Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii

Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asr

SURAT AL-ARS
Wafasiri wengi wanasema sura hii ilishuka Makka.
Imam Shafii anasema, Sura hii ina maana nyingi na pana. Na kama mtu aifikiri, haja zake zote za dini zinaweza kutimizwa. Imesimuliwa katika Hadithi ya kuwa masahaba wawili kila mara walipokuwa wanakutana wakati wa kuagana walikuwa wakisomeana sura hii.




Neno hili maana yake ni wakati, wakati wa alasiri, na pia maana yake ni kukamua. Katika Aya hii Mwenyezi Mungu analeta ushahidi wa wakati kuonyesha ya kwamba kadiri wakati unavyopita umri wa kila mtu unapungua na kuingia katika hasara maana kila kitu kinasogelea mwisho wake na kitakufa. Lakini watu wanaweza kujiepusha na hasara hiyo kwa kuamini na kutenda mema na kuusiana kushika haki na subira, maana mambo haya yatafanya roho zao ziendelee katika maisha ya raha huko Akhera.



Katika sura hii habari za watu wa namna mbili zimeelezwa. Ya kwanza ni wale ambao wamo hasarani, na pili ni wale ambao wameamini na kufanya vitendo vizuri. Ni dhahiri ya kuwa wasioamini wala hawafanyi vitendo vizuri wao ndio watakaokuwa katika hasara. Lakini wanaoamini kwa moyo wote, tena wanaionyesha imani yao kwa viungo vyao, kwa kutenda sawa na walivyoamini, bila shaka wao watalindwa na hasara. Tena ikumbukwe ya kuwa Mwenyezi Mungu aliposema "walioamini" kwa hakika ameashiria kwenye ukamilifu wa elimu; maana imani haiwezi kupatikana bila elimu, Basi mtu anapopata ukamilifu katika elimu, anakuwa mwenye imani hasa. Na Mwenyezi Mungu aliposema "kufanya vitendo vizuri" ameelekeza kwenye ukamilifu wa amali, yaani matendo. Hivyo Mwenyezi Mungu amesema ya kuwa watu wanaokamilika katika elimu, na wanaokamilika katika vitendo, wao wanasalimika katika hasara na wanaokoka.



Hakuna sababu maalumu yenye kuaminika juu ya kushuka kwa sura hii.



UMUHIMU WA SURA HII
Sura hii inachukuliwa kama muhtasari wa Qur'ani nzima na karibu wasomi wote mashuhuri wa kitamaduni na wa kisasa wa Kiislam wakiwemo Imam Shafi, Ibn Kathir, Israr Ahmed na Farhat Hashmi.



Ibn Kathir, mfasiri wa Quran anashikilia kwamba sura hii, kama onyo kwa waumini kutopoteza wakati au wangeweza kudhalilishwa au hata kuharibiwa.



Imam Shafi, alishikilia-kwamba ikiwa Mungu angefunua tu surah hii ingetosha kwa mwongozo wa wanadamu wote. Ilielezea kwa muhtasari kiini cha ujumbe wa Kurani. Kwa hivyo, Imam Shafi'i anasisitiza kwamba ikiwa mtu angefuata ushauri wake, ilitosha kwa wanadamu kupata mafanikio maishani.



Sayyid Qutb, Mfasiri wa Quran, anathibitisha kwamba surah hii inaelezea mfumo kamili wa maisha ya mwanadamu kulingana na maoni ya Kiisilamu. Anasema kuwa inafafanua, kwa njia iliyo wazi na fupi zaidi, dhana ya kimsingi ya imani katika muktadha wa ukweli wake kamili.



Al-Tabarani: wakati wanadamu wanajikuta wamepotea; inaweza kujihuisha kwa kurudi kwenye fomula iliyotolewa na aya ya tatu na kanuni / masharti manne, ambayo yanazingatiwa kama msingi.






                   





Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1077

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

surat al mauun

SURATUL-MAM’UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat..

Soma Zaidi...
Faida za kujuwa Quran tajwid

Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid.

Soma Zaidi...
quran tahadhari

TAHADHARI KWA WASOMAJI WA QURAN Wasomaji wa qurani wawe na tahadhari katika usomaji wao.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA

SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’).

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq

Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al-Falaq na surat an-Nas na fadhila za kusoma sura hizi

SURAT AL-MUAWIDHATAYN (SURAT AL-FALAQ NA SURATUN-NAS) Inaelezwa kuwa sura mbili hizi zilishuka pamoja, na maulamaa wanaelezea kuwa Mtume (s.

Soma Zaidi...