picha

Kujiepusha na kula mali ya Yatima

Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).

Kujiepusha na kula mali ya Yatima

(f)Kujiepusha na kula mali ya Yatima



Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).



Katika aya ya (17:34) tunakatazwa hata kukurubia mali ya yatima kwa maana ya kwamba tusithubutu kuchanganya mali zao na zetu kwa kisingizio chochote kile na tusizitumie hata kwa matumizi yao wenyewe iwapo tunao uwezo wa kuwalea pasina kuhitajia mali zao:


"Na wapeni mayatima mali zao wala msibadilishe kibaya kwa kizuri. Wala msile mali zao pamoja na mali zenu. Hakika (yote) hayo ni jukumu kubwa." (4:2)



β€œNa waogope (Mawasii kuwadhulumu mayatima; na wakumbuke) kama na wao wangewacha nyuma yao watoto madhaifu wangekuwa na khofu juu yao; basi wamwogope Mwenyezi Mungu na waseme maneno yaliyo sawa (kwa hao mayatima waliousiwa kuwatazama). Hakika wale ambao wanakula mali ya may atima kwa dhuluma, bila shaka wanakula moto matumboni mwao; na wataungua katika huo Moto (wa jahannam) uwakao.” (4:9-10)




                   


Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 2174

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Mitume wa uongo

Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s.

Soma Zaidi...
Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah

Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe).

Soma Zaidi...