Katika post hii utakwenda kujifunza maana ya neno firewall
Firewall ni kifaa au programu ya usalama inayotumika kudhibiti na kuchuja mawasiliano yanayopita kati ya kompyuta (au mtandao) na nje ya mfumo huo — iwe ni mtandao mwingine au intaneti.
Kwa lugha rahisi, firewall ni kama mlinzi wa lango la mtandao, ambaye anaangalia kila mawasiliano yanayoingia au kutoka, kisha anaamua kuruhusu au kuyazuia kulingana na sheria zilizowekwa.
Firewall ya Vifaa (Hardware Firewall)
Hii ni kifaa maalum kinachowekwa kati ya mtandao wa ndani (kama wa ofisi) na intaneti.
Mfano: Router yenye firewall iliyojengwa ndani.
Firewall ya Programu (Software Firewall)
Hii huwekwa moja kwa moja kwenye kompyuta au seva.
Inaweza kudhibiti programu fulani zisifungue mawasiliano yasiyotakiwa.
Kuzuia virusi na mashambulizi ya nje (hacking)
Kuzuia programu zisizoruhusiwa kuwasiliana na nje
Kuruhusu huduma au trafiki salama pekee
Kusaidia kuzuia udukuzi (cyber attacks)
Ukifungua tovuti yenye virusi, firewall inaweza kuizuia kuwasiliana na kompyuta yako.
Kama programu kwenye kompyuta yako inajaribu kutuma data bila ruhusa, firewall inaweza kuizuia.
Umeionaje Makala hii.. ?
Zani ilikuwa sehemu ya ku comment ni muhimu sana kwenye blog, ila Sasa sehemu hii imeondolewa kwenye blog nyingi. Ni Kwa nini hasa imeondolewa. Post hii itakujibu swali hilo
Soma Zaidi...Virusi vya kompyuta ni programu hasidi (malware) inayojishikiza kwenye faili au programu halali na kujiendesha pale faili hiyo inapofunguliwa. Virusi vinaweza kuharibu data, kupunguza kasi ya kompyuta, au kusababisha upotevu wa taarifa.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu HDD (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive)
Soma Zaidi...Blogger na WordPress ni majukwaa maarufu ya kuunda blogu na tovuti. Blogger ni huduma ya bure inayomilikiwa na Google, rahisi kutumia lakini ina mipaka katika uhariri na udhibiti. WordPress ni jukwaa lenye uhuru mkubwa wa kubinafsisha tovuti, lenye toleo la bure (WordPress.com) na la kujitegemea (WordPress.org).
Soma Zaidi...Hapa tunajadili sababu kuu zinazoifanya simu iwe rahisi kudukuliwa, mbinu zinazotumiwa na wadukuzi, na mambo ya kawaida ambayo watumiaji hufanya bila kujua na kujipeleka kwenye hatari.
Soma Zaidi...RAM (Random Access Memory) na ROM (Read-Only Memory) ni aina za kumbukumbu kwenye kompyuta au vifaa vya kielektroniki, lakini zina malengo na tabia tofauti.
Soma Zaidi...Leo tutajifunza sababu zinazoifanya simu kuwa rahisi kudukuliwa na hatua madhubuti za kuzuia udukuzi. Tutazungumza kuhusu matumizi salama ya intaneti, usimamizi wa apps, usalama wa akaunti, pamoja na tabia muhimu za kujikinga.
Soma Zaidi...Server ni kompyuta au mfumo unaotoa huduma au rasilimali kwa kompyuta na vifaa vingine kupitia mtandao. Zinaweza kutoa huduma kama kuhifadhi data, kuendesha tovuti, kusambaza faili, au kushughulikia barua pepe.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza kuhusu tofauti ya programmer na developer
Soma Zaidi...Thibitisha akaunti yako kwa hatua za usalama kama kutumia nenosiri imara, kuweka uthibitisho wa hatua mbili (2FA) kwa kutumia authenticator, kukagua matumizi ya vifaa vilivyoingia (logged in devices), kuondoa apps zisizo za lazima, na kuzuia ulaghai (phishing). Hatua hizi zinaongeza sana ulinzi na kupunguza hatari ya kudukuliwa.
Soma Zaidi...