image

Ana za vyakula somo la 37: Faida za kula njegere

Katika somo hili utakwend akujifunza faidaza kiafya za kula njegere

AIDA ZA KIAFYA ZA KULA NJEGERE

Njegere ni mboga jamii ya kunde. Njegere ni mboga tamu, kama hujawahi kuila, tafuta siku ujaribu. Mboga hii, mbali na utamu wake, imekuwa ikitajwa sana katika nyanja za afya. Hivi unazijua faida za kula njegere? Hakika, faida zake ni nyingi sana kiafya, kimwili, na hata kwa utamu. Makala hii inakuletea faida za kiafya za kula njegere.

Faida za Kula Njegere

  1. Virutubisho Vingi Njegere zina virutubisho vingi sana ukilinganisha na mboga nyingi. Njegere zina vitamini A, K, B, na C. Pia, njegere zina madini ya chuma, manganese, phosphorus, na folate. Njegere pia zina protini na nyuzinyuzi. Katika mboga, njegere ni mojawapo ya mboga zinazokusanya protini kwa wingi sana.

  2. Kudhibiti Kiwango cha Sukari Mwilini Njegere husaidia kudhibiti matumizi ya sukari mwilini. Hii husaidia kuwapa nafuu watu wenye kisukari aina ya pili (type 2 diabetes). Hali hii pia husaidia kuboresha afya ya moyo.

  3. Kuboresha Afya ya Mfumo wa Mmeng'enyo wa Chakula Kama unasumbuliwa na kukosa haja kubwa, njegere ndio mtatuzi wako. Njegere husaidia kuondoa vimbe zilizopo kwenye njia ya chakula na kufanya choo kiwe kizito na kupita kwa urahisi. Pia, njegere husaidia kuzuia saratani ya utumbo mpana na kusaidia kuondoa chakula chote kupitia haja.

  4. Kulinda Mwili Dhidi ya Maradhi Hatari Njegere husaidia kulinda mwili dhidi ya maradhi hatari kama saratani, maradhi ya moyo, na kisukari. Kwa sifa hii, njegere ni mboga pekee ambayo unatakiwa uile mara nyingi kwa lengo la kujikinga na maradhi haya. Hata hivyo, kwa ambaye ni mgonjwa tayari, mboga hii itamsaidia kupunguza uzito wa tatizo.

    A. Kuzuia Maradhi ya Moyo: Njegere zina madini ya magnesium, potassium, na calcium. Ulaji wa chakula chenye madini haya kwa wingi husaidia kuzuia shinikizo la juu la damu (presha ya kupanda) ambalo ndio chanzo kikuu cha maradhi ya moyo. Pia, ndani ya njegere kuna flavonols, carotenoids, na vitamini C. Pamoja, husaidia kupunguza uwezekano wa kupata maradhi ya moyo kwa sababu huzuia uharibifu wa seli.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-07-24 11:13:26 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 59


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Aina za vyakula somo la 35: Faida za kula mbaazi
Katika somo hili utakwend akujifunza faida za kiafya za kula mbaazi Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 62: Faida za kula topetope
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula topetope Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 16: Faida za kula chungwa na chenza
Katika somo hili utakwend akujifunza faida za kiafya za kula tunda la chungwa na chenza. Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 56: Faida za kula spinach
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula spinach Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 63: Faida za kula ubuyu
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula ubuyu Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 69: Faida za kula zaituni
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula zaituni Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 51: Faida za kula papai
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula papai Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 8: Vyakula vya vitamini C
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu vitmini C, kazi zake mwilini, na vyakula vya vitamini C. Soma Zaidi...

Ana za vyaula somo la 46: Faida za kula nazi
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula nazi Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 38: Faida za kula mahindi
Kkatika somo hil utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula mahindi Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 33: Faida za kula maharage
Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula maharagwe Soma Zaidi...

Aina za vyakula somo la 27: Faida za kula komamanga
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu faida za kiafya za kula komamanga Soma Zaidi...