Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu vitamini D, kazi zake, vyanzo vyake na upungufu wake mwilini.
Vitamini D ni vitamini muhimu sana kwa afya ya binadamu, hasa katika uwezo wa mwili kuvyonza madini ya calcium, magnesium, na phosphate. Vitamini D hutengenezwa chini ya ngozi kwa kutumia mwanga wa jua. Vitamini D ipo katika makundi mawili makuu: vitamini D2 na vitamini D3. Vitamini hizi ni muhimu kwa kazi mbalimbali mwilini. Katika makala hii, tutaangazia zaidi kuhusu vitamini D, namna inavyotengenezwa mwilini, kazi zake, na athari za upungufu wake.
Vitamini D ni fat-soluble vitamin ambayo imetokana na compound za cholesterol. Vitamini D viligunduliwa mwaka 1922 na mwanasayansi Elmer McCollum. Historia ya uchunguzi huu ulianzia toka mwaka 1914 wakati Elmer McCollum na Marguerite Davis walipogundua vitamini A.
Vitamini hivi viliitwa D kwa sababu ndio vitamini vya nne kugundulika baada ya vitamini A, B, na C. Ugunduzi wa vitamini D ulianzia kwenye mbwa mgonjwa aliyekuwa na matege, na baada ya utafiti, ilibainika kuwa mbwa huyo alipona kutokana na chembechembe ambazo baadaye ziliitwa vitamini D.
Kama ilivyo kwa vitamini K na B, vitamini D pia imegawanyika katika makundi kadhaa. Makundi makuu ni vitamini D2 na vitamini D3. Makundi haya mawili kwa pamoja hufahamika kama vitamini D.
Vitamini D2 na vitamini D3 kwa pamoja pia huitwa calciferol. Vitamini D2 ilipewa sifa yake ya kikemikali mwaka 1931, na vitamini D3 ilipewa sifa yake ya kikemikali mwaka 1935.
Vitamini D ina kazi kuu ya kusaidia katika metabolism ya madini ya calcium. Kwa lugha nyepesi, vitamini D inahakikisha unyonzwaji wa madini ya calcium, magnesium, na phosphate unafanyika vyema ndani ya utumbo mdogo.
Chanzo kikuu cha vitamini D ni mwanga wa jua, ambao husaidia katika utengenezwaji wa vitamini D chini ya ngozi. Watu ambao hawawezi kupata mwanga wa jua wa kutosha wanaweza kupata upungufu wa vitamini D.
Upungufu wa vitamini D unaweza kusababisha athari kubwa kwenye afya. Miongoni mwa athari hizo ni:
Vitamini D ni muhimu sana kwa afya ya binadamu, hasa katika uwezo wa mwili kuvyonza madini ya calcium, magnesium, na phosphate. Ni muhimu kuhakikisha unapata vitamini D ya kutosha kwa njia ya mwanga wa jua na lishe sahihi ili kudumisha afya bora ya mifupa na mfumo wa kinga. Endelea kujifunza na kuwa makini katika lishe yako ili kuhakikisha unapata vitamini D ya kutosha na kuepuka athari za upungufu wake.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowKatika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula spinach
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula zabibu
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula nanasi
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula ubuyu
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kutumia ndimu na limao
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula miwa
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula tangawizi
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula magimbi. Magimbi ni vyakula aina ya mihogo na viazi.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhus vyakula vya fati, kazi zake na vyanzo vyake.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu faida za kiafya za kula korosho
Soma Zaidi...