Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu vitmini C, kazi zake mwilini, na vyakula vya vitamini C.
Vitamini C ni mojawapo ya vitamini muhimu sana katika mfumo wa kinga mwilini. Inajulikana kwa sifa zake za antioxidant, ambazo husaidia kuupa mwili nguvu na kinga ya kupambana na sumu na vijidudu shambulizi. Vitamini C inapendelewa kuwepo ndani ya miili yetu kwa wingi muda wote. Wataalamu wa afya wanapendekeza kutumia vitamini C kwa ajili ya kupunguza uwezekano wa kupata mafua na homa ya mafua mara kwa mara. Katika makala hii, tutachambua kwa kina kuhusu vitamini C, kuanzia maana yake, vyanzo vyake, kazi zake mwilini, dalili za upungufu, na athari za kuwa na vitamini C kupitiliza.
Vitamini C, kitaalamu pia hufahamika kama ascorbic acid au ascorbate. Ni vitamini inayoyeyuka kwenye maji na husaidia kukinga mwili dhidi ya maradhi ya kiseyeye (scurvy), ambayo ni hatari sana kwa afya. Ugunduzi wa vitamini C ulifanywa miaka ya 1920 na mwanasayansi Albert von Szent Györgyi. Mwanasayansi Kazimierz Funk ndiye aliyeeleza kwanza kuhusu maradhi yanayosababishwa na upungufu wa virutubisho mwilini, akitaja ugonjwa wa scurvy na kuupa virutubisho herufi C.
Baada ya ugunduzi wa Albert von Szent Györgyi, na tafiti za Haworth, kemikali iitwayo ascorbic acid ilipewa herufi C. Hivyo, herufi C kwenye vitamini C ina maana ya ascorbic acid. Wataalamu wa afya wanatueleza kuwa wanyama hawawezi kuishi bila ya vitamini C mwilini mwao. Vitamini C ndiyo vitamini ya kwanza kutengenezwa na binadamu kikemikali.
Kwa kuwa tumeshafahamu maana na historia ya vitamini C, hapa tutachambua vyanzo vya vitamini C. Vitamini C hupatikana kwenye matunda yenye ladha ya uchachu (citrus) na matunda yenye rangi ya njano, pamoja na mboga za majani.
Mbali na mboga za majani na matunda, pia unaweza kupata vitamini C kwa kula maini, maziwa, na mayai. Vidonge vya vitamini C pia ni chanzo kizuri.
Kama tulivyoona, vitamini C hulinda mwili dhidi ya mashambulizi na sumu za vyakula. Pia husaidia katika kulinda mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali kama kiseyeye, magonjwa ya ngozi, mifupa, na moyo. Katika kipengele hiki, tutaona kwa undani zaidi kuhusu kazi hizi za vitamini C mwilini.
Utengenezaji wa Collagen: Collagen ni protini muhimu kwa ajili ya utengenezaji wa tishu zinazojulikana kama connective tissues na kusaidia uponaji wa vidonda na majeraha. Mtu mwenye upungufu wa vitamini C vidonda vyake vitachelewa sana kupona ukilinganisha na mwenye vitamini C vya kutosha.
Antioxidant: Vitamini C ni antioxidant inayosaidia kulinda miili yetu dhidi ya mipambano ya kikemikali ya molekuli ndani ya miili yetu. Antioxidant husaidia katika uuguzi wa oksijeni mwilini na kupunguza sumu za vyakula mwilini.
Kinga ya Mwili: Vitamini C husaidia mfumo wa kinga mwilini kwa kuimarisha seli nyeupe za damu, zinazojulikana kama lymphocytes, ambazo ni askari wa mwili dhidi ya vimelea vya maradhi kama virusi, fangasi, protozoa, na bakteria.
Endapo kutatokea upungufu wa vitamini C mwilini, kuna athari kubwa zinazoweza kutokea, ikiwemo:
Kila kirutubisho kinahitajika ndani ya miili yetu kwa kiwango maalumu. Endapo kirutubisho kitakuwa kingi kupitiliza, athari zinaweza kutokea katika afya ya mtu. Miongoni mwa athari za kuwa na vitamini C kupitiliza ni kama zifuatazo:
Ugonjwa wa kiseyeye husababishwa na upungufu wa vitamini C mwilini. Dalili za ugonjwa huu huanza kutokea mwezi mmoja baada ya upungufu wa vitamini C kuanza kutokea mwilini. Dalili za ugonjwa wa kiseyeye ni pamoja na:
Vitamini C ni muhimu sana kwa afya ya binadamu. Hakikisha unakula vyakula vyenye vitamini C kwa wingi ili kuboresha afya yako na kuzuia maradhi mbalimbali. Endelea kujifunza na kuwa makini katika lishe yako ili kudumisha afya bora.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Katika somo hili uakwenda kujifunza faida za kiafya za kula fyulis
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula fenesi.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu faida za kiafya za kula tunda tufaha - apple
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula ubuyu
Soma Zaidi...Katika somo ili utakwenda kujifunza kuhusu faida za kiafya zakula maboga. Utajifunza virutubisho vinavyopatikana kwenye maboga.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula mbegu za matango
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza faida za kiafya za kula majani ya maboga ama majani ya mmboga
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz afaida za kiafya za kula supu ya kuku.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kutumia ndimu na limao
Soma Zaidi...Katika post hii utajifunza faida za kula mbegu za tikiti. Baada ya post hii utajifunza kuwa mbegu za tikiti hazitupwi.
Soma Zaidi...