image

Bongoclass ni nini, ipo wapi bongoclass na ni zipi kazi zake?

Bonoclass ni muunganiko wa maneno mawili, kutoka katika lugha mbili yaani lugha ya kiingereza na lugha ya kiswahili.

Bongoclass ni nini, ipo wapi bongoclass na ni zipi kazi zake?

MUKHTASARI KUHUSU BONGOCLASS

Utangulizi

Bonoclass ni muunganiko wa maneno mawili, kutoka katika lugha mbili yaani lugha ya kiingereza na lugha ya kiswahili. Maneno hayo ni “bongo” kutoka katika lugha ya kiswahili na “class” kutoka katika lugha ya kiingereza. Neno “bongo” maana yake kwa lugha ya kiswahili ni ubongo, akili au maarifa. Na neno class katika lugha ya kiingereza ni darasa. Muunganiko wa maneno haya mawili ndipo tunapata bongoclass.


Nini maana ya bongoclass?


Kilugha kama tulivyoona hapo juu bongoclass ni darasa la kutumia akili na maarifa. Kulingana na malengo ya tovuti hii neno bongoclass lina maana kuu zifuatazo:
1.Bongoclass ni darasa la kutumia akili na maarifa
2.Ni darasa linaloshirikisha akili na maarifa kutoka watu mbalimbali
3.Bongoclass ni darasa la kutumia akili na maarifa katuka kutatua matatizo na changamoto
4.Bongoclass ni darasa la kutumia maarifa katika kuingiza kipato
5.Bongoclass ni darasa la kutumia akili na maarifa katika kutumia fursa zilizopo.


Bongoclass ni nini hasa?


Kama utachanganya maana zilizopo hapo juu kwa pamoja unaweza kupata maana halisi ya bongoclass kwa mujibu wa tovuti hii. Kwa hivyo tunasema kuwa:-


Bongoclass ni darasa la kushiriika akili na maarifa kutoka kwa watu mbalimbali katika kutumia fursa zilizopo ili kuzalisha kipato na kuleta maendeleo katika jamii.


Hiyo ndiyo maana halisi ya bongoclass kwa mujibu wa tovuti hii. Maana hii itaendelea kutumika kwenye blog zetu nyingine na kwenye huduma zetu nyingine. Bongoclass tunashirikiana na wadau mblimbali na lengo letu kuu ni kuleta maendeleo katika jamii kwa kiasi tutakachoweza.


Tunatumia jina hili katika social media kama bongoclass kwenye facebook, instagram, twitter na youtube. Tutaendelea kutumia jina hili katika maeneo yeyote ambayo huduma zetu zitaweza kupatikana. Ukiwa na maoni ama mapendekezo na maswali wasiliana nasi kwa mawasiliano yetu. Bofya hapa kupata mawasiliano



HUDUMA ZETU


Kama maelezo ya hapo juu yanavyojieleza yenyewe kuwa tunatowa huduma ya kielimu katika jamii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali. Na huduma hii inatolewa bure bila hata ya malipo yeyote. Kwa ufupi wa maneno zifuatazo ndizo huduma ambazo bongoclass inatoa:-


Kutoa elimu katika jamii kuhusu maswala yote ya afya, afya ya uzazi na mlo kamili, elimu ya dini, elimu kuhusu matumizi ya sayansi na teknolojia, elimu kuhusu sayansi ya viumbe na kilimo, pia tunatoa msaada kwa wanafunzi wa mashuleni. Mwisho tunatoa elimu inayochangamsha akili kama game, maswali na nahau, methali na vitendawili bila kusahau chemshabongo.


Tunatoa burudani kwa watu wa rika zote. Burudani tunayotoa ni utunzi wa hadithi tamu na murua zinazoweza kusomwa na watu wa rika zote. Bila kusahau chemshabongo ambazo huburudisha na kuchangamsha akili. Tunakupatia game rahisi kuzicheza.


Tunaunga, kutengeneza na kusambaza vitabu kupitia tovuti yetu na blog yetu. Vitabu hivi ni vya bure. Ni vijijarida vidogo vilivyokusanya mada zihusuzo afya, dini na burudni. Unaweza kudownload moja kwa moja ndani ya tovuti hii bila hata malipo.


Tunatengeneza tovuti na kuboresha, tunafungua blog na kuziporesha. Hapa tunalenga kuwasaidia mablogger walio wachanga katika ujuzi huu. Lengo letu ni kusaidia maendeleo ya sayansi na teknolojia yaweze kufika mbali kwa kutumia lugha ya kiswahili.


Tunatengeneza App za android. Hii ni kwa ajili ya bishara. Hapa tunakwenda kuwasaidia wafanyabiashara kuweza kufikia malengo yao ya kukuza majina yao, kampuni na kuwafikia walengwa kwa urahisi kabisa kupitia simu za mkononi.


Tunatangaza matangazo mbalimbali katika blog na tovuti yetu. Ukiwa wewe ni mfanyabishara na unataka biashara yako ifikie mamia maelfu ya watu. Bongoclass ndio sehemu sahihi kwako. Tutakutangazia biashara yak na utaweza kufikia walengwa wako kwa urahisi zaidi.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 320


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Njia za kuwasiliana na Bongoclass
wasiliana nasi muda wowote kupitia mitandao yetu Soma Zaidi...

Books
Vinjari ukiwa na vitabu vyetu ukiwa kwenye maktaba yetu Soma Zaidi...

bongoclass health
1. Soma Zaidi...

Bongoclass ni nini, ipo wapi bongoclass na ni zipi kazi zake?
Bonoclass ni muunganiko wa maneno mawili, kutoka katika lugha mbili yaani lugha ya kiingereza na lugha ya kiswahili. Soma Zaidi...

ZOEZI
Zoezi la 1 (a) Ainisha maana ya sunnah kilugha na kisheria. Soma Zaidi...

Kitabu Cha ayansi ya viumbe
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

MAKTABA YA VIBABU KUTOKA BONGOCLASS
Soma Zaidi...

Vitabu
VITABU: Karibu kwenye Maktaba yetu ya vitabu, hapa utaweza kusoma na kudownload vitabu vyetu bure. Soma Zaidi...

Tembo ni katika wanyama wenye kushangaza sana.
Tembo wana maajabu makubwa kama utazingatia kwa umakini umbo lake zuri. Soma Zaidi...

MNYAMA ANAYEKIMBIA ZAIDI YA WOTE
4. Soma Zaidi...

TUNAKUTAKIENI RANADHANI MUBARAKA
Wikibongo inawatakia waislamu wote heri ya mfungo wa ramadhaji Soma Zaidi...

MAKTABA YA VITABU
Soma Zaidi...