Menu



Ana za vyaula somo la 10: Vyaula vya vitamini E

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu vitamini E, kazi zake mwilini, vyakula vyenye vitamini E pamoja na madhara ya kutokuwa na vitamini E vya kutosha mwilini

Vitamini E na Faida Zake Mwilini

Vitamini E ni moja ya vitamini muhimu vinavyopatikana kwenye vyakula, matunda, na mboga. Pia unaweza kuipata kwa njia ya vidonge kutoka kwenye maduka ya madawa. Kama ilivyo kwa vitamini A, B, C, D na K, upungufu wa vitamini E mwilini unaweza kusababisha madhara ya kiafya, ijapokuwa upungufu wa vitamini huu ni nadra sana kutokea. Katika makala hii, nitakupa somo linalohusu vitamini E, kazi zake, chanzo chake, na madhara ya upungufu wake.

Yaliyomo:

  1. Maana ya Vitamini E
  2. Kazi za Vitamini E
  3. Vyakula vya Vitamini E
  4. Upungufu wa Vitamini E
  5. Tafiti Kuhusu Vitamini E

 

Maana ya Vitamini E

Mnamo mwaka 1922, wanasayansi wawili kwa majina ya Herbert Mclean Evans na Katharine Scott Bishop waligundua vitamini E. Baada ya ugunduzi wa vitamini E, tafiti mbalimbali zilifanywa ili kuonyesha kazi zake mwilini. Kwa mfano, mwaka 1946, wanasayansi walikuwa wakifanya tafiti juu ya nadharia inayodai kuwa vitamini E husaidia dhidi ya maradhi ya moyo na mishipa ya damu (coronary heart diseases). Mwaka 1949, tafiti zilifanywa kuhusu nadharia ya kuwa vitamini E huweza kusaidia watoto njiti kuwakinga na maradhi kadhaa.

 

Kazi za Vitamini E Mwilini

Vitamini E katika miili yetu ina kazi kuu zifuatazo:

  1. Antioxidant: Vitamini E ni antioxidant, ambayo husaidia kuzuia athari za kemikali mbaya ambazo zinaweza kuharibu miili yetu.
  2. Utando wa Seli: Husaidia katika utengenezwaji wa utando wa seli na kulinda seli dhidi ya uharibifu wa kemikali.
  3. Ukuaji wa Misuli: Husaidia katika ukuaji mzuri wa misuli.
  4. Utando wa Neva na Mapafu: Husaidia katika utengenezwaji wa utando katika maeneo mbalimbali ya mwili kama neva, mapafu, na maeneo mengine.

 

Upungufu wa Vitamini E

Upungufu wa vitamini E hutokea nadra sana, lakini tafiti zinaonyesha kuwa upungufu huu unaweza kusababisha matatizo kwenye mfumo wa fahamu, ukuaji mzuri wa misuli, na udhaifu wa misuli. Pia, upungufu wa vitamini E unaweza kuathiri macho na hivyo kupelekea mtu kutoona vizuri.

 

Vyakula vya Vitamini E

  1. Nyama ya kuku na ng'ombe
  2. Maini
  3. Mayai
  4. Alizeti
  5. Karanga
  6. Spinach
  7. Korosho
  8. Mchele
  9. Viazi vitamu
  10. Siagi
  11. Samaki
  12. Maziwa
  13. Palachichi

 

Tafiti Kuhusu Vitamini E

Tafiti mbalimbali zimefanywa kuhusu vitamini E, lakini zinahitaji kuendelea zaidi maana bado majibu ya uhakika hayajapatikana juu ya matokeo ya tafiti hizo. Ijapokuwa maneno ni kama hivyo, ukweli ni kuwa vitamini E vina faida katika afya zetu. Miongoni mwa tafiti hizo ni:

  1. Mwaka 2017: Tafiti zilionyesha kuwa vitamini E husaidia kupunguza udhaifu wa misuli wakati wa kuzeeka.
  2. Maradhi ya Ubongo: Tafiti zinaonyesha kuwa vitamini E husaidia kulinda dhidi ya maradhi ya ubongo kama kusahausahau na kuchanganyikiwa.
  3. Saratani: Tafiti zinaonyesha kuwa vitamini E husaidia kupunguza uwezekano wa kupata saratani ya figo, kibofu, mapafu, na korodani.
  4. Maradhi ya Moyo na Mishipa ya Damu: Vitamini E husaidia kulinda mwili dhidi ya maradhi ya moyo na mishipa ya damu.
  5. Wajawazito: Vitamini E ni muhimu kwa wajawazito kwani husaidia katika ukuaji wa fetasi na kulinda afya ya mama.

 

Hitimisho

Vitamini E ni muhimu sana kwa afya ya binadamu. Ni muhimu kuhakikisha unapata vitamini E ya kutosha kupitia lishe sahihi na, inapohitajika, kupitia vidonge vya vitamini E. Kwa kufanya hivyo, utakuwa unadumisha afya yako na kuepuka athari zinazoweza kusababishwa na upungufu wa vitamini E. Endelea kuwa makini katika lishe yako na ufuatilie tafiti mpya kuhusu vitamini E ili kujua faida zaidi zinazoweza kutolewa na vitamini hii muhimu.

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-07-21 17:21:33 Topic: Aina za vyakula Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 192


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Ana za vyakula somo la 37: Faida za kula njegere
Katika somo hili utakwend akujifunza faidaza kiafya za kula njegere Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 38: Faida za kula mahindi
Kkatika somo hil utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula mahindi Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 55: Faida za kula senene panzii na kumbikumbi
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula senene, panzi na kumbikumbi Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula mbegu za matikiti
Katika post hii utajifunza faida za kula mbegu za tikiti. Baada ya post hii utajifunza kuwa mbegu za tikiti hazitupwi. Soma Zaidi...

Maina za vyakula somo la 39: Faida za kula maini
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula mainai Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula mbegu za matango
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula mbegu za matango Soma Zaidi...

Aina za vyakula somola 50: Faida za kula parachichi
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula parachichi Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula mbegu za pipilipi
Katika somohili utakwenda kujifunzafaida za kiafya za kula mbegu za pilipili. Hapa ttunazunumzia pilipili kwaujumla bila kujali ni aina gani ya pilipili. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula mbegu za mafenesi
Katia post hii utakwend akujifunza namna ambavyo tunaweza kufaidika kwa kula mbegu za mafenesi mwilini. Fenesi ama jackfruit ni moja katika matunda yanayopatikana katika maeneo ya kitropic. Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 57: Faida za kula stafeli
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula stafeli Soma Zaidi...