Ana za vyakula somo la 37: Faida za kula njegere

Katika somo hili utakwend akujifunza faidaza kiafya za kula njegere

AIDA ZA KIAFYA ZA KULA NJEGERE

Njegere ni mboga jamii ya kunde. Njegere ni mboga tamu, kama hujawahi kuila, tafuta siku ujaribu. Mboga hii, mbali na utamu wake, imekuwa ikitajwa sana katika nyanja za afya. Hivi unazijua faida za kula njegere? Hakika, faida zake ni nyingi sana kiafya, kimwili, na hata kwa utamu. Makala hii inakuletea faida za kiafya za kula njegere.

Faida za Kula Njegere

  1. Virutubisho Vingi Njegere zina virutubisho vingi sana ukilinganisha na mboga nyingi. Njegere zina vitamini A, K, B, na C. Pia, njegere zina madini ya chuma, manganese, phosphorus, na folate. Njegere pia zina protini na nyuzinyuzi. Katika mboga, njegere ni mojawapo ya mboga zinazokusanya protini kwa wingi sana.

  2. Kudhibiti Kiwango cha Sukari Mwilini Njegere husaidia kudhibiti matumizi ya sukari mwilini. Hii husaidia kuwapa nafuu watu wenye kisukari aina ya pili (type 2 diabetes). Hali hii pia husaidia kuboresha afya ya moyo.

  3. Kuboresha Afya ya Mfumo wa Mmeng'enyo wa Chakula Kama unasumbuliwa na kukosa haja kubwa, njegere ndio mtatuzi wako. Njegere husaidia kuondoa vimbe zilizopo kwenye njia ya chakula na kufanya choo kiwe kizito na kupita kwa urahisi. Pia, njegere husaidia kuzuia saratani ya utumbo mpana na kusaidia kuondoa chakula chote kupitia haja.

  4. Kulinda Mwili Dhidi ya Maradhi Hatari Njegere husaidia kulinda mwili dhidi ya maradhi hatari kama saratani, maradhi ya moyo, na kisukari. Kwa sifa hii, njegere ni mboga pekee ambayo unatakiwa uile mara nyingi kwa lengo la kujikinga na maradhi haya. Hata hivyo, kwa ambaye ni mgonjwa tayari, mboga hii itamsaidia kupunguza uzito wa tatizo.

    A. Kuzuia Maradhi ya Moyo: Njegere zina madini ya magnesium, potassium, na calcium. Ulaji wa chakula chenye madini haya kwa wingi husaidia kuzuia shinikizo la juu la damu (presha ya kupanda) ambalo ndio chanzo kikuu cha maradhi ya moyo. Pia, ndani ya njegere kuna flavonols, carotenoids, na vitamini C. Pamoja, husaidia kupunguza uwezekano wa kupata maradhi ya moyo kwa sababu huzuia uharibifu wa seli.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aina za vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 550

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Ana za vyakula somo la 64: Faida za kula ukwaju

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula ukwaju

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 33: Faida za kula maharage

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula maharagwe

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 9: Vyakula vya vitamini D

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu vitamini D, kazi zake, vyanzo vyake na upungufu wake mwilini.

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 26: Faida za kula kitunguu saumu - garlic

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula kitunguu ssaumu - garlic

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 36: Faida za kula njugumawe

Katika somo hili utakwenda kjifunza faida za kiafya za kula njugumawe

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 2: Vyakula vya protini

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu vyakula vya protini, faida zake na vyanzo vyake.

Soma Zaidi...
Ana za vyaula somo la 46: Faida za kula nazi

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula nazi

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 45: Faida za kula nanasi

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula nanasi

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 17: Faida za kula embe

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula tunda embe

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 47: Faida za kula ndizi

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula nazi

Soma Zaidi...