Katita somo hili sasa tutaenda kujifunza namna ya kuunda table kwenye database ya SQLITE kwa kutumia Python
Somo la 3 python sqlite: Jinsi ya kuunda table kwenye database ya SQLITE na Python
Baada ya kujua jinsi ya kuunda database, hatua inayofuata ni kuunda meza (table) ndani yake. Fikiria database kama faili la kuhifadhia (file cabinet), na meza ndiyo droo unayoweka data yako. Kila droo ina sehemu zake maalum za kuandikia vitu, ambazo tunaziita safu (columns).
CREATE TABLE IF NOT EXISTS products: Hii ndio amri inayoanzisha uundaji wa meza.
CREATE TABLE inaiambia database "tengeneza meza".
IF NOT EXISTS inahakikisha kwamba kama meza ya products tayari ipo, amri hii itapuuzwa na hakuna kosa (error) litatokea. Hii ni njia nzuri ya kuzuia makosa unaporun msimbo mara nyingi.
products ni jina la meza yetu.
Ndani ya mabano (...), unaeleza muundo wa meza yako, ukiorodhesha kila safu (column) na aina ya data (data type) itakayoifadhiwa.
id INTEGER PRIMARY KEY AUTOINCREMENT: Hii ndio safu ya kwanza, ya id.
INTEGER ni aina ya data inayohifadhi namba kamili.
PRIMARY KEY inamaanisha id ni kitambulisho cha kipekee kwa kila mstari (row) katika meza. Hakuna mistari miwili inayoweza kuwa na id sawa.
AUTOINCREMENT inamaanisha id itajiongeza yenyewe kwa namba moja kila unapoongeza bidhaa mpya. Huwezi kuiandika mwenyewe.
name TEXT: Hii ni safu ya kuhifadhi jina la bidhaa. TEXT inaashiria kuwa data itakuwa maandishi (k.m., "Simu," "Laptop").
taken_by TEXT: Safu ya kuhifadhi jina la mtu aliyechukua bidhaa. Aina ya data ni TEXT.
quantity REAL: Hii inahifadhi idadi ya bidhaa kama namba kamili au desimali mfano (0.5). Aina ya data ni REAL Kwani inapokea flot points.
location TEXT: Safu ya kuhifadhi eneo la bidhaa kama maandishi. Aina ya data ni TEXT.
price INTEGER: Hii inahifadhi bei ya bidhaa kama namba kamili. Aina ya data ni INTEGER.
SQLite inasaidia aina tano za data, ambazo zinatumika kufafanua ni aina gani ya habari itakayohifadhiwa kwenye kila safu.
NULL: Hii inaashiria kwamba thamani ya safu ni haipo au ni batili.
REAL: Hii inahifadhi namba za desimali (decimal numbers). Kwa mfano, 3.14, 25.5. Ungeitumia kwa bei au hesabu zinazohitaji desimali.
BLOB: Hii inasimama kwa "Binary Large Object." Inatumika kuhifadhi data ya binary kama vile picha, sauti, au faili zingine. Data hii haisomeki kama maandishi.
VIDEO TUTORIAL: 👇
MWISHO:
Katita somo linalofuata tutaenda kujifunza jinsi ya kuweka data kwenye table ndani ya database
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Trojan ni Moja ya maneno tunayoyasikia sana kwneye tehama. Leo nitakupa maana yake
Soma Zaidi...Katika kompyuta, worm ni aina ya programu hasidi (malware) inayojinakili yenyewe na kusambaa kupitia mitandao bila kuhitaji kushikamana na faili au programu nyingine. Tofauti na virusi, worm husambaa haraka zaidi na mara nyingi hutumia mtandao kuenea.
Soma Zaidi...Virusi vya kompyuta ni programu hasidi (malware) inayojishikiza kwenye faili au programu halali na kujiendesha pale faili hiyo inapofunguliwa. Virusi vinaweza kuharibu data, kupunguza kasi ya kompyuta, au kusababisha upotevu wa taarifa.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu HDD (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive)
Soma Zaidi...Zani ilikuwa sehemu ya ku comment ni muhimu sana kwenye blog, ila Sasa sehemu hii imeondolewa kwenye blog nyingi. Ni Kwa nini hasa imeondolewa. Post hii itakujibu swali hilo
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza utaratibu unaotumiwa kuweka matoleo kwnye software.
Soma Zaidi...Tupo katika kipindi ambacho, tafiti nyingi zinahitajika kuhusu athari za AI kwenye ubunifu na taaluma.
Soma Zaidi...RAM (Random Access Memory) na ROM (Read-Only Memory) ni aina za kumbukumbu kwenye kompyuta au vifaa vya kielektroniki, lakini zina malengo na tabia tofauti.
Soma Zaidi...Post hii utakwenda kujikitabzaidi kujibu swali, hata hivyo itambulike kuwa wengi wa wanasayansi waliohusika kwenye lugha hizi sio wamarekani.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza utangulizi wa SQLITE na jinsi ya kuitumia katika python
Soma Zaidi...