Historia ya adhana na nama ya kuadhini

Historia ya adhana na nama ya kuadhini

Download Post hii hapa

Historia ya adhana na nama ya kuadhini

Adhana na iqama



Katika kutekeleza amali ya kusimamisha swala kwa nyakati zake na hasa za mwanzo, kumewekwa mwito maalum wa kuwakumbusha na kuwafahamisha waumini kuingia kwa kila swala. Mwito huu ni Adhana. Adhana ni miongoni mwa sunnah kubwa kabla ya swala.


Historia ya Adhana



Waislamu walipohamia Madinah walipata hali ya utulivu na amani pamoja na uhuru kamili wa kuabudu. Walipata fursa ya kukutana pamoja kwa swala za jamaa na mashauri mengine yaliyohitajia mkusanyiko wa Waislamu. Hivyo katika hali hii tatizo lililowakabili kwa siku za mwanzo za maisha ya Madinah ni namna ya kuitana kwa mkusanyiko wa swala na mikusanyiko mbali mbali ya Kiislamu. Waliwakuta Mayahudi wakiitana kwa mikusanyiko yao kwa tarumbeta (sauti ya upembe) na Wakristo wakiitana kwa kengele. Namna zote hizi mbili hazikumpendeza Mtume (s.a.w) na Waislamu kwa ujumla. Mtume (s.a.w) aliona kuwa si vyema kuitana kwa mikusanyiko mitakatifu kwa njia hizo za kitwaghuti, bali alipendelea kuwa sauti ya binaadamu ingelitumiwa kufanya kazi hiyo ambayo itaamsha hamasa za waumini na kuleta mwamko mpya wa imani zao na matendo yao. Hali ya mahangaiko ya kutafuta namna ya kuitana inaelezwa vyema katika Hadithi ifuatayo:



Ibn Umar amesimulia kuwa: “Waislamu walipokuja Madina, walikusanyika pamoja kwa swala, na walipendelea kufanya hivyo kwa wakati mmoja, lakini hapakuwa na yeyote wa kuwaita. Siku moja ilibidi w ajadili jam bo hili na baadhi yao w akasem a: “Tutum ie kitu kam a kengele wanayotumia Wakristo na wengine wakasema: Tutumie tarumbeta kama mayahudi. Umar akasema: Kwa nini asichaguliwe mtu akawa anawaita watu kwa ajili ya swala? Mtume (s.a.w) akasema: Oh! Bilali, nenda ukawaite watu kwa Swala”. (Muslim)



Hadithi hii pamoja na maelezo juu ya historia ya Adhana kwa ujumla hufafanuliwa na hadithi nyingi. Katika Hadithi nyingine tunafahamishwa kuwa maoni waliyoyatoa maswahaba kwenye mkutano wao yalifikishwa kwa Mtume (s.a.w) lakini hayakumvutia. Aliona kwamba si sahihi kutumia njia ya kitwaghuti katika miito mitakatifu, bali alikubaliana na Umar (r.a) kuwa sauti ya binaadamu katika wito huu ni bora kuliko chochote kingine. Pia imesimuliwa katika hadithi iliyopokelewa na Imamu Abu Daud kuwa wakati tatizo hili lilipokuwa bado halijapatiwa ufumbuzi, siku moja, swahaba mmoja, Abdullah bin Zayd alikuja kwa Mtume (s.a.w) na kumsimulia:



“Usiku uliopita am enijia ndotoni m tu akishikilia mkononi m wake ken gele na nikamuomba aniuzie; Aliponiuliza, kuwa nataka kufanyia nini chombo kile, nilijibu kuwa, ni cha kuwaitia watu kwenye swala, baada ya kumjibu hivyo alisema: “Siwezi kukufahamisha njia iliyo bora kuliko hiyo? Nilijibu kuwa nilikuwa tayari kumsikiliza aniambie. Hivyo alinifahamishamane


Allaahu Akbaru x 2, Allahu Akbar x 2, Ashhadu anllailaha illallah x2, Ashhadu anllailaha illallah x2, Ashahadu annna Muhammadar-Rasuullullaah x2, Ashahadu annna Muhammadar-Rasuullullaah x2, Hayya ‘alas-swalaat-Hayya ‘alasswalaat x2, Hayya ‘alas-swalaat-Hayya ‘alasswalaat x2, Hayya ‘alal-fallah. Hayya ‘alalfallah x2 Hayya ‘alal-fallah. Hayya ‘alalfallah x2, Allahu Akbaru, allaahu Akbaar, Laaillaaha illaallah.


NB: x2 maana yake Mara mbili


Wakati wa Adhana ya swala ya Asubuhi - Muadhini baada ya kusema Hayya’allal falaah aongeze: Asswalaatu khairum minan-naumi. (mara 2) “Sw ala ni bora kuliko usingizi”. Kisha aendelee Allahu Akbaru hadi mwisho.



