Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu HDD (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive)
HDD vs SSD
HDD (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive) ni aina mbili za hifadhi (storage devices) kwenye kompyuta. Zote hutumika kuhifadhi mfumo wa uendeshaji, programu, na faili zako, lakini zinatofautiana kwa teknolojia, kasi, na uimara.
Maana: Hifadhi inayotumia diski za sumaku zinazozunguka (platters) na kichwa cha kusoma/kuandika data.
Kasi: Ni ya kawaida lakini polepole ukilinganisha na SSD (mfano 80 – 160 MB/s).
Uwezo: Mara nyingi ina uwezo mkubwa kwa bei nafuu (500GB – 10TB).
Uimara: Ni dhaifu zaidi kwa mshtuko kwa sababu ina sehemu zinazozunguka.
Muda wa kuishi: Huharibika kirahisi endapo itapigwa au kudondoka.
Bei: Ni nafuu kuliko SSD.
Mfano wa matumizi: Hifadhi ya kompyuta za ofisini au server zenye data kubwa zisizohitaji kasi sana.
Maana: Hifadhi inayotumia chip za flash memory (kama zile za flash drive) bila sehemu zinazozunguka.
Kasi: Ni ya juu sana (mfano 500 MB/s – 3500 MB/s au zaidi kwa NVMe).
Uwezo: Mara nyingi ndogo kuliko HDD kwa bei sawa (256GB – 4TB).
Uimara: Ina nguvu zaidi kwa mshtuko, haina sehemu za kusogea.
Muda wa kuishi: Hudumu vizuri, hasa kwa matumizi ya kawaida, lakini inategemea kiwango cha kuandika data (write cycles).
Bei: Ni ghali zaidi kwa kila GB ukilinganisha na HDD.
Mfano wa matumizi: Laptop za kisasa, kompyuta za michezo (gaming), na kazi zinazohitaji kasi kubwa (mfano video editing).
| Kipengele | HDD | SSD |
|---|---|---|
| Teknolojia | Diski zinazozunguka (platters) | Flash memory |
| Kasi ya kusoma | Polepole (80–160 MB/s) | Haraka (500–3500 MB/s) |
| Uimara | Inaathirika kirahisi na mshtuko | Imara, haina sehemu zinazozunguka |
| Uwezo | Kawaida mkubwa (500GB–10TB) | Kawaida mdogo (256GB–4TB) |
| Bei | Nafuu | Gharama kubwa |
| Matumizi bora | Hifadhi kubwa za data | Kasi ya juu na boot time ya haraka |
Chagua HDD kama unahitaji hifadhi kubwa kwa gharama ndogo.
Chagua SSD kama unataka kasi kubwa, uimara, na ufanisi wa juu, hasa kwa kompyuta zinazotumika kila siku.
Umeionaje Makala hii.. ?
Hapa tunajadili sababu kuu zinazoifanya simu iwe rahisi kudukuliwa, mbinu zinazotumiwa na wadukuzi, na mambo ya kawaida ambayo watumiaji hufanya bila kujua na kujipeleka kwenye hatari.
Soma Zaidi...Tupo katika kipindi ambacho, tafiti nyingi zinahitajika kuhusu athari za AI kwenye ubunifu na taaluma.
Soma Zaidi...Trojan ni Moja ya maneno tunayoyasikia sana kwneye tehama. Leo nitakupa maana yake
Soma Zaidi...Leo tutajifunza sababu zinazoifanya simu kuwa rahisi kudukuliwa na hatua madhubuti za kuzuia udukuzi. Tutazungumza kuhusu matumizi salama ya intaneti, usimamizi wa apps, usalama wa akaunti, pamoja na tabia muhimu za kujikinga.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutaeleza maana ya AMP (Accelerated Mobile Pages), jinsi inavyofanya kazi, faida zake katika SEO, changamoto zake, na njia bora za kuitumia ili kuboresha utendaji wa tovuti yako kwenye injini za utafutaji kama Google.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza utaratibu unaotumiwa kuweka matoleo kwnye software.
Soma Zaidi...Post hii utakwenda kujikitabzaidi kujibu swali, hata hivyo itambulike kuwa wengi wa wanasayansi waliohusika kwenye lugha hizi sio wamarekani.
Soma Zaidi...Ninutani lakini Kuna mafunzo, programmer wote hawatamsahau rafiki huyu
Soma Zaidi...Katika kompyuta, worm ni aina ya programu hasidi (malware) inayojinakili yenyewe na kusambaa kupitia mitandao bila kuhitaji kushikamana na faili au programu nyingine. Tofauti na virusi, worm husambaa haraka zaidi na mara nyingi hutumia mtandao kuenea.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza maana ya neno firewall
Soma Zaidi...