SAMAKI WA AJABU

Download kitabu Hiki Bofya hapa SAMAKI WA AJABU Walikwenda upane wa magharibu na mji wakauacha upande wa kusini.

SAMAKI WA AJABU


Download kitabu Hiki Bofya hapa

SAMAKI WA AJABU

Walikwenda upane wa magharibu na mji wakauacha upande wa kusini. Walikwnda kwa muda usiopunguwa masaa saba. Kisha wakakutana na milima minne. Wakaipanda milima ile juu ya milima wakakuta kuna kijibwawa cha maji yaliyo meupe sana. Kisha jini akamwambia mvuvi atupe nyavu yake. Alipotupa akavuwa samaki wanne wa rangi tofauti. Mvuvi alishangaa hajawahi ona samaki wenye umbo na rangi kama hizi maishani kwakwe. Kisha jini likamwambia โ€œchukuwa samaki hawa na ukawauze kwa mfalme, utapata utajiri bila shaka. Ila kumbuka utavua hapa kwa siku mara moja tu?โ€ kisha jini likapiga miguu yake chini na kupotea.

Mvuvi akatoka na samaki wake wale na akakutana na mpishi wa mfalme, mpishi akawachukuwa samaki wale mpka kwa mfalme. Mfalme alishangaa uzuri ulioje wa samaki wale. Akawanunua kwa pesa nyingi sana iliyomfanya mvuvi asahau maisha ya kimasiki jitena. Mpishi akatoka kwendapika samaki wale. Akaanza kuwakaanga , pindi walipoanza kuiva, upande mmoja akawageuza ghafla akashangaa ukuta wa jiko umepasuka na kukatokea mwanamke mzuuri. Mwanamke yule akaaambia samaki โ€œje mnafanye kazi niliyo watuma?โ€ samaki wakamjibu โ€œndio tunafanya kazโ€ kisha mwanamke yule akapiga teke karai lile na samaki wakaanguka na kugeuka mkaa. Baada ya hapo akapoka na ukuta ukarudi ukawa kama vile ulivyokuwa.

Matukio yote haya yakifanyika mpishi aliyaona, na alikuwa akishangaa. Zaidi ni pale alipoona samaki wa mfalme wamegeuka mkaa, aliogopa sana na akatoka kumtafuta mvuvi ili amwambie amletee wengine. Kwa kuwa mvuvi aliwauza wawili akampatia wale wawili walobakia kwa pesa nyingi sana. Kisha mpishi akaenda jikoni. Tukio lielile likatokea tena na samaki wakageuka mkaa. Mara hii aliamua kumweleza mfalme mfalme alishangaa sana na kaamrisha aletwe mvuvi. Mvuvi alipofika akampewa amri ya kuleta samaki kama wale siku itakayofata.

Mambo yakawa kama hivi siku ilofata mvuvi akawaleta samaki wale na akapewa pesa kama ile ya jana mara mbili yake maana amempa wote wanne. Mfalme akaingia jikoni mwenyewe na akaanza kuwakaanga. Tukio kama la jana likatokea tena na samaki wakageuka mkaa. Sasa mfalme akaona hawa sio samaki wa kawaida. Akaagiza mvuvi aletwe. Alipokuja mvuvi akamweleza nataka unipeleke nikapaone hapo unapovua samaki hawa. Mvuvu akawaeleza ni bali lamda kwa kesho. Mvuvi alijitetea hivi akiogopa ahadi aliyoekeana na jini

Basi siku iliyofata mfalme akatoka na msafara wake kuelekea kule kwenye bwawa. Wakafika mida ya mchana, kwenye bwawa lililozungukwa na milima minne. Watu wote walistaajabu kuona bwawa likiwa milimani na lina maji masafi sana kiasi kile. Kila mmoja alitamani luyaonja maji yale. Ilipofika jioni mfalme akamwagiza mlinda mlango kuwa anatoka lakini asimwambie mtu yeyote. Na atakaemuuliza mwambie amesema hataki kusumbuliwa. Basi mambo yakawa kama hivi.

Usiku ule mfalme alitoka na upanga wake akiwa anazunguruka katika eneo lile, alikuwa akisaidiwa na mwanga wa mwezi ulioonekana unawaka sana. Katika kuzunguruka akaona kinjia kidogo kinaelekea upande wa ashariki kutokea kwenye ziwa. Akafata njia ile akakutana na bostani nzuri, yenye maua na matuta mazuri sana. Alistaajabishwa na bostani ile yenye vitu vizuri ambavyo kwenye ufalme wake havipo. Kwa sahuku aliendelea kuchunguza ndani mule kuona maajabu zaidi.

Kwa muda mrefu katika kuzunguka kwake alikutana na geti kubwa la rangi ya dhahabu, akaingia kupitia geti hili. Akakutana na njia iliyowekwa taizi za almasi. Alishangazwa na ururi ulioje wa njia hiyo. Mbele yake akakutana na kitu kizuri, kiti hiki kimenakshiwa dhahabu na fedha. Kuangalia vizuri akaona kwenye kiti kiel kuna mtu amekaa. Mtu huyu ni wa ajabu sana, alikuwa ni jiwe kwa chini mapaka kiunono. Kuanzia kiunini mpaka juu ni mtu aliye sawa.

Kwa shauku mfalme akataka kujuwa nini kunaendelea eneo lile. Akawa anamuuliza kuhusu yeye ni nani na anafanya nini pale. Na ni kipi kimetokea eneo lile. Maswali yote aliuliza bila ya kujibiwa. Kijana yule alikuwa anatokwa na machozi muda wote ule. Kisha kijana akaanza kuzungumza โ€œhayo maji unayoyaona sio maji, na hao samaki unaowaona ni watu. Hiyo milima ni visiwa na mimi ndiye mfalme wa eneo hiliโ€ ni maneno ya kijana aliye jiwe nusu. Mfalme akauliza nini kilitokea sasa. Kijana akaanza kusimulia hadithi ya eneo hili kama ifuatavyo;-


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aliflela1 Main: Burudani File: Download PDF Views 2274

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰2 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰5 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

SAFARI YA KWANZA YA SINBAD

Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA KWANZA YA SINBAD Tambua kuwa baba yangu alikuwa ni mfanya biashara mkubwa sana katika nchi ya baghdad wakati wa utawala wa sultan harun Rashid.

Soma Zaidi...
SAFARI YA PILI YA SINBAD

Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA PILI YA SINBAD Basi siku ile Sinbad mbeba mizigo aliwahi haraka sana na mapema zaidi, na akamkuta Sinbad wa baharini ameshakaa na watu wake wanamsubiri kuanza hadithi.

Soma Zaidi...
USULUHISHWAJI KWA WALODHULUMIWA

Download kitabu Hiki Bofya hapa USULUHISHAJI WA WALODHULUMIWA.

Soma Zaidi...
Hadithi ya chongo wa kwanza mtoto wa mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
MFUGAJI NA MKEWE

Download kitabu Hiki Bofya hapa KISA CHA MFUGAJI NA MKEWE.

Soma Zaidi...
HADITHI YA KISIWA CHA MAWE YANAYOLIA

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YAKISIWA CHA MAWE YANAYOLIA.

Soma Zaidi...
Hadithi ya waziri aliyeadhibiwa

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
HADITHI YA MJI ULOGEUZWA MAWE

Download kitabu Hiki Bofya hapa HDITHI YA MJI ULOGEUZWA MAWE.

Soma Zaidi...
Kuelekea bonde la uokozi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad

Soma Zaidi...