Aina za vyakula somo la 11: Vyakula vya vtamini K

Aina za vyakula somo la 11: Vyakula vya vtamini K

katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu vitamini K, kazi zake mwilini, athari za upungufu wake, na vyakula vyenye vitamini K kwa wingi

Download Post hii hapa

Vitamini K na Faida Zake Mwilini

Vitamini K ni moja ya vitamini ambavyo miili yetu inavihitaji kwa ajili ya shughuli mbalimbali muhimu. Endapo upungufu wa vitamini hii utatokea, madhara makubwa ya kiafya yanaweza kumkumba mtu. Katika makala hii, tutaangalia zaidi kuhusu vitamini K, vyanzo vyake, kazi zake mwilini, athari za upungufu wake, na athari za kuzidi kwa vitamini K mwilini.

Yaliyomo:

  1. Nini Maana ya Vitamini?
  2. Vitamini K ni Nini?
  3. Wapi Nitapata Vitamini K?
  4. Ni Zipi Kazi za Vitamini K?
  5. Ni Zipi Athari za Upungufu wa Vitamini K?
  6. Ni Zipi Athari za Kuzidi kwa Vitamini K?

 

Nini Maana ya Vitamini?

Vitamini ni kampaundi za ogania ambazo zinahitajika na mwili kwa ajili ya ukuaji na utendaji wa michakato ya kibaiolojia ndani ya miili yetu (metabolism). Ni virutubisho ambavyo havitengenezwi ndani ya miili yetu. Vitamini vipo katika makundi mawili makuu: fat-soluble (hupatikana kwenye mafuta) na water-soluble (hupatikana kwenye maji).

 

Vitamini K ni Nini?

Vitamini K ni vitamini katika kundi la fat-soluble ambazo zimetokana na kampaundi za naphthoquinone. Vitamini hivi vimeitwa K kutokana na neno la lugha ya Danish "koagulation" ambalo lina maana ya "coagulation" kwa Kiingereza, yaani kuganda. Hii ni kwa sababu vitamini K inahitajika mwilini kusaidia mchakato wa kuganda kwa damu pindi mtu anapopata jeraha.

Kwa mara ya kwanza vitamini K vilianza kuandikwa kwenye maandishi na mwanasayansi wa Danish Henrik Dam mwaka 1929 alipokuwa akifanya tafiti juu ya kazi za cholesterol mwilini. Wataalamu wa lishe wameigawa vitamini K katika makundi mawili: K1 na K2. Vitamini K1, kitaalamu huitwa phytonadione, hupatikana kwenye mboga za majani, na vitamini K2, kitaalamu huitwa menaquinone, hupatikana kwenye nyama, mayai, na maziwa.

 

Wapi Nitapata Vitamini K?

Vitamini K1:

 

Vitamini K2:

 

Ni Zipi Kazi za Vitamini K?

1. Kuganda kwa Damu:

Hii ndiyo kazi kuu ya vitamini K. Pindi unapopata jeraha lolote ambalo litapelekea damu kutoka, vitamini K huhakikisha damu inaganda na kusimamisha kutokwa na damu. Vitamini K hutumika katika kutengeneza prothrombin, factors VII, IX, pamoja na X, ambazo zote huitwa clotting factors na husaidia kusimamisha damu isiendelee kutoka kwenye jeraha.

2. Afya ya Mifupa:

Vitamini K husaidia katika kuboresha afya ya mifupa kwa kudhibiti ujazo na tungamo la mifupa na kuzuia mifupa kuwa midhaifu na kupasuka kwa urahisi (osteoporosis). Tafiti zinaonyesha kuwa vitamini K ni muhimu katika kulinda mifupa dhidi ya maradhi haya.

3. Afya ya Ubongo na Kumbukumbu:

Tafiti zinaonyesha kuwa watu wenye umri wa zaidi ya miaka 70 ambao wana vitamini K vya kutosha kwenye damu zao wana uwezo mkubwa wa kukumbuka kuliko wale wenye upungufu wa vitamini K.

4. Afya ya Moyo:

Vitamini K husaidia kushusha presha ya damu kwa kuzuia kuganda kwa madini ndani ya mishipa ya damu. Hii husaidia moyo kusukuma damu bila matatizo na kupunguza athari za kupata stroke (kupooza).

5. Kulinda Mwili Dhidi ya Saratani:

Baadhi ya waandishi wanaeleza kuwa vitamini K husaidia kulinda mwili dhidi ya vimbe za saratani, lakini bado hakuna ushahidi wa kisayansi wa kutosheleza kuthibitisha madai haya.

 

Ni Zipi Athari za Upungufu wa Vitamini K?

 

Ni Zipi Athari za Kuzidi kwa Vitamini K?

Ijapokuwa vitamini K vina faida kubwa ndani ya miili yetu, vikizidi mwilini vinaweza kusababisha madhara ya kiafya kama:

 

Hitimisho

Vitamini K unaweza kuvipata kwa njia ya chakula au kwa kumeza vidonge. Kwa wale ambao wana upungufu wa vitamini K, vidonge vinaweza kununuliwa kwa kufuata maelekezo ya daktari. Ni muhimu kufuatilia makala nyingine za afya ili kupata maarifa zaidi na kudumisha afya bora kwa kutumia vitamini na virutubisho sahihi.

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aina za vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 377

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Faida za kiafya za kula mbegu za maboga mwilini
Faida za kiafya za kula mbegu za maboga mwilini

Katika somo hili utakwenda kujufunza faida za kiafya za kula mbegu za maboga katika mwili wako

Soma Zaidi...
Vyakula somo la 71: Faida za kiafya za kula Mchicha
Vyakula somo la 71: Faida za kiafya za kula Mchicha

Katika somo hili utajifunza Faida za kiafya za kula Mchicha

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 33: Faida za kula maharage
Aina za vyakula somo la 33: Faida za kula maharage

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula maharagwe

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 42: Faida za kunywa chai ya mcaichai
Aina za vyakula somo la 42: Faida za kunywa chai ya mcaichai

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kutumia mcaihai kwenye chai yako

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 9: Vyakula vya vitamini D
Aina za vyakula somo la 9: Vyakula vya vitamini D

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu vitamini D, kazi zake, vyanzo vyake na upungufu wake mwilini.

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somola 18: Faida za kula tufaha - apple
Aina za vyakula somola 18: Faida za kula tufaha - apple

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu faida za kiafya za kula tunda tufaha - apple

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 62: Faida za kula topetope
Aina za vyakula somo la 62: Faida za kula topetope

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula topetope

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 14: Faida za kula Maboga
Aina za vyakula somo la 14: Faida za kula Maboga

Katika somo ili utakwenda kujifunza kuhusu faida za kiafya zakula maboga. Utajifunza virutubisho vinavyopatikana kwenye maboga.

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 48: Faida za kula nyama
Aina za vyakula somo la 48: Faida za kula nyama

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula nyama

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 55: Faida za kula senene panzii na kumbikumbi
Aina za vyakula somo la 55: Faida za kula senene panzii na kumbikumbi

Katika somo hili utakwenda kujifunza faida za kiafya za kula senene, panzi na kumbikumbi

Soma Zaidi...