Trojan ni Moja ya maneno tunayoyasikia sana kwneye tehama. Leo nitakupa maana yake
Trojan ni aina ya programu hasidi (malware) inayojificha kama programu halali au muhimu ili kuingia kwenye kifaa chako bila wewe kujua. Baada ya kuingia, Trojan hutekeleza shughuli mbaya kama:
1. Kuiba taarifa - kama nywila, data za kifedha, au taarifa binafsi.
2. Kufungua mlango wa nyuma - kuruhusu wadukuzi kudhibiti kifaa chako kwa mbali.
3. Kuenea kwa virusi vingine - kusaidia kusambaza malware nyingine.
4. Kuharibu data - kufuta au kubadilisha faili zako muhimu.
5. Kufuatilia shughuli zako - kama kuandika kila unachotype (keylogging).
Trojan hupatikana mara nyingi kupitia viambatisho vya barua pepe, faili zilizopakuliwa kutoka kwa vyanzo visivyo salama, au hata programu zilizodukuliwa. Ili kujilinda, hakikisha unatumia antivirus yenye nguvu na unapakua tu programu kutoka kwa vyan
zo vya kuaminika.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Virusi vya kompyuta ni programu hasidi (malware) inayojishikiza kwenye faili au programu halali na kujiendesha pale faili hiyo inapofunguliwa. Virusi vinaweza kuharibu data, kupunguza kasi ya kompyuta, au kusababisha upotevu wa taarifa.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza kuhusu tofauti ya programmer na developer
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu HDD (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive)
Soma Zaidi...Post hii utakwenda kujikitabzaidi kujibu swali, hata hivyo itambulike kuwa wengi wa wanasayansi waliohusika kwenye lugha hizi sio wamarekani.
Soma Zaidi...Hapa tunajadili sababu kuu zinazoifanya simu iwe rahisi kudukuliwa, mbinu zinazotumiwa na wadukuzi, na mambo ya kawaida ambayo watumiaji hufanya bila kujua na kujipeleka kwenye hatari.
Soma Zaidi...Katika kompyuta, worm ni aina ya programu hasidi (malware) inayojinakili yenyewe na kusambaa kupitia mitandao bila kuhitaji kushikamana na faili au programu nyingine. Tofauti na virusi, worm husambaa haraka zaidi na mara nyingi hutumia mtandao kuenea.
Soma Zaidi...