Kuitikia Adhana



Ni sunnah kuitikia adhana kama alivyotufundisha Mtume (s.a.w) katika Hadithi ifuatayo:-
Umar (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Muadhini anaposema “Allaahu Akbaru x 2 ”. Mtu aitikie: Allahu Akbar x 2. Kisha anaposema: “Ashhadu anllailaha illallah ”, aitikie: “Ash-hadu anllailaha illallah ”. Kisha anaposema: “Ash-hadu anna Muhammadar-Rasuullullaah” aitikie: “Ashahadu annna Muhammadar-Rasuullullaah ” Anaposema “Hayya ‘alas-swalaat-Hayya ‘alasswalaat”, aseme: “Lahaula walaa Quwwata illa billah” (Hapana hila wala nguvu zinazomkiuka Allah). Kisha akisema: Hayya ‘alal-fallah. Hayya ‘alalfallah ” asema: “Lahaula walaa Quwwata illa billah ”. Kisha akisema: “Allahu Akbaru, allaahu Akbaar, aitikie: “Allaahu akbar Allahu Akbaar”. Kisha anaposema: “Laaillaha illaallah ”, aitikie: “Laaillaaha illaallah ”, akifanya hivyo kwa unyenyekevu na mazingatio ataingia Peponi. (Muslim).



Dua baada ya Adhana



Baada ya adhana kwisha Muislamu anatakiwa amswalie Mtume (s.a.w) kisha aombe dua. Kutokana na hadithi iliyosimuliwa na “Abdullah ibn, Umar (Mtume (s.a.w)) alisema kuwa:-



Ukisikia adhana rudia kama asemavyo muadhini, kisha niswalie mimi mara moja Allah humuongezea rehema (humswalia yeye) mara kumi. Kisha niom bee sehemu ya wasillah. Hii ni sehemu huko Peponi iliyohifadhiwa kwa ajili ya mmoja katika waja wa Allah: nategemea huenda nikawa mimi, na yeyote atakayeniombea Allah anipe afya hiyo ya wasilah basi uombezi wangu utaruhusiwa kwake (siku ya Kiyama). (Muslim).



Allaahuma rabba haadhihid-daawatit-taamma. Wasswalaatil-qaaimah. Ati Muhammadal-wasiilata walfadhiilat Wab-’ath-hu
maqaaman mahmuudanil-ladhii wa’ad-tahu.Innaka laa tukhliful miiaad.



Tafsiri:



“Ewe Allah, Mola wa mlingano huu uliokamilika na swala iliyosimama,Mpe Muhammad (s.a.w) daraja kubwa na enzi na mpe hicho cheo ulichomuahidi, Hakika yako wewe si mwenye kuvunja miadi”. (Bukh ari).



Ni vyema kipindi kati ya adhana na Iqama kiwe kirefu kidogo, kiasi cha kumuwezesha mtu kujitayarisha na kuwahi swala ya jamaa. Hivyo, hapana budi pawe na kipindi cha kuwangojea watu. Kipindi hiki ni kiasi cha kuswali rakaa mbili.



Ames imulia Abdullah bin Mughaffal al-Muzani (r.a): “Kuna swala (sunnah) kati ya Adhana mbili (adhana na iqama) na kaongeza: kwa mtu anayetaka kuswali”.
Pia katika hadithi tunafahamishwa kuwa kipindi kati ya adhana na Iqama ni wakati mzuri wakuomba dua. Anas bin Malik (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema:-
Hairudishwi (haikataliwi) dua, baina ya Adhana na Iqama. (Abu Daud, An-Nisani, tirmidh).



Iqama



Ni wito au amri yakusimama tayari kuanza swala. Utakuta maneno ya Iqamat ni yale yale ya Adhana lakini hutamkwa nusu yake tu isipokuwa neno la mwisho (Laailaaha illa-llahu) ambalo huwa hutamkwa mara moja kuongezea maneno:
Qad qaamat sw-swalat - qad-qaamat sw-swalat (Sw ala ipo tayari).


Haya husemwa baada ya maneno (Njooni katika kheri). Ndivyo tunavyofahamishwa katika Hadithi ifuatayo:
Ibn Umar (r.a) amesimulia kuwa palikuwa na adhana wakati wa Mtume (s.a.w) kila tamko mara mbili na Iqamat mara moja isipokuwa aliongezea kusema: Swala iko tayari. Swala iko tayari. (Abuu Daud, Nisai).
Swala ya Sunnah baada ya Iqamat



Ikisha kimiwa kwa ajili ya swala ya jamaa, hairuhusiwi kuendelea na swala ya sunnah kama tunavyojifunza kutokana na hadith ifuatayo:
“Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Swala ya faradh ikianza,hapana swala nyingine (kuswaliwa ” Na katika riwaya nyingine Mtume (s.a.w) amesema: Sw ala ni ile ambayo imetolewa Iqama ”. (Ahmad, Abu Daud, At-tirmidh, an-Nisai na Ibn Majah).




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1308

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Haki ya kumiliki mali na mipaka yake katika uislamu
Haki ya kumiliki mali na mipaka yake katika uislamu

Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo

Soma Zaidi...
 Riba na Madhara Yake Katika Jamii
Riba na Madhara Yake Katika Jamii

- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.

Soma Zaidi...
Misingi ya fiqh
Misingi ya fiqh

Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu.

Soma Zaidi...
haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu
haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu

Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee.

Soma Zaidi...
Vipi utapata uchamungu kupitia funga
Vipi utapata uchamungu kupitia funga

Vipi lengo la funga litafikiwa na kumfanya mfungaji awe mchamungu.

Soma Zaidi...
 Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
Hadathi ya kati na kati
Hadathi ya kati na kati

Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati.

Soma Zaidi...