Somo la 4 Python sqlite: Jinsi ya kuingiza data kwenye table na database

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuingiza data kwenye table na database tuliyoiunda katika somo lililopita

Somo la 4 Python sqlite: Jinsi ya kuingiza data kwenye table na database

INSERT ndio roho ya kuanza kujaza database na kufanya iwe na maana. Tumeunda kabati la faili (database) na droo (meza), sasa ni wakati wa kuweka taarifa zetu za kwanza.

 


 

Kuelewa Syntax: INSERT INTO

 

Amri ya INSERT INTO ndio tunayotumia kuongeza mstari mpya (record) kwenye meza yetu. Muundo wake wa jumla unaonekana hivi:

INSERT INTO jina_la_meza (safu1, safu2, ...) VALUES (thamani1, thamani2, ...);

Katika Python na SQLite, hatutumii amri hii moja kwa moja. Badala yake, tunatumia placeholders (?) ili kuzuia mashambulizi ya kiusalama yanayojulikana kama SQL Injection. Njia hii ni salama zaidi na inafaa zaidi kwa programu.

Unda faili jipya liite insert.py kisha paste code hizi. 

NB: Ni vizuri kuandika mwenyewe ili kupata uzoefu thabiti.

import db_conn as dbConn

def InsertData(name:str, takenBy:str, quantity:int, location:str, price:int):
    connection = dbConn.get_connection()
    pointer = connection.cursor()
    query = """
    INSERT INTO products (name, taken_by, quantity, location, price) VALUES (?, ?, ?, ?, ?)
    """
    data = (name, takenBy, quantity, location, price)
    pointer.execute(query, data)
    connection.commit()
    connection.close()
    print('Taafifa zimeifadhiwa kikamilifu')
   
   
def getUserData():
    try:
         Name = input('Ingiza jina la bidhaa > ')
         TakenBy = input('Jina la mdeni > ')
         Quantity = int(input('Kiasi cha bidhaa > '))
         Location = input('Eneo la mdeni > ')
         Price = int(input('Bei ya bidhaa > '))
         
         InsertData(Name, TakenBy, Quantity, Location, Price)
         
    except ValueError as error:
        print(f'Kosa: {error}')

getUserData()
 

Kuvunja Msimbo na kuelewa Kila Kazi

 

Hebu tuchambue code ili kuelewa kila sehemu.

 

1. Kazi ya InsertData()

 

Kazi hii inachukua data kutoka kwa mtumiaji na kuihifadhi kwenye database.

 

2. Kazi ya getUserData()

 

Kazi hii inasimamia mchakato wa kupokea data kutoka kwa mtumiaji.

 

Mambo ya msingi kufahamu

Unapaswa kuelewa kwamba kuna hatua tatu muhimu za kufanya kazi na database:

  1. Muunganiko na Cursor: Kwanza, unahitaji kuunganisha na database na kupata cursor.

  2. Kutekeleza Amri: Pili, unatumia cursor kutekeleza amri za SQL kama INSERT.

  3. Kuhifadhi Mabadiliko: Mwisho, unatumia commit() kuhifadhi mabadiliko na close() kufunga muunganiko.

VIDEO TUTORIALl: 👇

Tazama au Download video hapa

MWISHO:

Katika somo linalofuata tutajifunza namna ya kusoma data kutoka kwenye database yetu

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Emmanueli image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: Python Database Main: ICT File: Download PDF Views 53

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 web hosting    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Somo la 6 python sqlite: Jinsi ya kusasisha (UPDATE) data kutoka kwenye database

Karibu kwenye somo la sita! Leo tunajifunza UPDATE, amri ambayo inaruhusu kubadili au kusasisha data iliyopo tayari kwenye meza (table) yetu. 

Soma Zaidi...
Somo la 9 Python sqlite: Jinsi ya kuiweka project yetu kwenye file moja

Katika somo hili utaenda kujifunza namna ya kuunganisha mafaili mengi ya project na kuyaweka kwenye faili moja tu na kuweza kufikia faili zote kwa kupitia faili moja pekee

Soma Zaidi...
Somo la 7 Python Sqlite: Jinsi ya kufuta data kwenye database

Katika somo hili utakwenda kujifunza namna bora ya kufuta data kutoka kwenye database

Soma Zaidi...
Somo la 5 Python Sqlite: Jinsi ya kusoma (Read) data kutoka kwenye database

Katika somo hili tutaenda kujifunza jinsi ya kusoma (Read) data kutoka kwenye database yetu

Soma Zaidi...
Somo la 1: Utangulizi wa SQLITE na jinsi ya kuitumia katika python

Katika somo hili tutajifunza utangulizi wa SQLITE na jinsi ya kuitumia katika python

Soma Zaidi...
Somo la 8 Python Sqlite Jinsi ya kupata jumla ya madeni kutoka kwenye database

Katika Somo hili la nane utaenda kujifunza namna ya kuchambua data kwenye database yetu kwa kupata jumla ya kiasi cha fedha kilichokopwa

Soma Zaidi...
Somo la 3 python sqlite: Jinsi ya kuunda table kwenye database ya SQLITE na Python

Katita somo hili sasa tutaenda kujifunza namna ya kuunda table kwenye database ya SQLITE kwa kutumia Python

Soma Zaidi...
Somo la 2 Python Sqlite na muunganiko wa Database (Database Connection)

Karibu ujifunze Python Sqlite na muunganiko wa Database (Database Connection)

Soma Zaidi...