafasi kati ya maneno.
p {
word-spacing: 10px;
}
text-alignHudhibiti mpangilio wa maandishi katika mstari.
div {
text-align: center;
}
Chaguzi:
left – Maandishi yanapangwa upande wa kushoto
right – Maandishi yanapangwa upande wa kulia
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili tutajifunza kuhusu z-index, ambayo hutumika kudhibiti ni elementi ipi ionekane juu au chini wakati kuna elementi nyingi zinazofunika sehemu moja. Pia tutajifunza kuhusu stacking context, yaani jinsi vivinjari vinavyopanga
Soma Zaidi...katika somo hili utajifunza jinsi ya ku install css kwenye ukurasa wa html
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza kipengele kipya kinachoitwa if() function ndani ya CSS, kilichoanza kupatikana kwenye toleo la Chrome 137. Kipengele hiki kinaturuhusu kuandika mantiki ya masharti moja kwa moja kwenye property ya CSS, bila kutumia JavaScript wala media query zilizotawanyika. Tutajifunza pia aina za queries: media(), supports(), na style() pamoja na matumizi yao ya kivitendo kwenye tovuti. Mwisho, tutaeleza kwa kina kuhusu pointer na any-pointer.
Soma Zaidi...Katika somo hili, utajifunza vipengele vya juu zaidi vya Flexbox: flex-wrap, flex-grow, flex-shrink, na flex-basis. Pia tutajifunza jinsi ya kujenga muundo wa safu (rows) na nguzo (columns) kwa kutumia Flexbox layout.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza muundo wa boksi (Box Model) katika CSS. Box model ni mfumo wa msingi wa kupanga vipengele katika ukurasa wa HTML, ukiwa na sehemu kuu nne: content, padding, border, na margin.
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza kuhusu CSS functions muhimu zinazotumika kufanya mahesabu, kuweka vipimo vya kisasa vinavyobadilika kulingana na hali ya kifaa, na kutumia variables. Tutazingatia functions kama: calc(), clamp(), var(), min(), max(), na mwishoni tutajifunza jinsi ya kutengeneza custom function kwa kutumia variables.
Soma Zaidi...Katika somo hili uatkwenda kujifunza aina za css selectors
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kuleta miondoko na harakati kwenye tovuti kwa kutumia CSS Transitions na Animations. Hii itasaidia kuboresha muonekano na matumizi ya tovuti.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu CSS frameworks mbalimbali zinazosaidia kuharakisha uundaji wa mitindo kwenye tovuti. Tutazungumzia frameworks maarufu kama W3.CSS, Bootstrap, Google Fonts, na nyinginezo, faida, matumizi, na tofauti zao.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu CSS Timing Functions, ambazo hutumika kudhibiti kasi na mtiririko wa transition na animation. Utaelewa tofauti kati ya ease, linear, ease-in, ease-out, ease-in-out, pamoja na jinsi ya kutumia cubic-bezier() kwa kudhibiti mwendo wa mabadiliko kwenye elementi.
Soma Zaidi...