Kupanga uzazi na uzazi wa mpango katika uislamu

Kupanga uzazi na uzazi wa mpango katika uislamu

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kupanga uzazi na uzazi wa mpango katika uislamu

Kupanga Uzazi katika Uislamu



Kama ilivyo haramishwa kwa jamii, Uislamu umeharamisha pia kudhibiti uzazi kwa mtu binafsi kwa khofu ya kushindwa kuwalisha au visingizio vingine. Hata hivyo Uislamu haujawataka watu wazae kiholela. Kwanza umekataza watu kuzaana nje ya ndoa. Pili, walioona wanatakiwa wazingatie umri baina ya mtoto na mtoto mwingine. Kwa anayetaka kukamilisha muda wa kunyonyesha, basi amnyonyeshe mtoto wake kwa miaka mwili:


Na wanawake waliozaa wawanyonye.she watoto wao miaka miwili kainilz kwa anayetaka lwkamilisha lwnyonyesha..." (2:233)



Kunyonyesha humsababisha mama mzazi kuchukua muda mkubwa kabla ya kuingia tena katika siku zake. Iwapo mwanamke atapata siku zake wakati mtoto yungali mchanga (hajafikia umri wa miaka miwili), anatakiwa ajizuie asipate mimba; kwani katika Hadith iliyosimuliwa na Imamu Muslim, Mtume (s.a.w) amesema kuwa mwanamke akipata mimba wakati yungali na mtoto mchanga, afya ya mtoto hudhurika. Njia za kuzuia mimba katika kipindi hiki cha kunyonyesha ni zile ambazo hazina madhara ya kiafya kwa baba wala mama. Katika Hadith iliyopokelewa na Bukhari na Muslim, Jabir (r.a) amesema kuwa wakati wa Mtume (s.a.w) wao walikuwa wanatumia njia ya kuzuia mimba inayoitwa 'azal" (with drawal au coitus interuptus), yaani njia ya kumwaga mbegu za uzazi nje lakini Mtume (s.a.w) hakuikataza.



Hapa ifahamike kwamba suala Ia kupanga juu ya muda wa kunyonya mtoto linamhusu baba na mama na si suala Ia kuwekewa sera na taifa; kwani hali za watu zinatafautiana.



Ama kwa mama atakayekuwa na matatizo ya kiafya, ikathibiti kuwa akibeba mimba atadhurika au kuhatarisha maisha yake, anaruhusiwa kufunga kizazi hata kutoa mimba ambayo imeshatunga.



Hitimisho juu ya Kudhibiti uzazi
Tumeona kuwa kuongezeka kwa watu si tatizo kwani hakuna tatizo Ia riziki kama wale wasiomtegemea Allah (s.w) wanavyodai. Hivyo, kuwapangia watu wazae watoto idadi Fulani ni kinyume kabisa na mafundisho ya Uislamu. Wajibu wa mwanadamu ni kufanya kazi kwa bidii na maarifa, na pia kuweka utaratibu mzuri wa mgao wa rasilimali katika jamii.



Uislamu umekemea vikali zinaa na kuweka adhabu kali kwa wazinifu. Sera ya kudhibiti uzazi na Elimu ya ngono (sex education) ni nyenzo "nzuri sana na madhubuti" za kupalilia zinaa katika jamii. Katu waislamu hawatazikaribisha. Huu ndio msimamo wa Uislamu juu ya suala Ia kudhibiti uzazi na waislamu wa kweli daima watakuwa katika msimamo huu kwani:


Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume, hakika amepotea upotofu ulio wazi kabisa. (33:36)





                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1568

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mifano na namna ya kurithisha
Mifano na namna ya kurithisha

Ugawaji wa mirathi-Mume ana nusu (1/2) = 1/2 -Mama ana sudusi.

Soma Zaidi...
Haki za kiuchumi za mwanamke katika uislamu
Haki za kiuchumi za mwanamke katika uislamu

Haki za UchumiKuwa imara kiuchumi ni sababu mojawapo kubwa ya kumpa mtu hadhi katika jamii.

Soma Zaidi...
Sanda ya mwanamke na namna ya kumkafini
Sanda ya mwanamke na namna ya kumkafini

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Swala ya tahiyatul masjidi yaani maamkizi ya msikitini,  pamoja na swala za qabliya na baadiya
Swala ya tahiyatul masjidi yaani maamkizi ya msikitini, pamoja na swala za qabliya na baadiya

Post hii inakwenda kukujuza kuhusu swala za qabliya, baadiya na tahiyatul masjid.

Soma Zaidi...
Milki ya raslimali katika uislamu
Milki ya raslimali katika uislamu

Milki ya RasilimaliIli kujipatia maendeleo ya kiuchumi katika zama zote mwanaadamu anahitaji rasilimali za kumwezesha kufikia azma hiyo.

Soma Zaidi...