Somo la 1: Utangulizi wa SQLITE na jinsi ya kuitumia katika python
Katika somo hili tutajifunza utangulizi wa SQLITE na jinsi ya kuitumia katika python
Somo la 1: Utangulizi wa SQLITE na jinsi ya kuitumia katika python
1. SQLite Ni Nini?
SQLite ni database engine ambayo inapatikana kama library moja tu. Huwezi kuhitaji ku-install database server yoyote tofauti. Badala yake, database nzima inahifadhiwa kwenye faili moja kwenye kompyuta yako. Hii inafanya iwe rahisi sana kuanza nayo kwa sababu hakuna setup ya ziada inayohitajika.
-
Faida: Ni ndogo, inafanya kazi haraka, na ni rahisi kutumia. Inakuja pamoja na Python, hivyo huna haja ya kui-download tena.
-
Matumizi: Inafaa sana kwa ajili ya programu ndogo ndogo za desktop, mobile apps, na kwa kujifunzia.
2. import sqlite3 Inafanya Kazi Gani?
-
Lengo: Amri ya import sqlite3 inaiambia Python iandae moduli (module) ya sqlite3 ili tuweze kuitumia kuwasiliana na database yetu ya SQLite. Fikiria kama unafungua sanduku la vifaa ambalo lina zana zote za kufanya kazi na database.
3. Kazi Muhimu za Moduli ya sqlite3
Moduli hii ina kazi mbili kuu utakazozitumia mara kwa mara:
-
sqlite3.connect('jina_la_db.db'): Hii ndio kazi ya kwanza kabisa utakayotumia. Inafanya muunganiko (connection) na database.
-
Ikiwa faili ya jina_la_db.db haipo, Python inaiunda moja kwa moja.
-
Ikiwa faili ipo, Python inaifungua na kuungana nayo.
-
Kutoka hapa, unaunda object inayoitwa conn (mfano wa connection) ambayo ndiyo utatumia kufanya kazi nyingine zote.
-
conn.cursor(): Cursor ni kama pointer au mshale unaotumika kutekeleza amri za SQL kwenye database. Baada ya kuunda connection, unatumia amri hii kupata cursor na kuanza kufanya shughuli kama vile kuunda meza (tables), kuongeza data (INSERT), au kusoma data (SELECT).
Muhimu:
Katika subtopic hii ya PYTHON na SQLITE tutajifunza kwa vitendo zaidi ili kuimarisha ujuzi wetu. Vitendo vya kujifunza tutajikita kwenye kuunda CRUD rahisi (CREATE, READ, UPDATE and DELETE) Kwani ndio msingi wa programming yoyote katika ulimwengu wa coding.
Mwisho:
Somo litakalofuata tutasoma kwa undani zaidi ni kwa namna gani tunaweza kuanza kuitumia Sqlite kwenye python.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Somo la 4 Python sqlite: Jinsi ya kuingiza data kwenye table na database
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuingiza data kwenye table na database tuliyoiunda katika somo lililopita
Soma Zaidi...Somo la 6 python sqlite: Jinsi ya kusasisha (UPDATE) data kutoka kwenye database
Karibu kwenye somo la sita! Leo tunajifunza UPDATE, amri ambayo inaruhusu kubadili au kusasisha data iliyopo tayari kwenye meza (table) yetu.
Soma Zaidi...Somo la 7 Python Sqlite: Jinsi ya kufuta data kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza namna bora ya kufuta data kutoka kwenye database
Soma Zaidi...Somo la 9 Python sqlite: Jinsi ya kuiweka project yetu kwenye file moja
Katika somo hili utaenda kujifunza namna ya kuunganisha mafaili mengi ya project na kuyaweka kwenye faili moja tu na kuweza kufikia faili zote kwa kupitia faili moja pekee
Soma Zaidi...Somo la 3 python sqlite: Jinsi ya kuunda table kwenye database ya SQLITE na Python
Katita somo hili sasa tutaenda kujifunza namna ya kuunda table kwenye database ya SQLITE kwa kutumia Python
Soma Zaidi...Somo la 5 Python Sqlite: Jinsi ya kusoma (Read) data kutoka kwenye database
Katika somo hili tutaenda kujifunza jinsi ya kusoma (Read) data kutoka kwenye database yetu
Soma Zaidi...